• Wasiliana Nasi |
    • Maswali |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Complains |
Karatu District Council
Karatu District Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Karatu

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Dhamira na Dira
    • Historia
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Fedha na Biashara
      • Ujenzi
      • Afya
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
    • Vitengo
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma Zetu
  • Madiwani
  • Miradi
    • TASAF
    • BOOST
  • Machapisho
    • Hali ya Uwekezaji
      • Business License Form
  • Kituo cha Habari
    • Video
    • Habari
    • Hotuba kwa Vyombo vya Habari
    • Maktaba ya Picha

JAMII IPATE UHALISIA WA DHIMA YA KUADHIMISHA SIKU YA MWANAMKE

Posted on: March 8th, 2021

Na Tegemeo Kastus

Siku ya wanawake ni siku muhimu sana kwa ustawi  wa vijana wetu wa kike, lazima tufanye maandalizi kwa kuanza ngazi ya kijiji kata na kilele kifanyike katika ngazi ya wilaya. Maadhimisho yalenge kujenga uelewa wa pamoja kati wanawake na vijana wa kike walio bado shuleni.

Hayo yaemesemwa na Mwenyekiti wa Halmashuri ya wilaya ya Karatu Mh. John Lucian wakati akizungumza katika kilele cha siku ya wanawake kilichofanyika katika Uwanja wa mazingira Bora Karatu. Amesema malengo ni kumjengea uwezo wa kimaadili mama wa leo na mama wa kesho, kwa kuanzia katika ngazi ya kijiji  mpaka kufikia ngazi ya wilaya.

Mh. John Lucian akitoa salamu katika maadhimisho ya siku ya wanawake

Mh. Lucian amesema Halimashauri haitatoa mikopo ya upendeleo, itaendele kusimamia utoaji mikopo2% kwa walemavu, 4% kwa vijana na 4%kwa wakinamama. Lazima tuchukue hatua za kuwawajibisha watu ambao hawataki kurejesha fedha za mikopo. Amehimza  watendaji kutoa mikopo  kwa kuzingatia usawa bila kupendelea  maeneo.


Matukio tofauti wakati Mh. Lucian akitoa salamu

Naye afisa maendeleo ya Jamii wilaya ya Karatu Bi, Adelaida Shauri akitoa salamu za shukrani, amesema Halmashauri imetoa kiasi cha million 120 kwa vikundi vya kinamama  vijana na wazee 96. Amesema changamoto kubwa idara ya maendeleo ya jamii inakabiliana nayo ni baadhi ya wanawake wanaopewa mikopo kushindwa kurejesha kwa wakati. Amesema serikali imeunda sheria mpya ya mwaka 2019 inayomuwezesha Afisa sheria wa Halmashauri kuwashitaki Mahakamani watu wanaoshindwa kurejesha mikopo isiyo na riba ya Halmashauri. Amesema kwa kupitia sheria hiyo kikundi kitakachoshindwa kurejesha fedha hatua za kisheria zitachukuliwa dhidi yao. Amesema kama watu wanaopewa mikopo wangeweza kuirejesha kwa wakati Halmashauri ingeweza kutoa kiasi cha million 300 kwa ajili ya mikopo isIyo na riba kwa wanawake vijana na walemavu.

Matangazo

  • Matokeo ya upimaji wa Kitaifa kidoto cha pili January 07, 2024
  • Halmashauri ya Wilaya ya Karatu Uchaguzi wa Wanafunzi wa kidato cha kwanza, 2024 December 18, 2023
  • Matokeo ya Darasa la Nne January 07, 2024
  • NAFASI ZA KAZI 2024 April 21, 2024
  • Angalia Zote

Taarifa Mpya

  • MILIONI 400 ZATOLEWA KARATU, KUJENGA MABWENI NA MADARASA EYASI SEKONDARI

    January 30, 2025
  • WASIMAMIZI WAASWA KUSIMAMIA VIAPO VYAO KUELEKEA UCHAGUZI WA SERIKALI ZA MITAA 2024.

    November 23, 2024
  • JESHI LA AKIBA MKAWE WAZALENDO KWA TAIFA

    November 23, 2024
  • HALMASHAURI YAZINDUA KITABU CHA MPANGO MKAKATI WA UKUSANYAJI MAPATO.

    November 19, 2024
  • Angalia Zote

Video

DC KOLIMBA ATATUA KERO TARAFA YA EYASI KARATU
Video Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fursa za Uwekezaji

Viunganishi Linganifu

  • Tovuti ya Wizara ya Fedha na Mipango
  • Jamvi la Habari
  • Tovuti ya Tamisemi
  • Tovuti ya Serikali
  • Sekretarieti ya Ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Location Map

Wasiliana Nasi

    Karatu District Council

    Sanduku la Posta: P.O Box 190

    Simu: +255 272970648

    Simu ya Mkononi: 0754773947

    Barua Pepe: ded@karatudc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Haki Miliki @ 2017 Halmashauri ya Wilaya ya Karatu.Haki zote zimehifadhiwa