• Wasiliana Nasi |
    • Maswali |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Complains |
Karatu District Council
Karatu District Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Karatu

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Dhamira na Dira
    • Historia
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Fedha na Biashara
      • Ujenzi
      • Afya
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
    • Vitengo
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma Zetu
  • Madiwani
  • Miradi
    • TASAF
    • BOOST
  • Machapisho
    • Hali ya Uwekezaji
      • Business License Form
  • Kituo cha Habari
    • Video
    • Habari
    • Hotuba kwa Vyombo vya Habari
    • Maktaba ya Picha

SIMPA, AHIDI UTENGENEZAJI WA BARABARA YA LOSITETE

Posted on: May 1st, 2020

Na Tegemeo Kastus

Wananchi wanaotegemea usafiri wa umma kutoka na kuingia kata ya Mbulumbulu watakiwa kuvaa barakoa ili kuzuia kusambaa na kujikinga na virusi vya corona. Azimio hilo limeafikiwa na wajumbe wa kikao cha maendeleo ya kata wakati wakiajadili janga la virusi vya corona.

Kikao hicho cha maendeleo ya kata  kimefanyika katika makao makuu ya kata ya Mbulumbulu, pamoja na hatua hizo kikao kimeazimia kufunga sehemu zinazouza pombe za kienyeji, sehemu zinazohusika na uchezaji wa Pooltable na Karata kwa kipindi hiki cha janga la corona. Kikao hicho pia kimejadili desturi ya watu kulala wengi kwenye kirago kimoja na kuazimia kujikita katika kuelimisha jamii kuchukua tahadhari katika sehemu za kulala kwa kuacha tabia ya watu kulala wengi katika kirago kimoja.

Mhe. Elias Simpa amesema bado wananchi hawajahamasika kunawa mikono mara kwa mara amesema ni vyema tukahamasisha wananchi wapate muamko wa kunawa kwa maji yanayotiririka na sabauni. Mhe. Simpa amesema kuhamasisha kila familia iwe na sehemu ya kunawa mikono kwa maji tiririka na sabauni sambamba na hilo ametoa rai kwa wananchi juu ya shughuli za misiba. Amesema ili kupunguza uwezekano wa kupata maambukizi, Halmashauri imetoa maelekezo angalau wingi wa watu kwenye msiba usizidi watu 30.

Mhe. Simpa ametoa hofu wajumbe juu ya maendeleo ya ujenzi wa barabara amesema katika ujenzi wa barabara bado mkandarasi yupo eneo la kazi  na amesimama kutokana na mvua kubwa zinazoendelea. Amesema anaendelea kufanya mawasiliano na wadau mabalimbali ili kuunganisha nguvu katika kutenengeneza barabara katika maeneo ambayo mkandarasi hatafika hasa barabara za makao makuu ya kata pamoja na barabara ya Lositete mpaka makao makuu ya kata.

Mwenyekiti wa kikao cha maendeleo ya kata ya Mbulumbulu Mhe.Elias Simpa  akisisitiza jambo

Naye Mtendaji kata wa Mbulumbulu Ndg Elikana Sulumbu amesema eneo la kilimamoja limekuwa maarufu kwa utengenezaji wapombe haramu gongo. Amesema vita ya kongo ni vita ya muda mrefu, walishawahi kukamata lita zaidi ya 300 kijiji cha Slahhamo na kumwaga pombe hiyo kwenye mkutano mkuu wa kijiji. Lakini bado juhudi hizo zimekuwa zikipata upinzani mkubwa kutoka kwa watengenezaji hao wa pombe. Amesema pombe ya gongo inadhoofisha afya ya mwili, amesema hizi pombe za kienyeji za kawaida zinachanganywa na gongo ili kuongeza kilevi zaidi.

Pombe hiyo imekuwa ikisafirishwa kwa njia za uchochoro na kuibeba kwa vifungashio tofauti tofauti ili kujenga mazingira ya usiri katika usafirishaji. Ndg. Sulumbu amesema wenyeviti wa vitongoji wanapaswa kuanza kudhibiti kwenye maeneo yao ili isisambae kwenye maeneo mengine.  Kuna orodha ya watu sugu ambao wameshakamatwa mara kwa mara kwa kujihusisha na matukio ya gongo, kikao hicho cha maendeleo ya kata kimeazimia kuanza na orodha hiyo kwa umakini mkubwa wa kutengeneza ushahidi na kuwapeleka mahakani badala ya kutegemea jeshi la polisi.

Wajumbe wa kikao wamebaini namna jeshi la polisi, linavyowarudisha nyuma katika vita ya kukabiliana na gongo. Wajumbe wamesema Lositete kunamitambo midogo midogo ambayo inatengeneza gongo kali ile inayosisimua ubongo haraka. Biashara hiyo ya gongo imekuwa kama mtaji kwa jeshi la polisi, ambao hukamata watuhumiwa wa gongo na kuwachia bila hatua za kisheria kuchukuliwa zaidi. Kikao hicho kimeazimia kushirikisha jamii ili iweze kulaani matumizi ya pombe hiyo ya kienyeji, wakati hatua zaidi zikiendelea kuchukuliwa na viongozi katika ngazi mbalimbali.

Matangazo

  • Matokeo ya upimaji wa Kitaifa kidoto cha pili January 07, 2024
  • Halmashauri ya Wilaya ya Karatu Uchaguzi wa Wanafunzi wa kidato cha kwanza, 2024 December 18, 2023
  • Matokeo ya Darasa la Nne January 07, 2024
  • NAFASI ZA KAZI 2024 April 21, 2024
  • Angalia Zote

Taarifa Mpya

  • MILIONI 400 ZATOLEWA KARATU, KUJENGA MABWENI NA MADARASA EYASI SEKONDARI

    January 30, 2025
  • WASIMAMIZI WAASWA KUSIMAMIA VIAPO VYAO KUELEKEA UCHAGUZI WA SERIKALI ZA MITAA 2024.

    November 23, 2024
  • JESHI LA AKIBA MKAWE WAZALENDO KWA TAIFA

    November 23, 2024
  • HALMASHAURI YAZINDUA KITABU CHA MPANGO MKAKATI WA UKUSANYAJI MAPATO.

    November 19, 2024
  • Angalia Zote

Video

DC KOLIMBA ATATUA KERO TARAFA YA EYASI KARATU
Video Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fursa za Uwekezaji

Viunganishi Linganifu

  • Tovuti ya Wizara ya Fedha na Mipango
  • Jamvi la Habari
  • Tovuti ya Tamisemi
  • Tovuti ya Serikali
  • Sekretarieti ya Ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Location Map

Wasiliana Nasi

    Karatu District Council

    Sanduku la Posta: P.O Box 190

    Simu: +255 272970648

    Simu ya Mkononi: 0754773947

    Barua Pepe: ded@karatudc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Haki Miliki @ 2017 Halmashauri ya Wilaya ya Karatu.Haki zote zimehifadhiwa