• Wasiliana Nasi |
    • Maswali |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Complains |
Karatu District Council
Karatu District Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Karatu

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Dhamira na Dira
    • Historia
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Fedha na Biashara
      • Ujenzi
      • Afya
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
    • Vitengo
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma Zetu
  • Madiwani
  • Miradi
    • TASAF
    • BOOST
  • Machapisho
    • Hali ya Uwekezaji
      • Business License Form
  • Kituo cha Habari
    • Video
    • Habari
    • Hotuba kwa Vyombo vya Habari
    • Maktaba ya Picha

CSEE, KUTOA ELIMU YA COVID-19 SIKU 15

Posted on: June 2nd, 2020

Na Tegemeo Kastus

Taasisi ya Community aid and social education empowerment  (CSEE)  kwa kushirikiana  na Child fund Korea  ambao wamejikita katika kusaidia watoto dhidi ya kujikinga na maambukizi ya virusi vya corona wametoa msaada wa vifaa vienye thamani ya million 40 kwa wilaya ya Karatu.

Msaada huo ni vifaa vya kukabiliana na virusi vya corona pamoja na spika za sauti za kusaidia kuelimishia jamii sehemu mbalimbali zenye shughuli zinazokusanya watu wengi pamoja. Mkuu wa wilaya ya Karatu Mh. Theresia Mahongo ameshukuru taasisi ya CSEE kwa msaada waliotowa kwa wananchi wa Karatu. Amesema taasisi hiyo  imegusa vijana  wetu wengi hasa kwa kipindi hiki ambacho vyuo na shule za sekondari za kidato cha tano na sita zikiwa zimefunguliwa. Amesema msaada umekuja wakati sahihi na  kamati ya wilaya ya covid-19 itakaa kikao ili kuweka mpangilio mzuri wa ugawaji wa vifaa kwa watoto katika shule.

Mh. Mahongo amesema bado anaendelea kutoa elimu kwa watu mbalimbali juu ya namna ya kujikinga na virusi vya corona. Ameomba taasisi hiyo kujikita  katika kambi za wavuvi tarafa ya Eyasi pamoja na sehemu za minada. Amesema muda mzuri wa kutoa elimu kwenye kambi ni jioni saa kumi ambao ni muda watu wengi wanakuwa wanarudi kwenye mialo . Mh. Mahongo amepongeza juhudi zilizochukuliwa na Rais wa jamhuri ya muungano wa Tanzania katika kukabiliana na covid-19.

Afisa wa mradi wa CSEE Ndg. Ombeni Sakafu amesema taasisi inafanya kazi na watoto amesema vifaa hivyo vitasambazwa katika shule. Amesema wametoa barokoa 500 N95 lakini  Gun themometre nne za kupima joto.   Amesema wamekabidhi box 20 za sabuni za maji ya kunawia mikono, middle’s Paddle hand wash-facilities 35  Matanki ya kuhifadhia maji kwenye vifaa vya kunawia mikono 20, Chlorine powder kilo 126, Chlorine tablets kilo 5 za Kuna vitakasa mikono mabox  24, PPE 63, gloves boxes 83, spika 3 kwa ajili ya matangazo ya kuelimisha juu ya corona, vipeperushi 144, vienye ujumbe wa kuelimisha juu ya corona pamoja na bronchure 200 na bango 1na Face shield 333.

Amesema mbali na vifaa hivyo wamejikita katika kutoa elimu kwa njia ya bodaboda ambazo watatumia vipaza sauti kucheza sauti iliyorekodiwa na wataalamu wa afya  juu ya namna ya kujikinga na virusi vya corona. Ndg. sakafu amesema watutumia wataalamu wa Halmashauri kutoa elimu ya corona kwa wananchi na watapita kwenye vijiji na magari, kutembelea kaya kuelimisha watu juu ya namna ya kujikinga na corona.


Mh. Theresia Mahongo Mkuu wa wilaya ya Karatu (kushoto) na Katibu tawala  wa wilaya ya Karatu Ndg. Abbas Kayanda wakikagua vifaa vilivyoletwa na CSEE

Matangazo

  • Matokeo ya upimaji wa Kitaifa kidoto cha pili January 07, 2024
  • Halmashauri ya Wilaya ya Karatu Uchaguzi wa Wanafunzi wa kidato cha kwanza, 2024 December 18, 2023
  • Matokeo ya Darasa la Nne January 07, 2024
  • KIKAO CHA BARAZA LA MADIWANI 2024 May 11, 2024
  • Angalia Zote

Taarifa Mpya

  • MAAFISA UANDIKISHAJI WALA KIAPO KARATU

    May 14, 2025
  • DED HOKORORO ASHIRIKI KIKAO CHA ALAT WILAYA YA MERU

    May 15, 2025
  • MADAKTARI BINGWA WA SAMIA AWAMU YA TATU WATUA KARAU

    May 12, 2025
  • KARATU WASAPOTIJUHUDI ZA RAIS SAMIA WATANGAZA UTALII WA NDANI

    May 11, 2025
  • Angalia Zote

Video

DC KOLIMBA ATATUA KERO TARAFA YA EYASI KARATU
Video Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fursa za Uwekezaji

Viunganishi Linganifu

  • Tovuti ya Wizara ya Fedha na Mipango
  • Jamvi la Habari
  • Tovuti ya Tamisemi
  • Tovuti ya Serikali
  • Sekretarieti ya Ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Location Map

Wasiliana Nasi

    Karatu District Council

    Sanduku la Posta: P.O Box 190

    Simu: +255 272970648

    Simu ya Mkononi: 0754773947

    Barua Pepe: ded@karatudc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Haki Miliki @ 2017 Halmashauri ya Wilaya ya Karatu.Haki zote zimehifadhiwa