• Wasiliana Nasi |
    • Maswali |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Complains |
Karatu District Council
Karatu District Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Karatu

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Dhamira na Dira
    • Historia
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Fedha na Biashara
      • Ujenzi
      • Afya
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
    • Vitengo
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma Zetu
  • Madiwani
  • Miradi
    • TASAF
    • BOOST
  • Machapisho
    • Hali ya Uwekezaji
      • Business License Form
  • Kituo cha Habari
    • Video
    • Habari
    • Hotuba kwa Vyombo vya Habari
    • Maktaba ya Picha

DCC, YARIDHIA RASIMU YA MPANGO WA BAJETI

Posted on: February 18th, 2021

Na Tegemeo Kastus

Billion thelathini na saba ni bajeti mpya iliyopitishwa na Halmashauri ya wilaya ya Karatu kwa mwaka ujao wa fedha wa serikali. Bajeti imetenga kiasi cha million mia nne kwa ujenzi wa kituo kipya cha afya ambacho kitajengwa katika kata mojawapo itakayoainishwa na baraza la madiwani.

Hayo yamesemwa katika kikao cha Ushauri cha wilaya ambacho Mwenyekiti wa kikao ni Mkuu wa wilaya ya Karatu Mh. Abbas Kayanda. Amesema maelekezo ya serikali kwa Halmashauri zenye uwezo wa kukusanya kuanzia Bil 1.5 mpaka makusanyo ya Bil 5 kwa fedha za ndani, zinapaswa kutenga bajeti ya kujenga kituo kimoja cha afya kila mwaka wa fedha wa serikali. Amesema bajeti ikiendelea kupagwa kwa kuzingatia vigezo hivyo baada ya miaka mitano kutakuwa na vituo vya afya vitano vitakavyojengwa katika kata mbalimbali.

Amesema serikali inampango wa kuzifanya Halmashauri zijiendeshe zenyewe  kupitia mapato yake ya ndani. Ameongeza kusema zipo Halmashauri zimeenda mbali zaidi kwa kujenga vitega uchumi vyake vya mapato kama ofis au hotel ambazo wamezipangisha, amesema ni wakati sasa wa Halmashauri ya Karatu kuanza kubuni na kujenga vitega uchumi. Mh. Kayanda amepongeza wazo la kujenga ukumbi wa kisasa wa Halmashauri kwa ajili ya kuutumia kwenye vikao lakini unaweza kutumika kwenye shughuli nyingine za kijamii.

Matukio tofauti wakati Mwenyikiti wa kamati ya ushauri ya wilaya Mh. Abbas Kayanda akiongoza kikao.

Naye Mwenyekiti wa Halmashauri Mh. John Lucian amepongeza serikali ya awamu ya tano inayongozwa na Rais Mh. Dkt. John Pombe Magufuli kwa kutoa kiasi cha Bilion moja kwa ajili ya ujenzi wa hospitali ya wilaya na million mia hamsini nyingine kwa ajili ya ukarabati wa zahanati tatu ambazo ni zahanati ya Jobaj zahanati ya Mang’ola Juu na zahanati Huduma.

Katika hatua nyingine Mkurugenzi wa Halmashauri ya Karatu Ndg. Waziri Mourice ameshukuru baraza la la ushauri la wilaya kwa kupitisha rasimu ya bajeti. Amesema bajeti ya mwaka huu imeandaliwa kwa kuzingatia vipaombele vya serikali ikiwa ni pamoja na kuangalia mahitaji mbalimbali ya Halmashauri kwa mwaka ujao wa fedha.

Kikao kikiendelea chini ya uongozi wa mwenyekiti Mh, Abbas Kayanda.


Matangazo

  • Matokeo ya upimaji wa Kitaifa kidoto cha pili January 07, 2024
  • Halmashauri ya Wilaya ya Karatu Uchaguzi wa Wanafunzi wa kidato cha kwanza, 2024 December 18, 2023
  • Matokeo ya Darasa la Nne January 07, 2024
  • NAFASI ZA KAZI 2024 April 21, 2024
  • Angalia Zote

Taarifa Mpya

  • MADAKTARI BINGWA WA SAMIA AWAMU YA TATU WATUA KARAU

    May 12, 2025
  • KARATU WASAPOTIJUHUDI ZA RAIS SAMIA WATANGAZA UTALII WA NDANI

    May 11, 2025
  • MILIONI 400 ZATOLEWA KARATU, KUJENGA MABWENI NA MADARASA EYASI SEKONDARI

    January 30, 2025
  • WASIMAMIZI WAASWA KUSIMAMIA VIAPO VYAO KUELEKEA UCHAGUZI WA SERIKALI ZA MITAA 2024.

    November 23, 2024
  • Angalia Zote

Video

DC KOLIMBA ATATUA KERO TARAFA YA EYASI KARATU
Video Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fursa za Uwekezaji

Viunganishi Linganifu

  • Tovuti ya Wizara ya Fedha na Mipango
  • Jamvi la Habari
  • Tovuti ya Tamisemi
  • Tovuti ya Serikali
  • Sekretarieti ya Ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Location Map

Wasiliana Nasi

    Karatu District Council

    Sanduku la Posta: P.O Box 190

    Simu: +255 272970648

    Simu ya Mkononi: 0754773947

    Barua Pepe: ded@karatudc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Haki Miliki @ 2017 Halmashauri ya Wilaya ya Karatu.Haki zote zimehifadhiwa