• Wasiliana Nasi |
    • Maswali |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Complains |
Karatu District Council
Karatu District Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Karatu

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Dhamira na Dira
    • Historia
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Fedha na Biashara
      • Ujenzi
      • Afya
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
    • Vitengo
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma Zetu
  • Madiwani
  • Miradi
    • TASAF
    • BOOST
  • Machapisho
    • Hali ya Uwekezaji
      • Business License Form
  • Kituo cha Habari
    • Video
    • Habari
    • Hotuba kwa Vyombo vya Habari
    • Maktaba ya Picha

BARAZA LATENGA MILLION 100 KUKABILIANA NA CORONA

Posted on: April 29th, 2020

Na Tegemeo Kastus

Baraza la madiwani la Halmashauri ya wilaya ya Karatu limetenga million 100 kwa ajili ya kukabiliana na janga la corona. Fedha hizo zimetengwa ili kununua vifaa tiba madawa pamoja na  na kuandaa miundo mbinu salama kwa ajili ya kudhibiti kusambaa kwa ugonjwa wa COVID-19.

Mwenyekiti wa Halmashuri Mhe. Lazaro Gege  amesema kama kutakuwa kuna uhitaji wa baraza kukaa basi litakaa ili kujadili namna zaidi ya kukabiliana na janga la corona. Ameomba kamati ya kupambana na corona  ya wilaya kuweka mkakati wa kutoa elimu zaidi kwa wananchi. Amesema zile fedha kwa ajili ya mgao wa maadhimisho na shughuli mbalimbali  ambazo zilikuwa zifanyike, mchanganuo wake upelekwe kamati ya fedha kwa ajili ya kuidhinishwa. Ameomba kamati ya kupamabana na virusi vya corona iweke kipaombele  katika kuwapatia wananchi elimu zaidi juu ya maambukizi ya virusi vya corona.

Diwani wa kata ya Daa Mhe. Benedicto Modaha akiwa katika kikao cha baraza la madiwani

Mhe. Theresia Mahongo amepongeza hatua ya baraza hilo la madiwani kwa kutenga kiasi hicho cha Million 100 kwa ajili ya Kupambana na Corona. Mhe. Mahongo amesema awali kanisa la sabato, kanisa la KKT na watu binafsi wamechangia fedha kwa ajili ya kukabiliana na janga la corona. Kiasi cha michango hiyo kimetumika kununua dawa pamoja na mahitaji mengine, ambayo yanasaidia kukabiliana na janga la virusi vya corona.  Mhe. Mahongo amewapongeza sana watu wa afya kwa jitihada wanazofanya, amesema kwenye karantini lazima kuwepo askari Mgambo ili washukiwa wasitoke. Amesema kuna utaratibu maalumu kwa watu walio karantini wakiwa wanamahitaji wanawapa fedha wahudumu wa afya ambao wanawanunulia mahitaji na kuwaletea watu hao walio katika karantini.

Mhe. Mahongo ametoa wito kwa wananchi kufanya shughuli za mazishi kwa idadi isiyozidi watu 30 ili kupunguza misongamano. Amesema kuna watu wamekaa usiku wanacheza Pooltable wanacheza karata, watu wanakunywa pombe za kienyeji bila utaratibu. Ameomba maafisa Tarafa kuchukua hatua za kulinda usalama kwa wananchi kwa kuzuia vitendo vinavyoweza kuongeza maambukizi kipindi hiki cha mlipuko wa virusi vya Corona. Mhe. Mahongo Amemjumuisha Mwenyekiti wa kamati ya elimu afya na maji Mhe. Yotham Manda kuwa mjumbe katika kamati ya wilaya inayokabiliana na Virusi vya corona.

