• Wasiliana Nasi |
    • Maswali |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Complains |
Karatu District Council
Karatu District Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Karatu

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Dhamira na Dira
    • Historia
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Fedha na Biashara
      • Ujenzi
      • Afya
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
    • Vitengo
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma Zetu
  • Madiwani
  • Miradi
    • TASAF
    • BOOST
  • Machapisho
    • Hali ya Uwekezaji
      • Business License Form
  • Kituo cha Habari
    • Video
    • Habari
    • Hotuba kwa Vyombo vya Habari
    • Maktaba ya Picha

FAHAMU KANUNI ZINAZOMUONGOZA MWENYEKITI WA KITONGOJI

Posted on: December 5th, 2019

Uchaguzi wa serikali za mitaa uliofanyika tarehe 24 mwezi wa kumi na moja mwaka Elfu mbili na kumi na tisa, umeshuhudia Halmashauri ya wilaya ya Karatu ikipata wenyeviti wote wa vitongoji kwa tiketi ya Chama Cha Mapinduzi. Wenyeviti hao walipita bila kupingwa na wengine wakishinda katika maeneo yaliyofanya uchaguzi.

Kitongoji ni eneo la kijiji lilogawanywa kufuatia maagizo ya Mkurugenzi mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya au Mji. Hivyo Halmashauri ya kijiji baada ya kupata idhini ya halmashauri ya mji au  kijiji itaamua idadi ya vitongoji, kaya katika kila kitongoji na mipaka ya kila kitongoji. Vigezo ambavyo huzingatiwa katika kugawa eneo la kijiji katika vitongoji ni ukubwa wa eneo linalokusudiwa kuwa la kitongoji na idadi ya wakazi waliopo. Hii ni kwa mujibu wa KANUNI TARATIBU ZA SHERIA ZA UENDESHAJI WA KIJIJI NA KITONGOJI NA MTAA zilizotolewa na Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na serikali za Mitaa mwezi wa kumi mwaka elfu mbili.

Uendeshaji wa Kitongoji, huongozwa na Mwenyekiti wa kitongoji wa eneo husika ambaye huchaguliwa na wakazi wa kitongoji wenye umri wa kuanzia miaka kumi na nane. Uchaguzi wa Mwenyekiti wa kitongoji hufanyika kwa kila baada ya miaka mitano kwa mujibu wa taratibu za uchaguzi wa viongozi wa vitongoji. Kazi za Mwenyekiti wa kitongoji ni zile zile kama za Mwenyekiti wa kijiji  katika ngazi ya kitongoji na hii ni kwa mujibu wa kanuni za taratibu za sheria za uendeshaji wa kijiji na kitongoji na mtaa zilizotolewa na Ofisi ya Rais Tawala za serikali za Mitaa October (2000)

 kanuni za taratibu za sheria za uendeshaji wa kijiji na kitongoji na mtaa zilizotolewa na Ofisi ya Rais Tawala za serikali za Mitaa zinasema Mwenyekiti anaweza kuondolewa na Mkutano wa wakazi wa kitongoji. Mwenyekiti wa kitongoji anaweza akaondolewa atakapodhihirika kwamba ameshindwa kutekeleza kazi zake au anakiuka maadili ya kazi zake endapo wakazi wa kitongoji watatoa malalamiko.

Hivyo ni vyema wenyeviti wa vitongoji wakafuata matakwa ya kanuni za taratibu za sheria za uendeshaji wa vijiji ili kuepuka kuondolewa kwenye nyadhifa zao hasa ukizingatia serikali imemaliza kufanya uchaguzi wa serikali za mitaa mwezi wa kumi na moja mwaka elfu mbili na kumi na tisa. Wenyeviti wa vitongoji ni viongozi muhimu sana kwa ustawi wa jamiii katika ngazi ya kitongoji. Wao ni viungo muhimu katika kutatua kero za wananchi mahali walipo na ni viongozi wanaowakilisha viongozi wengine wajuu katika nyadhifa tofauti.

Tunahitaji viongozi wa vitongoji kwa kushirikiana na viongozi wengine wa wahamasishe wananchi katika shughuli za maendeleo. Maendeleo yataletwa na sisi wenyewe wananchi tukiwapa ushirikiano wa kutosha viongozi wetu wa vitongoji. Si jambo zuri kwa  kiongozi wa kitongoji kuondolewa katika nafasi yako inapodhihirika umeshindwa kutekeleza majukumu ya kiuongozi katika eneo lako. Wananchi waliowachagua katika maeneo wanashauku kuona utendaji mzuri wa shughuli zenu katika kipindi cha miaka mitano kuanzia sasa.

