• Wasiliana Nasi |
    • Maswali |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Complains |
Karatu District Council
Karatu District Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Karatu

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Dhamira na Dira
    • Historia
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Fedha na Biashara
      • Ujenzi
      • Afya
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
    • Vitengo
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma Zetu
  • Madiwani
  • Miradi
    • TASAF
    • BOOST
  • Machapisho
    • Hali ya Uwekezaji
      • Business License Form
  • Kituo cha Habari
    • Video
    • Habari
    • Hotuba kwa Vyombo vya Habari
    • Maktaba ya Picha

BARAZA KUTETA NA WAWEKEZAJI WA MASHAMBA MAKUBWA

Posted on: April 29th, 2021

Na Tegemeo Kastus

Baraza la madiwani la Halmashauri ya Karatu lakusudia kukaa na wawekezaji wa mashamba makubwa ili kusaidia kuondoa vichaka na mapori ambayo yamekuwa hifadhi ya wanyamapori katika maeneo ya makazi ya watu. Kikao hicho kitalenga kujenga na kuimarisha mahusiano mazuri kati ya wananchi na wawekezaji na kuhimiza wawekezaji kuendeleza  maeneo ambayo hawajaendeleza.

Hayo yamesemwa na Mwenyekiti wa Halmashauri ya wilaya ya karatu, Mh. John Lucian katika kikao cha baraza la madiwani cha robo ya tatu ya mwaka. Kikao ambacho katika siku yake ya kwanza taarifa za maendeleo ya kata zimewasilishwa, Mh. Lucian amesema ameshawaalika wawekezaji wa mashamba makubwa kata ya Oldean, Ofisini kwake ili kufanya nao mazungumzo. Amesema lengo kubwa ni kuimairisha mawasiliano na ukarabati wa barabara zinazoingia na kutoka katika kata hiyo, amesema muwekezaji wa shamba la Tembotembo na Agacia wamekubali kutoa fedha kwa ajili kutengeneza barabara itakayopita nje ya mashamba na ofisi zao.

Watendaji wakiwa katika kikao cha cha robo ya tatu ya mwaka ya baraza la madiwani

Mh. Lucian amesema  katika kujenga mazingira ya usalama barabara itayopita nje ya mashamba ya wawekezaji hao itasaidia kuwapa wananchi uhuru wa kuitumia, amesema ni lazima kulinda na kuimarisha mazingira mazuri ya uwekezaji. Wawekezaji hawa lazima walindwe kwa sababu wanaipatia serikali kodi ambayo inaenda kutekeleza shughuli mbalimbali za maendeleo. Ameongeza kusema katika kikao hicho watawaomba wawekezaji ili kupata sehemu ya maeneo kwa ajili ya wananchi kufanya shughuli zao za uzalishaji. Amesema wananchi wengi wanaoishi katika kata ya Oldean hawana kipato kutokana na kuwa na maeneo machache ya kilimo.

Naye Mh. Maria Patrice diwani wa viti maalumu amesema katika kusaidia kutatua changamoto katika eneo la Oldean amesema kumekuwa na mkwamo kwa sababu mara nyingi wakifanya vikao wanakutana na mameneja wa mashamba. Amesema vikao vingekuwa na tija zaidi kama vingefanywa na wamiliki wenyewe wa maeneo husika ambao wanakauli juu ya maeneo yao ya uwekezaji.

Amesema miaka ya nyuma wananchi walikuwa wanaruhusiwa kulima maharage na mahindi hivyo kuzuia hatare ya wanyama pori kujificha katika vichaka vilivyoachwa katika maeneo ya uwekezaji. Amesema sasa hivi wananchi wamezuiwa kujihusisha na kufanya shughuli za kilimo hivyo kufanya kuwa eneo lenye vichaka na kusababisha wanyama pori kuishi katika vichaka hivyo. Mh. Patrice diwani wa viti maalumu amesema kuna jitihada za dhati zilizofanywa na serikali ikiwa ni pamoja na kulichukua eneo la (Rivacu) Rift Valley Cooperative union ambalo Halmashauri  ililitenga eneo kwa ajili ya wananchi kupata eneo la makazi. Lakini bado wananchi wanahitaji maeneo zaidi kwa ajili ya kujihusisha na shughuli za kilimo na makazi.

uwasilishaji wa taarifa za maendeleo za kata ukifanyika katika siku ya kwanza ya baraza la madiwani

Akizungumza katika baraza hilo mkurugenzi mtendaji wa Halmashauri ya wilaya ya Karatu Ndg. Waziri Mourice amesema swala la kuzungumza na wawekezaji wa mashamba ili waridhie kutoa sehemu ya maeneo kwa wananchi liangaliwe kwa tafsiri ya sheria. Amesema kama muwekezaji anaridhia kutoa sehemu ya ardhi kadri atakavyowiwa ni vyema akatoa nyaraka za umiliki wa eneo ili ziweze kurekebishwa. Ili kuja kuondoa migongano ya kisheria baadae  kati ya muwekezaji na wananchi kuliko kutoa ahadi za maneno peke yake.

Matangazo

  • Matokeo ya upimaji wa Kitaifa kidoto cha pili January 07, 2024
  • Halmashauri ya Wilaya ya Karatu Uchaguzi wa Wanafunzi wa kidato cha kwanza, 2024 December 18, 2023
  • Matokeo ya Darasa la Nne January 07, 2024
  • NAFASI ZA KAZI 2024 April 21, 2024
  • Angalia Zote

Taarifa Mpya

  • MILIONI 400 ZATOLEWA KARATU, KUJENGA MABWENI NA MADARASA EYASI SEKONDARI

    January 30, 2025
  • WASIMAMIZI WAASWA KUSIMAMIA VIAPO VYAO KUELEKEA UCHAGUZI WA SERIKALI ZA MITAA 2024.

    November 23, 2024
  • JESHI LA AKIBA MKAWE WAZALENDO KWA TAIFA

    November 23, 2024
  • HALMASHAURI YAZINDUA KITABU CHA MPANGO MKAKATI WA UKUSANYAJI MAPATO.

    November 19, 2024
  • Angalia Zote

Video

DC KOLIMBA ATATUA KERO TARAFA YA EYASI KARATU
Video Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fursa za Uwekezaji

Viunganishi Linganifu

  • Tovuti ya Wizara ya Fedha na Mipango
  • Jamvi la Habari
  • Tovuti ya Tamisemi
  • Tovuti ya Serikali
  • Sekretarieti ya Ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Location Map

Wasiliana Nasi

    Karatu District Council

    Sanduku la Posta: P.O Box 190

    Simu: +255 272970648

    Simu ya Mkononi: 0754773947

    Barua Pepe: ded@karatudc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Haki Miliki @ 2017 Halmashauri ya Wilaya ya Karatu.Haki zote zimehifadhiwa