• Wasiliana Nasi |
    • Maswali |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Complains |
Karatu District Council
Karatu District Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Karatu

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Dhamira na Dira
    • Historia
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Fedha na Biashara
      • Ujenzi
      • Afya
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
    • Vitengo
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma Zetu
  • Madiwani
  • Miradi
    • TASAF
    • BOOST
  • Machapisho
    • Hali ya Uwekezaji
      • Business License Form
  • Kituo cha Habari
    • Video
    • Habari
    • Hotuba kwa Vyombo vya Habari
    • Maktaba ya Picha

DC, APOKEA TAARIFA YA AWALI YA TATHIMINI-JUWAMABOE

Posted on: August 19th, 2020

NA TEGEMEO KASTUS

Mkuu wa wilaya ya Karatu Mh, Abbas Kayanda amepokea taarifa ya awali ya zoezi la uthamini iliyotolewa na kamati maalumu iliyounda na Juwamaboe katika vijiji vinavyojishughulisha na kilimo cha umwagiliaji Tarafa ya Eyasi. Mh. Kayanda amepongeza kamati kwa kazi waliyofanya na kuitaka kutoa mapendekezo ya changamoto zitakazoonekana kwenye tathimini ili isaidie kuondoa malalamiko.

Mh. Kayanda amesema hayo wakati akizungumza na wajumbe wa kamati hiyo katika kikao kilichofanyika Eyasi. Ameelekeza Kamati tendaji  ifanye tathimini ya utafiti katika vijiji vya Jobaj, Lakangarer na Malenchand na kamati ialike mjumbe mmojawapo nje ya kamati atakayeshirikiana na kamati katika kufanya tathimini ya maendeleo ya  kilimo cha  umwagiliaji katika maeneo ambayo hayakufanyiwa tathimini.

Mh. Abbas Kayanda akiwa katika matukio tofauti wakati wa mkutano.

Mh. Kayanda ameelekeza wajumbe wa Juwamaboe kuanza kufikiria namna wakulima wanaweza kuunganisha nguvu na kuanza kujenga visima vitakavyosaidia katika kuendeleza kilimo cha umwagiliaji Tarafa Eyasi. Akitolea mfano wa  kitongoji cha Kambi ya Simba namna ambavyo wameweza kuendelea na kilimo cha umwagiliaji kwa kujenga visima vya umwagiliaji.

Mh. Abbas Kayanda akiwa katika kikao Tarafa ya Eyasi na wajumbe wa Juwamaboe.

Mh. Kayanda amesema kuna swala la ada za mifereji ya umwagiliaji, ameelekeza viongozi wa scheme kusimamia na kuhakikisha ada zinatolewa katika scheme za maji. Amesema fedha zinazochangwa zitasaidia katika uboreshaji wa ukarabati wa mifereji ya umwagiliaji. Amesema katika ukusanyaji wa ada za mifereji lazima risti zitolewe, amesema wakulima wanapaswa kupewa taarifa ya mapato na matumizi ya michango. amesema lazima Jumuiya ya watumiaji maji iangalie upya kiwango cha gharama zinazotolewa, kama kinaendana na uhalisia wa maisha wanayoishi sasa.

Wajumbe wa kamati ya Juwamaboe wakifuatili kikao cha mkuu wa wilaya ya Karatu.

Mh. Kayanda amehimiza ushirikiano Mzuri kati ya uongozi wa jumuiya (Juwamaboe) na viongozi wa wa scheme katika utendaji wa kazi zao. Amesema kumekuwa na mahusiano yasiyo ya kuridhisha kati ya viongozi wa Juwamaboe na viongozi wa Scheme. Amesema uongozi wa wa scheme unatokana na wananchi na uongozi wa Juwamaboe unatokana na scheme. Hivyo kuna kila sababu ya kuimarisha mawasiliano kati ya viongozi hao na wananchi.

Mh.Kayanda amehimiza swala la kutunza amani, amesema hatuwezi kuishi kwa kufanya visa. Lazima kila mtu awe mtiifu kwa kufuata sheria na kuishi kwa upendo na amani.  kumekuwa na watu wanafanya uharibifu wa kuhujumu miundo mbinu ya maji kwa kisingizio cha kudai haki. Amesema yeyote atakayebainika kufanya uhalifu, hatua kali za kisheria zitachukuliwa dhidi yake.

Matangazo

  • Matokeo ya upimaji wa Kitaifa kidoto cha pili January 07, 2024
  • Halmashauri ya Wilaya ya Karatu Uchaguzi wa Wanafunzi wa kidato cha kwanza, 2024 December 18, 2023
  • Matokeo ya Darasa la Nne January 07, 2024
  • KIKAO CHA BARAZA LA MADIWANI 2024 May 11, 2024
  • Angalia Zote

Taarifa Mpya

  • MAAFISA UANDIKISHAJI WALA KIAPO KARATU

    May 14, 2025
  • DED HOKORORO ASHIRIKI KIKAO CHA ALAT WILAYA YA MERU

    May 15, 2025
  • MADAKTARI BINGWA WA SAMIA AWAMU YA TATU WATUA KARAU

    May 12, 2025
  • KARATU WASAPOTIJUHUDI ZA RAIS SAMIA WATANGAZA UTALII WA NDANI

    May 11, 2025
  • Angalia Zote

Video

DC KOLIMBA ATATUA KERO TARAFA YA EYASI KARATU
Video Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fursa za Uwekezaji

Viunganishi Linganifu

  • Tovuti ya Wizara ya Fedha na Mipango
  • Jamvi la Habari
  • Tovuti ya Tamisemi
  • Tovuti ya Serikali
  • Sekretarieti ya Ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Location Map

Wasiliana Nasi

    Karatu District Council

    Sanduku la Posta: P.O Box 190

    Simu: +255 272970648

    Simu ya Mkononi: 0754773947

    Barua Pepe: ded@karatudc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Haki Miliki @ 2017 Halmashauri ya Wilaya ya Karatu.Haki zote zimehifadhiwa