• Wasiliana Nasi |
    • Maswali |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Complains |
Karatu District Council
Karatu District Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Karatu

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Dhamira na Dira
    • Historia
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Fedha na Biashara
      • Ujenzi
      • Afya
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
    • Vitengo
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma Zetu
  • Madiwani
  • Miradi
    • TASAF
    • BOOST
  • Machapisho
    • Hali ya Uwekezaji
      • Business License Form
  • Kituo cha Habari
    • Video
    • Habari
    • Hotuba kwa Vyombo vya Habari
    • Maktaba ya Picha

JIFUNZE NAMNA YA KUKABILIANA NA SUMU YA MDUDU NAIROBI FLY

Posted on: January 11th, 2020

Narrow bee fly au Nairobi fly ni aina ya wadudu ambao wako katika makundi mawili, ambayo huishi Afrika ya mashariki.  Aina hizo mbili za Nairobi fly  zinaitwa  Paederus  Eximius na Paederus Sabaeus kwa mujibu wa Wikipedia.

Wadudu aina ya Nairobi fly hushamiri sana kipindi cha mvua , ambacho mara nyingi huonekana na husambaa kwa wingi katika mazingira yetu. Katika aina hizo mbili za Nairobi fly ambazo  kitaalamu (Botanic name) Paederus Eximus ni aina fupi ya Nairobi fly na Paedrus Sabaeus ni aina ndefu ya Nairobi fly.

Afisa Mhifadhi wanyamapori wilaya ya Karatu Ndg. Cornel Lengai anasema Nairobi fly ni wadudu ambao majimaji yao (Haemolymph) yana kemikali sumu inayoitwa Pederin. Anasema kamikali pederin inasumu sana endapo itagusana na ngozi ya binadamu.

Ndg.Lengai anasema wadudu hawa hawang’ati, ila mtu anapomuona mdudu anatambaa kwenye ngozi yake huamua kumpiga, au kumgandamiza juuya ngozi. Afisa Mhifandi wanyamapori Ndg. Lengai anasema unapofanya hivyo, majimaji yanayotoka kwenye mwili wa mdudu huyo baada ya kumgandamiza na akamuua ndio yanakiwango kikubwa cha kemikali sumu inayoitwa kitaalam Pederin.

Ndg. Lengai anasema kemikali hiyo inapogusana na ngozi ndio inaleta athari kama tatizo la ngozi linaloitwa (Paederu Dermatitis)  Malengelenge na mara nying dalili zake hujitokeza ndani ya masaa 12-48. Ndg. Lengai anasema dalili zinazojitokeza ni kuhisi muwasho wa ngozi, kuhisi sehemu iliyoathirika na majimaji ya sumu kama panawaka moto unaoambatana na maumivu makali. Ngozi kuonekana nyekundu katika eneo liloathririka, michubuko na michirizi huonekana kama pameungua.

Ndg. Lengai anasema Jinsi ya kukinga madhara ya mdudu aina ya Nairobi fly ukimuona  anatamba kwenye ngozi, ni vyema ukampuliza au kumuondoa adondoke na umuuwe kwa kitu na siyo mahusiano ya moja kwa moja na ngozi ya mwili wako  (direct contact) Ndg. Lengai anashauri endapo ikitokea umemuuwa juu ya ngozi au mkononi, unashauriwa kunawa mikono haraka, kusafisha sehemu hiyo ya ngozi kwa maji mengi ya kutosha na sabauni.

Ndg. Lengai anashauri kupaka  (tropical antihistamines) ambayo inaweza kupatikana kwenye dawa kama white dent ili kupunguza madhara kwenye ngozi (allegic reaction) inayotokana na sumu ya majimaji yanayotoka mwilini mwa Nairobi fly.

Matangazo

  • Matokeo ya upimaji wa Kitaifa kidoto cha pili January 07, 2024
  • Halmashauri ya Wilaya ya Karatu Uchaguzi wa Wanafunzi wa kidato cha kwanza, 2024 December 18, 2023
  • Matokeo ya Darasa la Nne January 07, 2024
  • NAFASI ZA KAZI 2024 April 21, 2024
  • Angalia Zote

Taarifa Mpya

  • MAAFISA UANDIKISHAJI WALA KIAPO KARATU

    May 14, 2025
  • DED HOKORORO ASHIRIKI KIKAO CHA ALAT WILAYA YA MERU

    May 15, 2025
  • MADAKTARI BINGWA WA SAMIA AWAMU YA TATU WATUA KARAU

    May 12, 2025
  • KARATU WASAPOTIJUHUDI ZA RAIS SAMIA WATANGAZA UTALII WA NDANI

    May 11, 2025
  • Angalia Zote

Video

DC KOLIMBA ATATUA KERO TARAFA YA EYASI KARATU
Video Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fursa za Uwekezaji

Viunganishi Linganifu

  • Tovuti ya Wizara ya Fedha na Mipango
  • Jamvi la Habari
  • Tovuti ya Tamisemi
  • Tovuti ya Serikali
  • Sekretarieti ya Ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Location Map

Wasiliana Nasi

    Karatu District Council

    Sanduku la Posta: P.O Box 190

    Simu: +255 272970648

    Simu ya Mkononi: 0754773947

    Barua Pepe: ded@karatudc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Haki Miliki @ 2017 Halmashauri ya Wilaya ya Karatu.Haki zote zimehifadhiwa