• Wasiliana Nasi |
    • Maswali |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Complains |
Karatu District Council
Karatu District Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Karatu

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Dhamira na Dira
    • Historia
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Fedha na Biashara
      • Ujenzi
      • Afya
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
    • Vitengo
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma Zetu
  • Madiwani
  • Miradi
    • TASAF
    • BOOST
  • Machapisho
    • Hali ya Uwekezaji
      • Business License Form
  • Kituo cha Habari
    • Video
    • Habari
    • Hotuba kwa Vyombo vya Habari
    • Maktaba ya Picha

DOMEL NA MANG’OLA; ONGEZENI JUHUDI YA UFUNDISHAJI

Posted on: July 10th, 2019

Afisa elimu sekondari ametembelea shule ya sekondari Mang’ola na Domel kukagua ufundishaji wa walimu. Katika ziara hiyo Bi. Maina ameambatana na watendaji wa elimu ngazi ya wilaya, na wamekagaua, na kuzungumza na walimu juu ya mambo mbalimbali yanayohusu taaluma.

Bi. Maina amejionea namna walimu wanavyotekeleza maagizo yake aliyowapa kwa ajili ya utekelezaji. Amesema kila kitu kinawezekana, walimu tuongeze jitihada za ufundishaji wa masomo. Katika ufaulu wa sekondari 32 za wilaya ya Karatu, shule ya sekondari Mang’ola imekuwa ya 16 hivyo ipo katikati kwa kiwango cha ufaulu wilaya. Ngazi ya mkoa imekuwa 135 kati ya shule 226 za mkoa wa arusha. Shule ya Domel imekuwa ya 19 kwa ngazi ya wilaya  na ngazi ya mkoa imekuwa ya 155. Amesema  watoto wa shule binafsi si kwamba wanauwezo sana kuzidi wanafunzi wa shule za serikali. Ila ni wanafunzi wanaopewa mazoezi ya mara kwa mara darasani jambo linalowapa uwezo wa kujibu maswali katika mitihani ya taifa. Bi, Maina  amesema vitu vinavyoangusha shule za sekondari za serikali ni idadi ya ufaulu wa daraja sifuri.

Picha za matukio mbalimbali wakati wa ukaguzi

Naye Afisa elimu Taaluma Bw, Robert Sijaona  amesema lazima walimu kuzingatia ujazaji wa maandalio ya kazi uwe mzuri na usiwe wa kuruka ruka. Amesema kukosa vipindi darasani ni kosa baya kitaaluma na linaweza kukufukuzisha kazi. Hiyo ni sawa na kuwauwa wanafunzi kitaaluma. Bw, Sijaona amesema ni vyema walimu wakawa wanapitia notice na mazoezi wanayowapa wanafunzi ili waweze kusahihisha dosari zinazojitokeza. Ameongeza kusema usipo wasahihisha wanafunzi wanaendelea kujifunza makosa na wanajibu makosa hayo kwenye mtihani. Kipimo cha mwalimu kipo kwenye ueledi anaotumia kumfundisha mwanafunzi, na hayo ndio majukumu ya taaluma ya ualimu.

 Naye Bi, Brenda Mlay ambaye ni mmoja wa wakaguzi amesema somo la kilimo kwa shule ya sekondari Domel limekuwa na vipindi vingi kuliko uwezo alionao mwalimu kufundisha idadi ya vipindi hivyo kwa wanafunzi. Bi. Brenda ametoa maelekezo kwa uongozi wa shule kuangalia namna ya kupunguza mzigo kwa mwalimu ili aweze kufundisha wanafuzi waliopo kwa ufanisi ili wapate matokeo mazuri. Lakini pia amewahimiza walimu walioajiriwa kuendelea kuhimiza walimu wa ziada katika ujazaji wa andalio la somo na kujaza (class journal) daftari la mahudhurio darasani. Hayo yanaenda sambamba na  Ikiwa ni pamoja mpango mkakati uliowekwa na mkuu wa idara ya elimu ya sekondari ya mikakati ishirini na tano ya kuinua kiwango cha elimu wilaya ya Karatu.


Matukio mbalimbali wakati waukaguzi wa walimu

Matangazo

  • Matokeo ya upimaji wa Kitaifa kidoto cha pili January 07, 2024
  • Halmashauri ya Wilaya ya Karatu Uchaguzi wa Wanafunzi wa kidato cha kwanza, 2024 December 18, 2023
  • Matokeo ya Darasa la Nne January 07, 2024
  • NAFASI ZA KAZI 2024 April 21, 2024
  • Angalia Zote

Taarifa Mpya

  • MILIONI 400 ZATOLEWA KARATU, KUJENGA MABWENI NA MADARASA EYASI SEKONDARI

    January 30, 2025
  • WASIMAMIZI WAASWA KUSIMAMIA VIAPO VYAO KUELEKEA UCHAGUZI WA SERIKALI ZA MITAA 2024.

    November 23, 2024
  • JESHI LA AKIBA MKAWE WAZALENDO KWA TAIFA

    November 23, 2024
  • HALMASHAURI YAZINDUA KITABU CHA MPANGO MKAKATI WA UKUSANYAJI MAPATO.

    November 19, 2024
  • Angalia Zote

Video

DC KOLIMBA ATATUA KERO TARAFA YA EYASI KARATU
Video Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fursa za Uwekezaji

Viunganishi Linganifu

  • Tovuti ya Wizara ya Fedha na Mipango
  • Jamvi la Habari
  • Tovuti ya Tamisemi
  • Tovuti ya Serikali
  • Sekretarieti ya Ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Location Map

Wasiliana Nasi

    Karatu District Council

    Sanduku la Posta: P.O Box 190

    Simu: +255 272970648

    Simu ya Mkononi: 0754773947

    Barua Pepe: ded@karatudc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Haki Miliki @ 2017 Halmashauri ya Wilaya ya Karatu.Haki zote zimehifadhiwa