• Wasiliana Nasi |
    • Maswali |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Complains |
Karatu District Council
Karatu District Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Karatu

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Dhamira na Dira
    • Historia
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Fedha na Biashara
      • Ujenzi
      • Afya
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
    • Vitengo
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma Zetu
  • Madiwani
  • Miradi
    • TASAF
    • BOOST
  • Machapisho
    • Hali ya Uwekezaji
      • Business License Form
  • Kituo cha Habari
    • Video
    • Habari
    • Hotuba kwa Vyombo vya Habari
    • Maktaba ya Picha

BODI YA AFYA ISAIDIE KATIKA KUBORESHA SEKTA YA AFYA

Posted on: January 25th, 2019

Bodi ya huduma za afya ya wilaya ya Karatu imezinduliwa jana na Mkuu wa Wilaya ya Karatu Mhe. Theresia Mahongo katika Ukumbi wa Halmashauri ya Karatu. Mhe. Theresia amewaomba wajumbe walioteuliwa kusaidia kuboresha sekta ya afya.

 Mhe. Theresia Mahongo amesema tangu tumepata uhuru maadui wetu wamekuwa ni elimu maradhi na tatizo la uchumi; serikali imeendelea kutatua mambo ya elimu kwa kutoa elimu bure, kujenga madarasa na kutoa mikopo kwa wanafunzi masikini katika ngazi ya elimu ya juu. Katika sekta ya afya serikali imeongeza bajeti na ameomba wajumbe wazipitie bajeti vizuri. Ameomba watendaji kutoa ushirikiano kwa bodi ili kufanikisha malengo ya serikali, Mhe. Theresia amesema hatapenda kuona migongano kati ya (watumishi) sekretarieti na bodi.

Dkt. Mustafa Waziri Mganga mkuu wa wilaya amesema katika taarifa yake hali ya utoaji huduma imeboreka, Wilaya Karatu mwezi 12 wakinamama waliojifungua kituo cha afya Karatu ni 188 ambayo ni zaidi ya mara tatu ya awali.

Dkt. Mustafa amesema ICHF mfuko wa afya ulioboreshwa usajili unafanyika kwa kutoa Tsh 30000 kwa watu sita. Utaratibu wa uwanaandikishaji ni kwenye zahanati na picha  ya mtu aliyeandikishwa itakuwepo kwenye kituo ulichojiandikisha, hospitali ya wilaya, na hospitali ya mkoa. Mwananchi aliyelipia ICHF iliyoboreshwa kwa watu sita inamwezesha yeye na wanufaika wa mfuko kutibiwa na kupata rufaa ya matibabu hospitali ya wilaya na hospitali ya mkoa.

Dkt, Mustafa amesema upatikanaji wa dawa muhimu kwenye vituo afya  ni kwa asilimia 97.9, amesema wana akiba ya chupa za damu  1272 ambayo ni sawa na asilimia 85, na kwa kanda ya kaskazini Wilaya ya Karatu ni ya kwanza kwa kuchangia damu. Karatu inawastani wa kutumia chupa tisini hadi mia moja kwa mwezi. Kupitia mpango wa Big result now (BRN) wamepandisha vituo vya afya vienye nyota tatu kumi na mbili na tumepunguza vituo vienye nyota sifuri kumi na mbili mpaka kufikia vituo vitatu.

Matangazo

  • Matokeo ya upimaji wa Kitaifa kidoto cha pili January 07, 2024
  • Halmashauri ya Wilaya ya Karatu Uchaguzi wa Wanafunzi wa kidato cha kwanza, 2024 December 18, 2023
  • Matokeo ya Darasa la Nne January 07, 2024
  • KIKAO CHA BARAZA LA MADIWANI 2024 May 11, 2024
  • Angalia Zote

Taarifa Mpya

  • MAAFISA UANDIKISHAJI WALA KIAPO KARATU

    May 14, 2025
  • DED HOKORORO ASHIRIKI KIKAO CHA ALAT WILAYA YA MERU

    May 15, 2025
  • MADAKTARI BINGWA WA SAMIA AWAMU YA TATU WATUA KARAU

    May 12, 2025
  • KARATU WASAPOTIJUHUDI ZA RAIS SAMIA WATANGAZA UTALII WA NDANI

    May 11, 2025
  • Angalia Zote

Video

DC KOLIMBA ATATUA KERO TARAFA YA EYASI KARATU
Video Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fursa za Uwekezaji

Viunganishi Linganifu

  • Tovuti ya Wizara ya Fedha na Mipango
  • Jamvi la Habari
  • Tovuti ya Tamisemi
  • Tovuti ya Serikali
  • Sekretarieti ya Ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Location Map

Wasiliana Nasi

    Karatu District Council

    Sanduku la Posta: P.O Box 190

    Simu: +255 272970648

    Simu ya Mkononi: 0754773947

    Barua Pepe: ded@karatudc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Haki Miliki @ 2017 Halmashauri ya Wilaya ya Karatu.Haki zote zimehifadhiwa