• Wasiliana Nasi |
    • Maswali |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Complains |
Karatu District Council
Karatu District Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Karatu

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Dhamira na Dira
    • Historia
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Fedha na Biashara
      • Ujenzi
      • Afya
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
    • Vitengo
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma Zetu
  • Madiwani
  • Miradi
    • TASAF
    • BOOST
  • Machapisho
    • Hali ya Uwekezaji
      • Business License Form
  • Kituo cha Habari
    • Video
    • Habari
    • Hotuba kwa Vyombo vya Habari
    • Maktaba ya Picha

WAKULIMA MANG’OLA WAMSHUKURU RAIS SAMIA KWA MRADI WA UMWAGILIAJI

Posted on: September 23rd, 2025



Rc Makalla ataja Mapinduzi makubwa ya kiuchumi kwa wananchi akiagiza mradi ukamilike haraka_

Wananchi wa Vijiji saba vya Kata za Mang’ola na Baray Wilayani Karatu Mkoani Arusha wamemshukuru Rais wa Tanzania Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa utekelezaji wa ujenzi wa mradi mkubwa wa skimu za Umwagiliaji za bonde la Eyasi, Mradi wenye kugharimu Shilingi Bilioni 38, 434, 137, 621. 18, wakisema mradi huo umekuwa na manufaa makubwa katika kuongeza tija na uzalishaji wa mazao ya chakula na biashara katika eneo hilo.

Wakati wa ziara ya Mkuu wa Mkoa wa Arusha Mhe. CPA Amos Gabriel Makalla leo Jumanne Septemba 23, 2025, wakati wa ukaguzi wa mradi huo, wananchi hao wameeleza pia namna ambavyo wamenufaika na ruzuku za mbolea na pembejeo za kilimo, wakisema maendeleo ya Kata zao kwasasa na ukuaji wa uchumi unaoshuhudiwa umetokana na tija kubwa wanayoipata kwenye kilimo cha Vitunguu, Mpunga na mahindi.

Akizungumza mbele ya Mkuu wa Mkoa, Bw. Joseph Hitla, Mkazi na Mkulima wa Kijiji cha Maleckchand amemshukuru pia Mhe. Makalla kwa kusimamia vyema utekelezaji wa shughuli za serikali katika eneo hilo pamoja na kuwatembelea kwenye mashamba yao, akisema Mhe. Makalla amekuwa Mkuu wa Mkoa wa kwanza kutembelea mashamba hayo na kukagua shughuli za kilimo zinazoendelea katika eneo hilo.

Kulingana na CPA Makalla, kukamilika kwa mradi huo kutawanufaisha wananchi wa Vijiji vya Mang’ola Barazani, Maleckchand, Laghangarer pamoja na Vijiji vya Qang’dend, Mbuga nyekundu, Jobaj na Dumbechand, akiagiza Mkandarasi na Tume ya Taifa ya Umwagiliaji kuongeza kasi kuhakikisha mradi huo unakamilika ndani ya muda uliopangwa Kimkataba.

Mradi wa skimu za umwagiliaji Bonde la Eyasi unatekelezwa na Mkandarasi M/S CRJE (EA) Ltd wakiingia makubaliano na Tume ya Taifa ya Umwagiliaji mnamo Machi 30, 2023 kwa Mkataba wa miezi 18 ya kiutekelezaji, mradi ukitarajiwa kukamilika na kukabidhiwa rasmi serikalini kufikia Machi Mosi mwaka 2026.

Matangazo

  • Matokeo ya upimaji wa Kitaifa kidoto cha pili January 07, 2024
  • TANGAZOLA KUITWA KWENYE USAILI September 04, 2025
  • Tangazo la maombi ya mpiga kura kupiga kura ya Rais wa Jamhuri ya Muungano waTanzania katika kituo tofauti na kituo alichojiandikisha September 23, 2025
  • Tangazo la maombi ya mpiga kura kupiga kura ya Rais wa Jamhuri ya Muungano waTanzania katika kituo tofauti na kituo alichojiandikisha September 23, 2025
  • Angalia Zote

Taarifa Mpya

  • RC MAKALLA AISHAURI TUME YA TAIFA YA UMWAGILIAJI KUFANYA MAAMUZI KWA MKANDARASI BWAWA LA EYASI.

    September 23, 2025
  • WAKULIMA MANG’OLA WAMSHUKURU RAIS SAMIA KWA MRADI WA UMWAGILIAJI

    September 23, 2025
  • WENYE SIFA WATAKIWA KUOMBA MIKOPO HALMASHAURI

    September 24, 2025
  • UKUSANYAJI WA MAPATO UNAZIDI KUONGEZEKA KARATU

    September 24, 2025
  • Angalia Zote

Video

DC KOLIMBA ATATUA KERO TARAFA YA EYASI KARATU
Video Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fursa za Uwekezaji

Viunganishi Linganifu

  • Tovuti ya Wizara ya Fedha na Mipango
  • Jamvi la Habari
  • Tovuti ya Tamisemi
  • Tovuti ya Serikali
  • Sekretarieti ya Ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Location Map

Wasiliana Nasi

    Karatu District Council

    Sanduku la Posta: P.O Box 190

    Simu: +255 272970648

    Simu ya Mkononi: 0754773947

    Barua Pepe: ded@karatudc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Haki Miliki @ 2017 Halmashauri ya Wilaya ya Karatu.Haki zote zimehifadhiwa