Mkurugenzi Mtendaji ndg. Waziri Mourice amesema janga tulilonalo ni kubwa tunahitaji kufanya maamuzi. Amesema kiwango cha 60% kinachotengwa kwa ajili ya uendeshaji wa Halmashauri ukiangalia namna bajeti inavyopangwa na utekelezaji wake si kweli matumizi yote ya uendeshaji ni 60%. Ndg. Mourice amesema kununua gari la Mkurugenzi si kipaumbele sana, kuna watumishi wanakaa geti la Manyara ambao wanapima joto kila mwanachi anayeingia Karatu na gharama za ufutiliaji zinabebwa na Halmashauri. Amesema kuna watumishi wanatoa tiba bado ni hiyo hiyo 60% inatumika ameomba madiwani kutotizama swala la kutenga fedha kwa kuangalia bajeti ya uendeshaji wa Halmashauri na badala yake litizamwe pande zote.

Mganga mkuu wa wilaya Dkt. Musatafa Waziri amesema mpaka sasa elimu imetolewa kwa watumishi wote na elimu hiyo ni endelevu. Amesema elimu imetolewa kata zote kwa njia ya kutangaza kwa kutumia gari la matangazo. Kuandika barua kwa Mafisa watendaji kata wote kutoa elimu na kuchukua tahadhari ya virusi vya corona. Kutoa elimu nyumba za ibada, mahotel, mamantilie pamoja na nyumba za kulala wageni, juu ya namna ya kujikinga na virusi vya corona. Dkt waziri amesema wamehamasisha jamii juu ya kuweka na kunawa na maji tiririka na sabuni kwenye sehemu zote za biashara nyumbani na maeneo yote yenye mikusanyiko.  Dkt waziri amesema wametoa elimu kwenye minada pamoja na masoko lakini pia kutambua kwa kutenga maeneo ambayo wagonjwa wanaweza kukaa pindi ikitokea kisa cha mgonjwa wa corona.  Waganga wafawidhi wamepewa maelekezo kwenye vituo vyote vya afya kuweka chumba maalum cha kumhifadhi mshukiwa wa ugonjwa wa corona  kwa muda, wakati hatua nyingine za kitabibu zikiendelea kwa mujibu wa miongozo.

Madiwani wakiwa katika kikao cha robo ya tatu wakifuatilia kwa makini mjadala

Dkt. waziri amesema watenga shule ambazo zitatumika kuweka wagonjwa, endapo itatokea wagonjwa wengi wa virusi vya corona, shule hizo ni Karatu sekondari na Ganako. Amesema vikao mbalimbali vya afya vinakaa kwa ajili kubaini changamoto na kuzitatua na kutoa elimu kwa wahudumu wa afya.

Matangazo

  • Matokeo ya upimaji wa Kitaifa kidoto cha pili January 07, 2024
  • Halmashauri ya Wilaya ya Karatu Uchaguzi wa Wanafunzi wa kidato cha kwanza, 2024 December 18, 2023
  • Matokeo ya Darasa la Nne January 07, 2024
  • NAFASI ZA KAZI 2024 April 21, 2024
  • Angalia Zote

Taarifa Mpya

  • MILIONI 400 ZATOLEWA KARATU, KUJENGA MABWENI NA MADARASA EYASI SEKONDARI

    January 30, 2025
  • WASIMAMIZI WAASWA KUSIMAMIA VIAPO VYAO KUELEKEA UCHAGUZI WA SERIKALI ZA MITAA 2024.

    November 23, 2024
  • JESHI LA AKIBA MKAWE WAZALENDO KWA TAIFA

    November 23, 2024
  • HALMASHAURI YAZINDUA KITABU CHA MPANGO MKAKATI WA UKUSANYAJI MAPATO.

    November 19, 2024
  • Angalia Zote

Video

DC KOLIMBA ATATUA KERO TARAFA YA EYASI KARATU
Video Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fursa za Uwekezaji

Viunganishi Linganifu

  • Tovuti ya Wizara ya Fedha na Mipango
  • Jamvi la Habari
  • Tovuti ya Tamisemi
  • Tovuti ya Serikali
  • Sekretarieti ya Ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Location Map

Wasiliana Nasi

    Karatu District Council

    Sanduku la Posta: P.O Box 190

    Simu: +255 272970648

    Simu ya Mkononi: 0754773947

    Barua Pepe: ded@karatudc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Haki Miliki @ 2017 Halmashauri ya Wilaya ya Karatu.Haki zote zimehifadhiwa