• Wasiliana Nasi |
    • Maswali |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Complains |
Karatu District Council
Karatu District Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Karatu

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Dhamira na Dira
    • Historia
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Fedha na Biashara
      • Ujenzi
      • Afya
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
    • Vitengo
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma Zetu
  • Madiwani
  • Miradi
    • TASAF
    • BOOST
  • Machapisho
    • Hali ya Uwekezaji
      • Business License Form
  • Kituo cha Habari
    • Video
    • Habari
    • Hotuba kwa Vyombo vya Habari
    • Maktaba ya Picha

ENDALA, VIONGOZI WAPEWA SOMO LA UTAWALA BORA

Posted on: September 9th, 2021

Na Tegemeo Kastus

 Viongozi wa serikali za Halmashauri za vijiji waaswa kujenga uadilifu katika utendaji wa majukumu ya kazi. Lengo la kuundwa kwa serikali za mitaa ni kuwezesha viongozi  kuwa karibu na umma na kusaidia kuunganisha wananchi na serikali kuu. Ukiwa kiongozi unakuwa mfano kwa watu wengine katika kufuata taratibu na sheria katika uendeshaji wa serikali ya kijiji. Moja ya sifa ya utawala bora ni pamoja na kulinda siri ya mambo yanayozungumzwa katika vikao vya ndani vya Ofisi.

Mh. Kayanda akiwa na wananchi wa kijiji cha Endala kwenye mkutano wa hadhara.

Hayo yamesemwa na Mkuu wa wilaya ya Karatu Mh. Abbas Kayanda alipofanya Mkutano wa hadhara na wananchi wa kijiji cha Endala. Amesema swala la kusoma mapato na matumizi ya Halmashauri ya serikali ya kijiji si swala la hiari bali ni wajibu wa viongozi kutekeleza takwa hilo la kisheria katika kuendesha serikali ya kijiji. Amesema athari viongozi wa kijiji kuvutana katika uongozi zinachangia kwa kiasi kikubwa kudorora kwa utekelezaji wa miradi ya maendeleo.

Matukio katika picha wakati wa kikao cha hadhara katika ofisi ya kijiji cha Endala

Mh. Kayanda amesema wananchi ndio waajiri wa viongozi, lazima hekima na busara itumike wakati wa kusikiliza kero zao. Kimbilio la wananchi ni viongozi wa serikali za kijiji, ameongeza kusema viongozi wanapozungumza na wananchi lazima watumie lugha za staha bila kuwa na kiburi cha madaraka. Amesema hakuna jambo viongozi wa serikali ya kijiji watafanya bila kushirikisha wananchi.  Ametoa rai kwa wananchi vilevile kutumia lugha ya staha kwa viongozi wanapoawasilisha kero na malalamiko yao kwa viongozi ili kuepusha kutunishiana misuli. Amesema wananchi mtoe ushauri kwa viongozi katika kujenga misingi ya maendeleo ya Halmashauri ya kijiji. Katika mkutano huo viongozi wa Halmashauri ya kijiji cha Endala na wajumbe wake wamemaliza tofauti zao zilizokuwa zimejitokeza awali na kufungua ukurasa mpya. Katika hatua nyingine viongozi hao wamekubaliana kufanya kikao cha Halmashauri kuu ya kijiji cha Endala mwishoni mwa wiki ijayo kwa ajili ya kusoma taarifa ya mapato na Matumizi.

Mh. Kayanda akiwa katika eneo la ujenzi wa choo kwenye shule ya sekondari ya Marang

Katika hatua nyingine Mh. Kayanda ametembelea na kujionea ujenzi wa choo cha wanafunzi katika shule ya sekondari Marang, mradi unaojengwa kwa nguvu za wananchi. Ujenzi wa choo hicho umegharimu takribani million 7 na upo katika hatua za umaliziaji. Mh. Kayanda amepongeza viongozi wa vijiji vya Ayalalio na Endonyawet kwa kusimamia ujenzi huo na ameelekeza viongozi wa vijiji husika kuhakikisha ifikapo tarehe 20/09/2021 ujenzi huo wa choo uwe umekamilika. Mh. Kayanda pamoja na kutembelea mradi huo ametembelea pia eneo linalotarajiwa kujengwa kituo cha afya Buger lilopo katika kijiji cha Ayalalio. Ujenzi huo umetengewa kiasi cha million 400 katika bajeti ya fedha ya mwaka huu.

