• Wasiliana Nasi |
    • Maswali |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Complains |
Karatu District Council
Karatu District Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Karatu

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Dhamira na Dira
    • Historia
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Fedha na Biashara
      • Ujenzi
      • Afya
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
    • Vitengo
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma Zetu
  • Madiwani
  • Miradi
    • TASAF
    • BOOST
  • Machapisho
    • Hali ya Uwekezaji
      • Business License Form
  • Kituo cha Habari
    • Video
    • Habari
    • Hotuba kwa Vyombo vya Habari
    • Maktaba ya Picha

WAKULIMA WAOMBA KIWANDA CHA KUCHAKATA VITUNGUU

Posted on: May 21st, 2019

Rais wa mfuko wa kimataifa na maendeleo ya kilimo (IFAD) Mhe. Gilbert Houngbo ametembelea ghala la wakulima wa vitunguu Mang’ola. Amejionea namna ghala la vitunguu linavyofanya kazi pamoja na kuzungumza na wanachama wa Lake Eyasi Commercial Farmers Networks (LEKOFANET) ambao alitaka kufahamu kuhusu shughuli zao za kilimo. 

 Awali Mkuu wa wilaya ya Karatu Mhe. Theresia Mahongo ameshukuru IFAD kwa kujenga ghala la kuhifadhia vitunguu. Mhe. Theresia amesema ghala limejengwa kwa gharama ya shilingi billion 1.5, mradi wa barabara wa km 27 uliojengwa na Marketing Infrastructure, Value Addition and Rural Finance Support (MIVAF) billion 1.54 IFAD walijenga Barabara ya km 27. Mhe. Mahongo amesema Halmashauri ilichangia 5% kila mradi, halmashauri ilichangia million 74.4 kwenye mradi wa barabara na Mivarf ilichangia billion 1.4, Mradi wa ghala Halmashauri ilichangia million 76.5 na Mivarf ilichangia billion 1.4.

Mhe. Theresia amesema ghala limesaidia sana wakulima kuhifadhi vitungu ili vipande bei, amesema wakulima wa vitunguu Tarafa ya Eyasi wako takribani 1400. Amesema Mwaka 2017 wakati wanaanza kutumia ghala gunia la vitunguu kwa bei ya awali liliuzwa kwa sh.45000 lakini wakulima walipo hifadhi vitunguu kwenye ghala baadae waliuza gunia kwa sh 100000.wakulima hawa waliweza kupata mafunzo ya namna ya kujiendesha wenyewe na wameweza kuunda ushirika ambao uko katika hatua za mwisho ili waweze kusajiliwa. Mhe. Theresia amesema Karatu ni wanufaika wakubwa wa serikali ya awamu ya tano, serikali imetoa zaidi ya shilingi billion 5 kwa elimu bure tangu mwaka 2015 mpaka sasa. Lakini serikali imeweka lami kiasi cha km 0.6 kwa sasa Karatu mjini, Mhe.Theresia amesema serikali itaweka   lami Karatu  mjini km 10 na tayari upembuzi yakinifu umeshafanyika.

Mhe. Ally Lorry mkazi wa Tarafa ya Eyasi amesema ghala limesaidia kuwaondolea matatizo waliokuwa wakiyapata hapo awali. Amesema kulikuwa kuna shida ya ubovu wa barabara zinazotoka mashambani, Mhe. Ally amemuomba Rais wa IFAD kuwatafutia wakulima masoko nje ya nchi,lakini pamoja na kuwatengenezea kiwanda cha kuchakata vitunguu ili zao la vitungu lipate bei nzuri zaidi.

Ndugu Gabriel Boay Mkazi wa Tarafa ya Eyasi amesema wao wanahitaji kupiga hatua katika kilimo cha vitunguu zaidi. Amesema ghala limewasaidia katika shughuli za kilimo cha vitunguu kwa kuongeza dhamani ya vitunguu. Barabara imesaidia kwa wafanyabisahara kutoka nje ya nchi kuja kununua kitunguu Mang’ola. Kutokana na uwekezaji huo wa miundo mbinu wakulima wametoka katika uchumi wa chini na kuelekea hatua ya uchumi wa katikakati.

Rais wa IFAD Mhe.Gilbert Houngbou kushoto na Mkuu wa wilaya ya Karatu Mhe. Theresia Mahongo  wakiangalia vitunguu ambavyo havipo pichani vilivyotandazwa kwenye ghala ili vikauke na kuweka kwenye mifuko tayari kwa kuuza.

Rais wa IFAD Mhe. Gilbert Houngbo kulia pamoja na Mhe. Theresia Mahongo wa pili kutoka kulia wakiangalia shamba la vitunguu Mang'ola.

Matangazo

  • Matokeo ya upimaji wa Kitaifa kidoto cha pili January 07, 2024
  • Halmashauri ya Wilaya ya Karatu Uchaguzi wa Wanafunzi wa kidato cha kwanza, 2024 December 18, 2023
  • Matokeo ya Darasa la Nne January 07, 2024
  • NAFASI ZA KAZI 2024 April 21, 2024
  • Angalia Zote

Taarifa Mpya

  • MILIONI 400 ZATOLEWA KARATU, KUJENGA MABWENI NA MADARASA EYASI SEKONDARI

    January 30, 2025
  • WASIMAMIZI WAASWA KUSIMAMIA VIAPO VYAO KUELEKEA UCHAGUZI WA SERIKALI ZA MITAA 2024.

    November 23, 2024
  • JESHI LA AKIBA MKAWE WAZALENDO KWA TAIFA

    November 23, 2024
  • HALMASHAURI YAZINDUA KITABU CHA MPANGO MKAKATI WA UKUSANYAJI MAPATO.

    November 19, 2024
  • Angalia Zote

Video

DC KOLIMBA ATATUA KERO TARAFA YA EYASI KARATU
Video Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fursa za Uwekezaji

Viunganishi Linganifu

  • Tovuti ya Wizara ya Fedha na Mipango
  • Jamvi la Habari
  • Tovuti ya Tamisemi
  • Tovuti ya Serikali
  • Sekretarieti ya Ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Location Map

Wasiliana Nasi

    Karatu District Council

    Sanduku la Posta: P.O Box 190

    Simu: +255 272970648

    Simu ya Mkononi: 0754773947

    Barua Pepe: ded@karatudc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Haki Miliki @ 2017 Halmashauri ya Wilaya ya Karatu.Haki zote zimehifadhiwa