• Wasiliana Nasi |
    • Maswali |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Complains |
Karatu District Council
Karatu District Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Karatu

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Dhamira na Dira
    • Historia
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Fedha na Biashara
      • Ujenzi
      • Afya
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
    • Vitengo
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma Zetu
  • Madiwani
  • Miradi
    • TASAF
    • BOOST
  • Machapisho
    • Hali ya Uwekezaji
      • Business License Form
  • Kituo cha Habari
    • Video
    • Habari
    • Hotuba kwa Vyombo vya Habari
    • Maktaba ya Picha

HATUTAKI MDONDOKO WA WASICHANA KWENYE ELIMU

Posted on: March 11th, 2020

Na Tegemeo Kastus

Naibu katibu Mkuu wa Wizara ya Elimu Sayansi na Technolojia  Dk. Avemaria Semakafu amefanya ziara katika shule ya sekondari ya Florian wilayani Karatu. Katika ziara hiyo amejionea kazi zinazofanywa na shirika la world education initiative (WEI)  katika kunyanyua taaluma ya mtoto wa kike.

Dkt. Avemaria Semakafu amewaambia wanafunzi wa shule ya sekondari Florian kwamba wote wanaoacha shule siyo kwa sababu ya mimba au kuolewa. Amesema kunawatoto wa kike wanaacha shule kwa sababu ya mila, wengine kwa sababu ya umbali mrefu na shule ilipojengwa.

Dkt. Semakafu amesemba wanafunzi wanaogopa mimba kuliko hata corona, amesema maisha yapo ili tuyafurahie. Amesema mwanafunzi atafurahia maisha yake ya shule kama hata jihusisha na mapenzi. Amesema ukianza kujihusisha na mapenzi; kuacha ni kazi, ameomba wanafunzi kujifunza kwa mabinti wenzao waliokatishwa masomo kwa sababu ya ujauzito. Amesema mtoto wa kike akisoma anakuwa na msimamo, amesema ni vyema wanafunzi wa kike wakawa na msimamo.

Dkt Semakafu amesema Tanzania inaelekea uchumi wa viwanda, je Florian mmejianda vipi ? amesema unapozungumzia uchumi wa viwanda unaongelea Mainjinia, Madaktari, Mafundi wasanifu, watu waliobobea kwenye mambo ya uchumi. Amesema kwa matokeo aliyopewa ya kidato cha sita na matokeo ya kidato cha nne hayaridhishi. Ameomba wanafunzi kutumia klabu zilizoanzishwa kuinua ufaulu wa kitaaluma. Amesema lazima Florian ijipange kutoa watu watakaosaidia kujenga uchumi wa viwanda.

Dkt. Avemari Semakafu (aliyekatikati) akizungumza jambo na  watendaji wa idara ya elimu wilaya ya Karatu

Dkt. Semakafu amesema mathalani katika ujenzi wa standard Gauge alioutembelea Ma-project Meneja wa  mradi wa reli kutoka Dodoma mpaka Makutupora ni mdada na Makutupora mpaka Mwanza Project Meneja ni mdada wa kitanzania. Katika ujenzi wa Mahandaki, sehemu ambazo treni itatoboa mlima na kupita chini ya milima kwa baadhi ya maeneo,  amesema anayesimamia mradi huo injinia mkubwa ni dada  mwenye asili ya kituruki. Ameomba mabinti wa kike wa shule ya wasichana ya Florian kuhamasika na kusoma kwa bidii ili waje waisaidie nchi.

Dkt . Semakafu amesema Mhe. Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli alipoamua kuondoa vikwazo katika elimu msingi  na sekondari  mpaka kidato cha nne kuwa bure alikuwa anamaana mwanafunzi asishindwe kwenda shule kawa sababu ya kukosa ada. Mwanafunzi asishindwe kwenda shule kwa sababu kuna mchango wa taaluma shuleni ambao ameambiwa achangie. Amesema Wanafunzi watasema asante ya aina gani ?? Amesema kazi ya mwanafunzi ni kusoma na kufaulu, amesema awali wanafunzi walikuwa wanasoma wanakosa shule au madarasa ya kusomea. Amesema lakini kwa Mhe, Rais Dkt. John Pombe Magufuli lazima madarasa yajengwe, ameuliza wanafunzi wa Florian wanatakwa wapendwe vipi ??

Amesema wanafunzi lazima wajipange kufaulu kwa kiwango cha daraja la kwanza ili hata wakianguka upate daraja la pili. Dkt. Semakafu amewaasa wanafunzi kuacha kupitia njia za mkato, ametumia fursa hiyo kuwaasa walimu kuacha kujihusisha kimapenzi na wanafunzi amesema hilo ni jambo la aibu na linachangia kudidimiza elimu mashuleni. Amewambia walimu tunahitaji kuwasaidia vijana wetu, na tutawasaidia kama hatutajihusisha na vitendo vya kuzalilisha wanafunzi. Amesema wizara ya elimu haitaki mimba shuleni, haitaki mdondoko wa wasichana kutoka kwenye elimu, kampeni kubwa sasa ni kujenga mabweni kwenye shule za sekondari.

Naibu katibu Mkuu Wizara ya Elimu Sayansi na Technolojia Dkt. Avemaria Semakafu (aliye katikati) akiwa katika picha ya pamoja na wanafunzi wa shule ya sekondari Florian.

Matangazo

  • Matokeo ya upimaji wa Kitaifa kidoto cha pili January 07, 2024
  • Halmashauri ya Wilaya ya Karatu Uchaguzi wa Wanafunzi wa kidato cha kwanza, 2024 December 18, 2023
  • Matokeo ya Darasa la Nne January 07, 2024
  • NAFASI ZA KAZI 2024 April 21, 2024
  • Angalia Zote

Taarifa Mpya

  • MILIONI 400 ZATOLEWA KARATU, KUJENGA MABWENI NA MADARASA EYASI SEKONDARI

    January 30, 2025
  • WASIMAMIZI WAASWA KUSIMAMIA VIAPO VYAO KUELEKEA UCHAGUZI WA SERIKALI ZA MITAA 2024.

    November 23, 2024
  • JESHI LA AKIBA MKAWE WAZALENDO KWA TAIFA

    November 23, 2024
  • HALMASHAURI YAZINDUA KITABU CHA MPANGO MKAKATI WA UKUSANYAJI MAPATO.

    November 19, 2024
  • Angalia Zote

Video

DC KOLIMBA ATATUA KERO TARAFA YA EYASI KARATU
Video Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fursa za Uwekezaji

Viunganishi Linganifu

  • Tovuti ya Wizara ya Fedha na Mipango
  • Jamvi la Habari
  • Tovuti ya Tamisemi
  • Tovuti ya Serikali
  • Sekretarieti ya Ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Location Map

Wasiliana Nasi

    Karatu District Council

    Sanduku la Posta: P.O Box 190

    Simu: +255 272970648

    Simu ya Mkononi: 0754773947

    Barua Pepe: ded@karatudc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Haki Miliki @ 2017 Halmashauri ya Wilaya ya Karatu.Haki zote zimehifadhiwa