• Wasiliana Nasi |
    • Maswali |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Complains |
Karatu District Council
Karatu District Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Karatu

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Dhamira na Dira
    • Historia
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Fedha na Biashara
      • Ujenzi
      • Afya
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
    • Vitengo
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma Zetu
  • Madiwani
  • Miradi
    • TASAF
    • BOOST
  • Machapisho
    • Hali ya Uwekezaji
      • Business License Form
  • Kituo cha Habari
    • Video
    • Habari
    • Hotuba kwa Vyombo vya Habari
    • Maktaba ya Picha

AFISA ELIMU ABAINI UDHAIFU MKUBWA WA KITAALUMA QANGDEND

Posted on: July 10th, 2019

Afisa elimu sekondari ameanza ziara ya kutembelea shule zote za sekondari wilayani Karatu. Ziara hiyo imejikita katika kuangalia na kukagua mikakati ishirini na tano aliyowaelekeza walimu wa sekondari kama inatekelezwa. Lakini pia kuangalia jitihada na ufanisi wa walimu katika kuinua kiwango cha kitaaluma.

Katika ziara hiyo ambayo amefanya Tarafa ya Eyasi  ameambatana na watendaji wa wilaya wa idara ya elimu sekondari wa ngazi ya wilaya. Bi, Kalista  Maina akiwa sekondari ya Qangdend amebaini udhaifu mkubwa wa kiufundishaji kwa walimu wa shule hiyo. Bi, Maina amesema walimu hao hawajishughulishi na kuandaa andalio la somo darasani lakini pia kuna udhaifu mkubwa wa ujazaji wa (class journal) daftari la kusaini walimu wanapofundisha au kuingia darasani.

Afisa elimu Bi, Maina amesema walimu wa shule hiyo hawafuatilii maelekezo aliyoyatoa ya kuzingatia mikakati ya ishirini na tano aliyotoa. Bi, Maina amesema faili la akiba ya maswali ya mitihani ya kitaifa hawana ya kujitosheleza, hawafuatili notice wanazowapa wanafunzi. Mahudhurio ya kusuasua kwa walimu, na kuzembea kujaza kitabu cha kujaza mahudhurio ni moja ya dosari za wazi wazi zilizoonekana. Katika ziara hiyo walimu wawili hakukukutwa katika kituo cha kazi, na ruhusa zao za kutokuwepo kazini zimeweka mashaka.

 Afisa elimu sekondari kulia, Bi Maina katika  ukaguzi

Bi. Maina amesema shule ya Qangdend imekuwa ya 32 na ya Mwisho kwa matokeo ya mtihani wa Moko na imekuwa shule ya 224 kati ya 226 za mkoa wa Arusha. Bi, Maina amesema walimu wa shule hiyo hawajali ufundishaji na matokeo yake watoto wamekuwa na ufaulu duni. Bi, Maina amesema shule hiyo ina walimu watatu ambao watoto wamepata ” F” darasa zima katika mtihani wa Moko kidato cha nne. Walimu  hao ni mwalimu wa historia, hesabu, na biology.

Bilogy  kwa muhula uliopita wa masomo, kuna vipindi 52 kwa kidato cha kwanza, na vipindi 34 havijafundishwa kwa kidato cha pili na kidato cha tatu vipindi 14 jumla kufika vipindi 100. Vipindi vya historia kidato cha kwanza 33 na vipindi vya kidato cha pili 14 kidato cha tatu kidato 11 na kidato cha nne 10 kufika jumla ya vipindi 68 ambavyo havijafundishwa. Vipindi vya hesabu ambavyo havijafundishwa  kwa kidato cha pili ni 24 na  kidato cha tatu ni vipindi 8  na kidato cha nne 10 hivyo kufanya vipindi kufika 42 kwa muhula uliopita.

Bi, Maina amesema kwa hali jinsi ilivyo taarifa ataipelekea kwa Mkurugenzi, ambaye ni mwajiri wa watumishi. Ili aweze kuchukua hatua stahiki za kinidhamu, ameongeza kusema kutokufundiha na kuanda andalio la somo ni kosa ambalo linaweza kukusababisha kufukuzwa kazi. Bi. Maina amesema hatuwezi kulaumu watoto tu wakati ufundishaji wa walimu unasuasua.

Matangazo

  • Matokeo ya upimaji wa Kitaifa kidoto cha pili January 07, 2024
  • Halmashauri ya Wilaya ya Karatu Uchaguzi wa Wanafunzi wa kidato cha kwanza, 2024 December 18, 2023
  • Matokeo ya Darasa la Nne January 07, 2024
  • KIKAO CHA BARAZA LA MADIWANI 2024 May 11, 2024
  • Angalia Zote

Taarifa Mpya

  • MAAFISA UANDIKISHAJI WALA KIAPO KARATU

    May 14, 2025
  • DED HOKORORO ASHIRIKI KIKAO CHA ALAT WILAYA YA MERU

    May 15, 2025
  • MADAKTARI BINGWA WA SAMIA AWAMU YA TATU WATUA KARAU

    May 12, 2025
  • KARATU WASAPOTIJUHUDI ZA RAIS SAMIA WATANGAZA UTALII WA NDANI

    May 11, 2025
  • Angalia Zote

Video

DC KOLIMBA ATATUA KERO TARAFA YA EYASI KARATU
Video Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fursa za Uwekezaji

Viunganishi Linganifu

  • Tovuti ya Wizara ya Fedha na Mipango
  • Jamvi la Habari
  • Tovuti ya Tamisemi
  • Tovuti ya Serikali
  • Sekretarieti ya Ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Location Map

Wasiliana Nasi

    Karatu District Council

    Sanduku la Posta: P.O Box 190

    Simu: +255 272970648

    Simu ya Mkononi: 0754773947

    Barua Pepe: ded@karatudc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Haki Miliki @ 2017 Halmashauri ya Wilaya ya Karatu.Haki zote zimehifadhiwa