• Wasiliana Nasi |
    • Maswali |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Complains |
Karatu District Council
Karatu District Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Karatu

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Dhamira na Dira
    • Historia
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Fedha na Biashara
      • Ujenzi
      • Afya
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
    • Vitengo
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma Zetu
  • Madiwani
  • Miradi
    • TASAF
    • BOOST
  • Machapisho
    • Hali ya Uwekezaji
      • Business License Form
  • Kituo cha Habari
    • Video
    • Habari
    • Hotuba kwa Vyombo vya Habari
    • Maktaba ya Picha

RC MAKALLA AISHAURI TUME YA TAIFA YA UMWAGILIAJI KUFANYA MAAMUZI KWA MKANDARASI BWAWA LA EYASI.

Posted on: September 23rd, 2025


Mkuu wa Mkoa wa Arusha Mhe. CPA Amos Gabriel Makalla ameitaka Tume ya Taifa ya Umwagiliaji kufanya maamuzi na majadiliano ya haraka na Mkandarasi Tunnel Sadd Ariana kutoka Nchini Iran anayetekeleza ujenzi wa Bwawa la Eyasi Wilayani Karatu, ili kujua hatma ya utekelezaji wa mradi huo unaosuasua kwa kipindi kirefu.

Mhe. Makalla amebainisha hayo Jumanne Septemba 23, 2025 alipofanya ziara ya kukagua utekelezaji wa mradi huo, akionesha kusikitishwa na kusuasua kwake ambapo mpaka sasa mradi huo umefikia asilimia nne pekee ya utekelezaji wake ilihali ulitakiwa kuwa umefikia asilimia 90 kufikia hivi sasa huku pande zote za Mkandarasi na Tume wakiwa na sababu tofauti kama sehemu ya vikwazo vinavyokwamisha utekelezaji wake.

“Mimi kama Mkuu wa Mkoa na Mwenyekiti wa Kamati ya usalama nishauri na kupendekeza kwa Tume kwamba mkae na Mkandarasi kama hana sifa ya kuendelea ni bora mkawa na makubaliano ya pande zote mbili tukaachana na tukatafuta Mkandarasi mwingine. Wananchi wana matarajio na mradi huu hivyo jambo hili lifanyike kwa haraka.” Amesema Mhe. Makalla akisisitiza kuzingatiwa kwa taratibu za kisheria katika majadiliano yao.


Awali katika maelezo yake, Mhe. Mkuu wa Mkoa akizungumza na Maofisa wa Tume ya Umwagiliaji pamoja

na Wakandarasi hao ameeleza kuwa serikali imetenga

Bilioni 21 na Milioni 831 katika kutekeleza mradi wa bwawa hilo ili kuondoa changamoto ya mafuriko kwenye Kata za

Mang’ola na Baray za Wilayani Karatu Mkoani Arusha pamoja na kuzisaidia Kata hizo katika kuimarisha Kilimo cha Umwagiliaji.


Kwa upande wake Bw. Leopard Lunji, Mkurugenzi wa Idara ya miundombinu kutoka Tume ya Taifa ya Umwagiliaji

amemueleza Mhe. Makonda kuwa ndani ya wiki mbili zijazo wataketi na Mkandarasi huyo ili kufanya makubaliano ya pamoja katika kutekeleza maagizo na maelekezo ya Mhe.Makalla ili wananchi waweze kunufaika na mradi huo kwa wakati

Matangazo

  • Wasimamizi, Wasaidizi, na Makarani wa Vituo October 06, 2025
  • Halmashauri ya Wilaya ya Karatu Uchaguzi wa Wanafunzi wa kidato cha kwanza, 2024 December 18, 2023
  • Matokeo ya Darasa la Nne January 07, 2024
  • KIKAO CHA BARAZA LA MADIWANI 2024 May 11, 2024
  • Angalia Zote

Taarifa Mpya

  • RC MAKALLA AISHAURI TUME YA TAIFA YA UMWAGILIAJI KUFANYA MAAMUZI KWA MKANDARASI BWAWA LA EYASI.

    September 23, 2025
  • WAKULIMA MANG’OLA WAMSHUKURU RAIS SAMIA KWA MRADI WA UMWAGILIAJI

    September 23, 2025
  • WENYE SIFA WATAKIWA KUOMBA MIKOPO HALMASHAURI

    September 24, 2025
  • UKUSANYAJI WA MAPATO UNAZIDI KUONGEZEKA KARATU

    September 24, 2025
  • Angalia Zote

Video

DC KOLIMBA ATATUA KERO TARAFA YA EYASI KARATU
Video Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fursa za Uwekezaji

Viunganishi Linganifu

  • Tovuti ya Wizara ya Fedha na Mipango
  • Jamvi la Habari
  • Tovuti ya Tamisemi
  • Tovuti ya Serikali
  • Sekretarieti ya Ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Location Map

Wasiliana Nasi

    Karatu District Council

    Sanduku la Posta: P.O Box 190

    Simu: +255 272970648

    Simu ya Mkononi: 0754773947

    Barua Pepe: ded@karatudc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Haki Miliki @ 2017 Halmashauri ya Wilaya ya Karatu.Haki zote zimehifadhiwa