• Wasiliana Nasi |
    • Maswali |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Complains |
Karatu District Council
Karatu District Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Karatu

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Dhamira na Dira
    • Historia
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Fedha na Biashara
      • Ujenzi
      • Afya
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
    • Vitengo
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma Zetu
  • Madiwani
  • Miradi
    • TASAF
    • BOOST
  • Machapisho
    • Hali ya Uwekezaji
      • Business License Form
  • Kituo cha Habari
    • Video
    • Habari
    • Hotuba kwa Vyombo vya Habari
    • Maktaba ya Picha

DC AWAPA KONGOLE WANANCHI WA KIJIJI CHA KAMBI YA SIMBA

Posted on: June 12th, 2021

Na Tegemeo Kastus

Wananchi wa kijiji cha Kambi ya simba wamekuwa chachu ya utekelezaji wa shughuli za maendeleo, wamekuwa vinara katika ujenzi wa miradi ya maendeleo ikilinganisha na vijiji vingine vya wilaya ya Karatu. Kwa uzalendo walionao wananchi wa kijiji cha Kambi ya simba wanatakiwa sasa wasambaze maarifa hayo kwa wananchi wa vijiji vingine ili kuongeza kasi ya utekelezaji wa miradi ya maendeleo.

Hayo yamesemwa na Mkuu wa wilaya ya Karatu Mh. Abbas Kayanda wakati akikabidhi gari lililonunulia na serikali kwa ajili ya kusaidia utoaji wa huduma katika ktuo cha afya cha Kambi ya Simba. Amesema serikali ikiahidi imekuwa ikitekeleza kwa wakati ahadi zake kwa wakati, gari la wagonjwa katika kituo cha afya cha Kambi ya simba lilikuwa hitaji muhimu.

Mh. Abbas Kayanda kushoto akionesha funguo ya gari la kituo cha afya Kambi ya Simba, akiwa na katibu wa chama cha mapinduzi wilaya (katikati) na Mbunge wa jimbo la Karatu Mh. Daniel Awack

Mh. Kayanda amesema gari kwa ajili ya kuhudumia wagonjwa wa kituo cha afya kambi ya simba litabaki kwa ajili ya matumizi ya kituo cha afya cha Kambi ya Simba. Amesema lazima uongozi wa kituo cha afya kambi ya simba ulitumze ili lisadie kuboresha huduma za afya katika kituo cha afya cha Kambi ya simba.

picha za gari la afya kituo cha Afya kambi ya simba

Mh. Kayanda amempongeza mbunge wa jimbo la Karatu Mh. Daniel Awack kwa jitihada zake za dhati katika kuleta maendeleo katika jimbo la Karatu. Amesema Mh. Mbunge amekuwa akiweka mbele maslahi ya maendeleo ya Karatu. Amesema hata hivyo uhitaji wa magari ya wagonjwa bado upo kwa kituo cha afya cha Endabash na kituo cha afya Mbuga nyekundu. Amemuomba mbunge kuendelea kulifuatilia jambo hilo ili na vituo hivyo viweze kupata magari ya wagonjwa.

Mbunge wa jimbo la Karatu Mh.Daniel Awack akiliwasha gari la wagonjwa la kituo cha afya Kambi ya Simba

Amesema serikali imeweka nguvu kubwa katika kuimarisha miundo mbinu ya afya, tunakila sababu ya kuipongeza na kuishukuru serikali inayoongonzwa na Mh. Rais Samia Suluhu Hasani. Uwekezaji mkubwa umefanyika katika kituo cha afya Kambi ya simba ambacho kimeweza kukidhi mahitaji ya kutoa huduma. Amewaasa watendaji wa afya kuitunza gari hiyo ili isaidie kuboresha huduma za afya  waliyopewa na wala sikufanya kazi nyingine  nje ya shughuli za afya.


Mh. Abbas Kayanda akikagua hatua za ujenzi wa Hospitali ya wilaya ya Karatu katika kijiji cha Changarawe

Katika ziara hiyo Mkuu wa wilaya ya Karatu Mh. Kayanda  na wajumbe wa kamati ya ulinzi na usalama wametembelea na kujionea maendeleo ya ujenzi wa Hospitali ya wilaya ya Karatu. Ujenzi ambao unaoendelea katika kijiji cha Changarawe, katika ziara hiyo wajumbe wamejionea jengo la kufulia na jengo la dawa likiwa tayari yakiwa yameshaanza ujenzi wa kuta za majengo lakini jengo la utawala likiwa limeshawekwa kenchi kwa ajili ya upauzi.

Ujenzi huo unahusisha jengo la wazazi ambalo litagharimu takribani milioni 55 jengo la mionzi utagharimu takribani million 24, ujenzi wa jengo la dawa million 25 na ujenzi wa jengo la kufulia utagharimu takribani million 19. Ujenzi huo wa majengo hayo unatarajiwa kukamilika mwezi june tarehe thelathini.

Picha katika matukio tofauti wakati wa ziara ya Mh. Kayanda katika hospitali ya wilaya ya Karatu katika kijiji cha Changarawe

Matangazo

  • Matokeo ya upimaji wa Kitaifa kidoto cha pili January 07, 2024
  • Halmashauri ya Wilaya ya Karatu Uchaguzi wa Wanafunzi wa kidato cha kwanza, 2024 December 18, 2023
  • Matokeo ya Darasa la Nne January 07, 2024
  • NAFASI ZA KAZI 2024 April 21, 2024
  • Angalia Zote

Taarifa Mpya

  • MILIONI 400 ZATOLEWA KARATU, KUJENGA MABWENI NA MADARASA EYASI SEKONDARI

    January 30, 2025
  • WASIMAMIZI WAASWA KUSIMAMIA VIAPO VYAO KUELEKEA UCHAGUZI WA SERIKALI ZA MITAA 2024.

    November 23, 2024
  • JESHI LA AKIBA MKAWE WAZALENDO KWA TAIFA

    November 23, 2024
  • HALMASHAURI YAZINDUA KITABU CHA MPANGO MKAKATI WA UKUSANYAJI MAPATO.

    November 19, 2024
  • Angalia Zote

Video

DC KOLIMBA ATATUA KERO TARAFA YA EYASI KARATU
Video Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fursa za Uwekezaji

Viunganishi Linganifu

  • Tovuti ya Wizara ya Fedha na Mipango
  • Jamvi la Habari
  • Tovuti ya Tamisemi
  • Tovuti ya Serikali
  • Sekretarieti ya Ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Location Map

Wasiliana Nasi

    Karatu District Council

    Sanduku la Posta: P.O Box 190

    Simu: +255 272970648

    Simu ya Mkononi: 0754773947

    Barua Pepe: ded@karatudc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Haki Miliki @ 2017 Halmashauri ya Wilaya ya Karatu.Haki zote zimehifadhiwa