• Wasiliana Nasi |
    • Maswali |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Complains |
Karatu District Council
Karatu District Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Karatu

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Dhamira na Dira
    • Historia
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Fedha na Biashara
      • Ujenzi
      • Afya
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
    • Vitengo
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma Zetu
  • Madiwani
  • Miradi
    • TASAF
    • BOOST
  • Machapisho
    • Hali ya Uwekezaji
      • Business License Form
  • Kituo cha Habari
    • Video
    • Habari
    • Hotuba kwa Vyombo vya Habari
    • Maktaba ya Picha

KAMATI ZA UJENZI SIMAMIENI UJENZI KWA UKAMILIFU

Posted on: September 10th, 2021

Na Tegemeo Kastus

Msisitizo  watolewa kwa kamati za ujenzi kuongeza uwajibikaji katika miradi ya ujenzi iliyo katika maeneo husika. Lengo likiwa ni kuhakikisha miradi inasimamiwa kuanzia mwanzo wa ujenzi wa msingi na kufuata miongozo ya ujenzi iliyotolewa na serikali. Ujenzi wa miradi hiyo unapokamilika unatakiwa  uendane na thamani ya fedha iliyowekwa.

Hayo yamejiri katika ziara ya Mkuu wa wilaya ya Karatu Mh. Abbas Kayanda alipotembelea miradi ya ujenzi inayoendelea katika shule za msingi wilayani Karatu. Katika ziara hiyo Mh. Kayanda ametembelea shule ya msing G-Arusha iliyopewa kiasi cha million 40 kwa ajili ya ujenzi wa  vyumba viwili vya darasa. Ameelekeza kamati ya ujenzi kusimamia vyema ujenzi  na kuhakikisha fundi anaongeza nguvu kazi ili ujenzi wa vyumba hivyo vya darasa viweze kukamilika katika muda ulioainishwa kwenye mkataba wa ujenzi.

Mh. Kayanda (kushoto) katika eneo la ujenzi wa vyumba viwili vya madarasa s/m G-Arusha

Katika ziara hiyo Mh. Kayanda ametembelea shule ya msingi Karatu na kukagua ujenzi wa darasa lilojengwa na mfadhili mpaka hatua ya lenta na kuweka madirisha na milango. Katika ujenzi huo serikali imetoa kiasi cha million 12 kwa ajili ya kukamilisha ujenzi wa darasa. Sambamba na kutembelea ujenzi wa chumba hicho cha darasa ameelekeza uongozi wa shule ya msingi Karatu kutoa taarifa ya mchanganuo wa fedha za ujenzi ulivyotumika.

Akiwa katika shule ya msingi Kainam Rhotia Mh. Kayanda ametembelea ujenzi wa madarasa mawili na ofisi yanayojengwa na mdau wa elimu Kamitei foundation. Madarasa hayo mawili yapo katika hatua za umaliziaji na yanatarajiwa kuisha mwishoni mwa mwezi ujao Mh. Kayanda ametembelea ujenzi wa vyumba vingine viwili vya madarasa ambavyo vinafanyiwa ukarabati na wadau wa elimu Kamitei foundation. Amepongeza jitihada hizo za wadau wa elimu zinazofanywa katika shule ya Kainam rhotia ambazo zimelenga kuboresha miundo mbinu ya elimu.

Mh. Kayanda akiwa katika darasa lililomaliziwa kujengwa shule ya msingi Karatu.

 Katika hatua nyingine Mh. Kayanda ametembelea shule ya msingi Hareahbi na kujionea ujenzi wa nyumba ya walimu two in one inayojengwa na wadau wa elimu Kamitei foundation. Ujenzi huo umefika katika hatua ya lenta na unatarajiwa kuisha mwishoni mwa mwezi wa kumi. Mh. Kayanda ameonesha kuridhishwa na kasi ya ujenzi wa nyumba hizo. Katika hatua nyingine Mh. Kayanda ametoa kiasi cha mifuko 20 ya saruji kwa ajili ya umaliziaji wa ujenzi wa boma la darasa katika shule ya msingi Hareahbi.

Katika ziara hiyo Mhandisi wa ujenzi, Ndg. Riziki Msite ametoa maelekezo kwa kamati za ujenzi kutoa taarifa kwa mhandisi wa wilaya wa kila hatua ya ujenzi inayofanyika. Ili Mhandisi athibitishe na kujiridhisha na aweze kutoa idhini ya  mafundi kuendelea na hatua nyingine za ujenzi. Amesema lengo ni kuhakikisha hakuna makosa yanafanyika ili ujenzi uendane vigezo vilivyotolewa na serikali. Katika ziara hiyo Mhandisi Msite ametoa maelekezo mbalimbali ambayo mafundi ujenzi wanapaswa kuyazingatia ili kutimiza vigezo vya ujenzi katika miradi.

Muonekano wa nyumba ya walimu two in Hareahbi

Matangazo

  • Matokeo ya upimaji wa Kitaifa kidoto cha pili January 07, 2024
  • Halmashauri ya Wilaya ya Karatu Uchaguzi wa Wanafunzi wa kidato cha kwanza, 2024 December 18, 2023
  • Matokeo ya Darasa la Nne January 07, 2024
  • KIKAO CHA BARAZA LA MADIWANI 2024 May 11, 2024
  • Angalia Zote

Taarifa Mpya

  • MAAFISA UANDIKISHAJI WALA KIAPO KARATU

    May 14, 2025
  • DED HOKORORO ASHIRIKI KIKAO CHA ALAT WILAYA YA MERU

    May 15, 2025
  • MADAKTARI BINGWA WA SAMIA AWAMU YA TATU WATUA KARAU

    May 12, 2025
  • KARATU WASAPOTIJUHUDI ZA RAIS SAMIA WATANGAZA UTALII WA NDANI

    May 11, 2025
  • Angalia Zote

Video

DC KOLIMBA ATATUA KERO TARAFA YA EYASI KARATU
Video Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fursa za Uwekezaji

Viunganishi Linganifu

  • Tovuti ya Wizara ya Fedha na Mipango
  • Jamvi la Habari
  • Tovuti ya Tamisemi
  • Tovuti ya Serikali
  • Sekretarieti ya Ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Location Map

Wasiliana Nasi

    Karatu District Council

    Sanduku la Posta: P.O Box 190

    Simu: +255 272970648

    Simu ya Mkononi: 0754773947

    Barua Pepe: ded@karatudc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Haki Miliki @ 2017 Halmashauri ya Wilaya ya Karatu.Haki zote zimehifadhiwa