• Wasiliana Nasi |
    • Maswali |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Complains |
Karatu District Council
Karatu District Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Karatu

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Dhamira na Dira
    • Historia
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Fedha na Biashara
      • Ujenzi
      • Afya
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
    • Vitengo
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma Zetu
  • Madiwani
  • Miradi
  • Machapisho
    • Hali ya Uwekezaji
      • Business License Form
  • Kituo cha Habari
    • Video
    • Habari
    • Hotuba kwa Vyombo vya Habari
    • Maktaba ya Picha

HATUNA BUDI KUWEKEZA KWENYE ELIMU

Posted on: October 30th, 2018

Na Tegemeo Kastus

Mdau wa elimu Ndugu Elias Philip Simpa, jana ametoa vifaa vya elimu vyenye thamani ya shilingi 300,000 kwa shule ya sekondari Awet, kata ya Mbulumbulu. Vifaa hivyo ni madaftari makubwa, mathematical set na mbuzi ili kuhamasisha shughuli za michezo shughuli za kitaaluma.

Ndugu Simpa ametoa daftari kubwa tatu na mathematical set kwa kila mtoto aliyeshika nafasi ya kwanza, daftari mbili kwa mtoto aliyeshika nafasi ya pili na daftari moja kwa mtoto aliyeshika nafasi ya tatu, zawadi hizo zimetolewa kwa kidato cha kwanza mpaka cha nne.

Ndugu simpa amehimiza jitihada kwa wazazi na walimu, amesema shule ya sekondari Awet ni shule Kongwe katika kata ya Mbulumbulu, tunahitaji kuwekeza kwenye elimu ili tupande kitaaluma. Kazi ya walimu ni kuelekeza wanafunzi hatuna budi kuondoa daraja la nne na sifuri. Bila taifa lenye elimu taifa litakuwa gizani, bila kusoma uchumi wa viwanda hatuwezi kuufikia, nyie wanafunzi ndio mtakao chukua nafasi zetu.

Ndugu Simpa amehimiza wanafunzi kupenda masomo ya sayansi na ameahidi kutoa shilingi 50000 kwa kila mwanafunzi atakaye faulu mtihani wa kuhitimu kidato cha nne kwa kiwango cha daraja la kwanza. Nidhamu zuri inahitajika kwa wanafunzi ili waweze kufanya vizuri katika masomo.

Ndugu Simpa ametoa zawadi ya mbuzi kwa mshindi wa ligi ya mbuzi iliyofanyika  katika shule hiyo ya sekondari Awet. Pia ametoa zawadi kwa mfungaji bora wa mashindano hayo, mchezaji bora wa mashindano, waamuzi waliochezesha michezo sambamba na makocha.

Mwalimu mkuu wa shule ya sekondari Awet Ndugu Christopher Sulle, amemshukuru Ndugu Simpa kwa mchango wake amefurahia zawadi hizo amesema swala la taaluma linamgusa kila mtu, ameesema Ndugu Simpa amejinyima ili kusaidia elimu huu ni mwanzo mzuri.

Matangazo

  • WALIOCHANGULIWA KIDATO CHA KWANZA - 2023, HALMASHAURI YA KARATU December 14, 2022
  • LAKE EYASI CULTURAL TOURISM PROGRAM NEW ENTRY FEE December 01, 2022
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI NAFASI YA MTENDAJI WA KIJIJI DARAJA LA 111 NA MSAIDIZI WA KUMBUKUMBU DARAJA LA 11 May 07, 2021
  • Angalia Zote

Taarifa Mpya

  • MIAKA (61) YA UHURU MKUU WA WILAYA YA KARATU MHE DADI HORICE KOLIMBA AFUNGUA MDAHALO WA MAENDELEO WILAYA YA KARATU.

    December 09, 2022
  • MAADHIMISHO YA MIAKA 61 YA UHURU WA TANGANYIKA

    December 09, 2022
  • MAADHIMISHO YA MIAKA 61 YA UHURU WA TANGANYIKA

    December 09, 2022
  • LAKE EYASI CULTURAL TOURISM TO BE IMPROVED

    November 08, 2022
  • Angalia Zote

Video

NDUGU. EDWARD MAURA MWENYEKITI WA BARAZA LA WAFUGAJI NGORONGORO
Video Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fursa za Uwekezaji

Viunganishi Linganifu

  • Tovuti ya Wizara ya Fedha na Mipango
  • Tovuti ya Tamisemi
  • Tovuti ya Serikali
  • Sekretarieti ya Ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Location Map

Wasiliana Nasi

    Karatu District Council

    Sanduku la Posta: P.O Box 190

    Simu: +255 272970648

    Simu ya Mkononi: 0754266833

    Barua Pepe: ded@karatudc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Haki Miliki @ 2017 Halmashauri ya Wilaya ya Karatu.Haki zote zimehifadhiwa