Mh. Kayanda akiwa katika eneo la ujenzi wa miundo mbinu ya umeme wa Rea Kijiji cha Ayalalio

Wakati huo huo Mh. Kayanda ametembelea kujionea miradi ya Rea mzunguko wa 3 awamu ya 1 iliyokuwa imeachwa kiporo na mkandarasi NIPO aliyevunjiwa mkataba. Miradi hiyo kwa sasa inatekelezwa na kampuni Tanzu iliyo ndani ya Tanesco, amesema maeneo yote ambayo yamesimikwa nguzo za umeme, huduma hiyo ya  umeme itaenda. Ameelekeza meneja wa Tanesco kuhakikisha kwamba kila genge linalohusika na kazi ya usambazaji wa umeme, linakuwepo eneo lake la mradi na kufanya kazi kikamilifu. Ameongeza kusema changamoto ya nguzo za umeme kuachwa chini  ni hatari, ameelekeza meneja wa Tanesco wa wilaya kuhakikisha nguzo zote za umeme zinasimikwa.

Naye meneja wa Tanesco wa wilaya ya Karatu Mhandisi Henry Chahe amesema wamepokea maelekezo ya serikali na wataanza kuyafanyia kazi. Amesema umeme wa Rea utaenda kwenye vijiji makao makuu ya vijiji na kuhakikisha taasisi za umma zinapata huduma ya umeme. Amesema kwa sasa wamejikita katika kusimika nguzo ndogo na baadae watajikita katika kusimika nguzo kubwa. Mhandisi Chahe ametoa rai kwa wananchi kuepuka kufanya usanifu wa  umeme kwenye nyumba kwa kutumia vishoka na badala yake watumie mafundi wanaotambulika na Tanesco. Ameomba wananchi kutumia contol number iliyowekwa na shirika la umeme ili kufanya malipo ya kupata huduma ya umeme lengo likiwa ni kukwepa vitendo vya ulaghai wa fedha vinavyofanywa na watu wenye nia ovu.

Mh.Kayanda akizungumza na viongozi wa serikali ya kijiji cha Endonyawet, katika ofisi za kijiji hicho cha Endonyawet.

Matangazo

  • Matokeo ya upimaji wa Kitaifa kidoto cha pili January 07, 2024
  • Halmashauri ya Wilaya ya Karatu Uchaguzi wa Wanafunzi wa kidato cha kwanza, 2024 December 18, 2023
  • Matokeo ya Darasa la Nne January 07, 2024
  • KIKAO CHA BARAZA LA MADIWANI 2024 May 11, 2024
  • Angalia Zote

Taarifa Mpya

  • MAAFISA UANDIKISHAJI WALA KIAPO KARATU

    May 14, 2025
  • DED HOKORORO ASHIRIKI KIKAO CHA ALAT WILAYA YA MERU

    May 15, 2025
  • MADAKTARI BINGWA WA SAMIA AWAMU YA TATU WATUA KARAU

    May 12, 2025
  • KARATU WASAPOTIJUHUDI ZA RAIS SAMIA WATANGAZA UTALII WA NDANI

    May 11, 2025
  • Angalia Zote

Video

DC KOLIMBA ATATUA KERO TARAFA YA EYASI KARATU
Video Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fursa za Uwekezaji

Viunganishi Linganifu

  • Tovuti ya Wizara ya Fedha na Mipango
  • Jamvi la Habari
  • Tovuti ya Tamisemi
  • Tovuti ya Serikali
  • Sekretarieti ya Ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Location Map

Wasiliana Nasi

    Karatu District Council

    Sanduku la Posta: P.O Box 190

    Simu: +255 272970648

    Simu ya Mkononi: 0754773947

    Barua Pepe: ded@karatudc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Haki Miliki @ 2017 Halmashauri ya Wilaya ya Karatu.Haki zote zimehifadhiwa