Wenyeviti wa vitongoji waliochaguliwa wanapaswa kufahamu, Mwenyekiti wa kitongoji anaweza kuondolewa itakaopdhihirika kwamba ameshindwa kutekekeleza kazi zake na anakiuka maadili ya kazi zake. Endapo wakazi wa kitongoji wakitoa malalamiko yaliyosainiwa na wakazi au watu wazima wenye umri wa miaka kumi na nane na kuendelea ambayo yatawasilishwa kwa Afisa mtendaji wa kijiji. Afisa Mtendaji lazima atajiridhisha kwamba tuhuma zilizotolewa zina ushahidi wa kutosha na zimetolewa maelekezo  kamili na yenye kueleweka kwa tuhuma hizo.

Afisa mtendaji wa kijiji mara apatapo taarifa  hiyo kabla ya kupita siku saba ataandaa mkutano wa dharura wa wakazi  wa kitongoji na kupeleka taarifa ya mkutano kwa katibu Tarafa akitaka ahudhurie  yeye mwenyewe au Mwakilishi wake. Kanuni za taratibu za sheria za uendeshaji wa kijiji na kitongoji na mtaa zilizotolewa na Ofisi ya Rais Tawala za serikali za Mitaa zinasema mkutano utaongozwa na Mweneyekiti Mwingine  aliyechaguliwa na wanakitongoji kwa ajili ya kuongoza kikao hicho. Baada ya mkutano kuanza Afisa Mtendaji wa kijiji atasoma tuhuma naushahidi wote uliotolewa dhidi ya mwenyekiti wa kijiji.

Mwenyekiti wa kijiji atapewa nafasi ya kujitetea na kutoa maelekezo dhidi ya tuhuma hizo mbele ya mkutano huo. Baada ya kutafakari tuhuma na utetezi uliotolewa, wajumbe wa mkutano watapiga kura ya kuamua kumuondoa madarakani Mwenyekiti wao wa kitongoji au la. Mwenyekiti wa kitongoji ataondolewa madarakani endapo kura za kumkataa zitafika theluthi mbili ya kura zilizopigwa  mkutanoni. Upigaji kura za kumuondoa madarakani Mwenyekiti wa kitongoji utakuwa wa siri.

Mwenyekiti aliyeondolewa madarakani ana hiari ya kukata rufaa dhidi ya uamuzi wa wanavitongoji wa kumuondoa madarakani, kwa Mkuu wa wilaya  ndani ya siku thelethini tangu uamuzi wa kumtoa madarakani ulipopitishwa. Baada ya kupita siku thelathini anazopewa za kukataa rufaa, Afisa Mtendaji wa kijiji  ataiarifu Halmashauri ya kijiji kuhusu kuondolewa  madarakani Mwenyekiti  wa kitongoji ili utaratibu wa uchaguzi wa Mwenyekiti wa kitongoji ufanyike. Haya yote yatafanyika kwa mujibu wa kanuni za taratibu za sheria za uendeshaji wa kijiji na kitongoji na mtaa zilizotolewa na Ofisi ya Rais Tawala za serikali za Mitaa October (2000)

Matangazo

  • Matokeo ya upimaji wa Kitaifa kidoto cha pili January 07, 2024
  • Halmashauri ya Wilaya ya Karatu Uchaguzi wa Wanafunzi wa kidato cha kwanza, 2024 December 18, 2023
  • Matokeo ya Darasa la Nne January 07, 2024
  • KIKAO CHA BARAZA LA MADIWANI 2024 May 11, 2024
  • Angalia Zote

Taarifa Mpya

  • MAAFISA UANDIKISHAJI WALA KIAPO KARATU

    May 14, 2025
  • DED HOKORORO ASHIRIKI KIKAO CHA ALAT WILAYA YA MERU

    May 15, 2025
  • MADAKTARI BINGWA WA SAMIA AWAMU YA TATU WATUA KARAU

    May 12, 2025
  • KARATU WASAPOTIJUHUDI ZA RAIS SAMIA WATANGAZA UTALII WA NDANI

    May 11, 2025
  • Angalia Zote

Video

DC KOLIMBA ATATUA KERO TARAFA YA EYASI KARATU
Video Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fursa za Uwekezaji

Viunganishi Linganifu

  • Tovuti ya Wizara ya Fedha na Mipango
  • Jamvi la Habari
  • Tovuti ya Tamisemi
  • Tovuti ya Serikali
  • Sekretarieti ya Ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Location Map

Wasiliana Nasi

    Karatu District Council

    Sanduku la Posta: P.O Box 190

    Simu: +255 272970648

    Simu ya Mkononi: 0754773947

    Barua Pepe: ded@karatudc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Haki Miliki @ 2017 Halmashauri ya Wilaya ya Karatu.Haki zote zimehifadhiwa