• Wasiliana Nasi |
    • Maswali |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Complains |
Karatu District Council
Karatu District Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Karatu

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Dhamira na Dira
    • Historia
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Fedha na Biashara
      • Ujenzi
      • Afya
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
    • Vitengo
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma Zetu
  • Madiwani
  • Miradi
    • TASAF
    • BOOST
  • Machapisho
    • Hali ya Uwekezaji
      • Business License Form
  • Kituo cha Habari
    • Video
    • Habari
    • Hotuba kwa Vyombo vya Habari
    • Maktaba ya Picha

KASI YA UJENZI WA HOSPITALI YA WILAYA NI NZURI

Posted on: May 27th, 2019

Mkuu wa mkoa wa Arusha Mhe. Mrisho Gambo amefanya ziara katika eneo linalojengwa hopitali ya Wilayaya karatu katika kijiji cha Changarawe. Ameangalia ujenzi wa jengo la Maabara, jengo la wagonjwa wa nje na jengo la utawala.

Mhe. Mrisho Gambo ameridhishwa na hatua za ujenzi wa hospitali. Ameshukuru bodi ya hifadhi ya Ngorongoro kwa kutoa shilingi million 500 kuanzisha ujenzi wa hospital. Amesema huu uwe ushuhuda kwa wananchi wa Karatu, kwamba tukipinga ujangili, tukilinda wanyamapori wetu, tukilinda hifadhi zetu faida ni kubwa sana. Hifadhi isingekuwepo watalii wasingekuja, tusingenufaika kama tunavyonufaika sasa. Ametoa wito kwa wanachi kuendelea kulinda hifadhi na kutoa taarifa ya vitendo vya ujangili  kwa vyombo husika

Naye Mhifadhi wa Ngorongoro Ndugu Fredy  Manongi amesema kazi iliyofanyika inawapa moyo. Ndugu Fredy anasema wao kama watu wa hifadhi walipopata ombi la fedha za awali za kujenga hospital ya wilaya walilichukulia wazo hilo kwa mtazamo chanya. Wakajenga hoja na kulipeleka wazo hilo kwenye bodi ya hifadhi ya Ngorongoro. Ndugu Fredy amesema wataomba bodi kuendelea kutoa fedha kwa ajili ya hospital ya wilaya ya Karatu  kwa mwaka ujao wa fedha ili iweze kukamilika. Amesema wanajua umuhimu wa karatu kwa uhifadhi lakini pia wanafahamu adhaa kubwa watu wanayopata juu ya wanayamapori. Wanyama huwa wanatoka kwenye hifadhi na wanaathiri maisha ya watu.Hivyo mamlaka ya hifadhi imeona kuna haja ya kuchangia  maendeleo ya wananchi wa Karatu.

Katika taarifa ya awali injinia Venance Malamla amesema Halmashauri kwa mwaka huu wa fedha imetoa kiasi cha shilingi million 32 ya ujenzi wa hospitali ya Wilaya. Mwaka ujao wa fedha Halmashauri imetenga kiasi cha shilingi million 40. Wananchi wameshiriki katika ujenzi wa hospitali kwa kujitolea nguvu kazi na zoezi hilo liliisha mwezi wa nne. Mpango kazi wa sasa ambao mafundi wamesaini utadumu kwa muda wa miezi minne na utaishia mwezi wanane.

Injinia Malamla anasema mpaka sasa hatua zilizofanyika katika ujenzi wa jengo la utawala ni kusafisha eneo; kuchimba msingi, kupanga mawe kwenye msingi, kujenga tofali za msingi,   kujenga zege la msingi, kupanga mawe na kusuka nondo.Kazi ya kupiga mbao kwa ajili ya ujenzi wa jamvi inaendelea ambayo kwa sasa ni 20%. Jengo la maabara; kusafisha eneo, kujenga eneo ujenzi wa mawe chini ya msingi, kujenga tofali za msingi, kujenga zege la msingi , kupanga mawe zoezi linaendelea. Jengo la wagonjwa wa nje: kusafisha eneo, kuchimba msingi  kupanga mawe, kujenga mawe chini ya msingi na kusuka nondo kazi bado inaendelea. Injinia Malamla amesema mpaka sasa imetumika million 249339475. Injinia Malamla amesema million 22000,194, ununuzi wa vifaa vya ujenzi million 222717475 na mafuta million 4428000 elfu.

Injinia Malamla amesema wanapata changamoto kipindi hiki cha mvua kupeleka vifaa vya ujenzi eneo la mradi. Magari ya mawe, mchanga, na kokoto kushindwa kufika eneo la ujenzi. Kazi za ufundi kukwama kwa sababu ya mvua kunyesha, hivyo wameamua kutumia mda mchache mvua inapopungua kwa wazabuni kuleta vifaa eneo la ujenzi na mafundi kutumia mda mchache wakati mvua inapopungua kuendelea na ujenzi.

Matangazo

  • Matokeo ya upimaji wa Kitaifa kidoto cha pili January 07, 2024
  • Halmashauri ya Wilaya ya Karatu Uchaguzi wa Wanafunzi wa kidato cha kwanza, 2024 December 18, 2023
  • Matokeo ya Darasa la Nne January 07, 2024
  • KIKAO CHA BARAZA LA MADIWANI 2024 May 11, 2024
  • Angalia Zote

Taarifa Mpya

  • MAAFISA UANDIKISHAJI WALA KIAPO KARATU

    May 14, 2025
  • DED HOKORORO ASHIRIKI KIKAO CHA ALAT WILAYA YA MERU

    May 15, 2025
  • MADAKTARI BINGWA WA SAMIA AWAMU YA TATU WATUA KARAU

    May 12, 2025
  • KARATU WASAPOTIJUHUDI ZA RAIS SAMIA WATANGAZA UTALII WA NDANI

    May 11, 2025
  • Angalia Zote

Video

DC KOLIMBA ATATUA KERO TARAFA YA EYASI KARATU
Video Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fursa za Uwekezaji

Viunganishi Linganifu

  • Tovuti ya Wizara ya Fedha na Mipango
  • Jamvi la Habari
  • Tovuti ya Tamisemi
  • Tovuti ya Serikali
  • Sekretarieti ya Ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Location Map

Wasiliana Nasi

    Karatu District Council

    Sanduku la Posta: P.O Box 190

    Simu: +255 272970648

    Simu ya Mkononi: 0754773947

    Barua Pepe: ded@karatudc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Haki Miliki @ 2017 Halmashauri ya Wilaya ya Karatu.Haki zote zimehifadhiwa