• Wasiliana Nasi |
    • Maswali |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Complains |
Karatu District Council
Karatu District Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Karatu

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Dhamira na Dira
    • Historia
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Fedha na Biashara
      • Ujenzi
      • Afya
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
    • Vitengo
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma Zetu
  • Madiwani
  • Miradi
    • TASAF
    • BOOST
  • Machapisho
    • Hali ya Uwekezaji
      • Business License Form
  • Kituo cha Habari
    • Video
    • Habari
    • Hotuba kwa Vyombo vya Habari
    • Maktaba ya Picha

KAYA 28 KUPEWA MAKAZI MBADALA OLDEAN

Posted on: February 27th, 2020

Mkuu wa wilaya ya Karatu Mh.Theresia Mahongo na wajumbe wa kamati ya ulinzi na usalama, wamefanya ziara  kwenye shamba la Muwekezaji na kukagua Makazi ya wafanyakazi Kiran huko Oldean.

 Ziara hiyo ililenga kukagua uimara wa nyumba za wananchi katika shamba la muwekezaji Sunial Aggarwal.Wakazi wanaoishi katka shamba hilo la Kiran wanaishi katika mazingira hatarishi baada ya nyumba zao kuwa na uchakavu wa muda mrefu. Mhe. Mahongo amesema eneo hilo lina wakazi wenye mkataba na Muwekezaji wa kufanya kazi na wakazi ambao hawana mkataba na Muwekezaji wa kufanya kazi. Mhe. Mahongo amemuelekeza Muwekezaji kuwapa makazi ya muda wananchi wote walio katika nyumba hizo 28 za muwekezaji.  

Mkuu wa wilaya ya Karatu Mhe. Theresia Mahongo akiwa mbele ya nyumba ya mkazi wa kiran iliyokuwa katika hali ya uchakavu.

Amemuelekeza Muwekezaji kuwapa notisi ya kuhama kwa wakazi wasio na mkataba wa kufanya kazi baada ya zoezi la kuhamisha kwenye makazi ya muda salama. Ameongeza kusema kama kutakuwa na wakazi watakaoendelea  kung’ang’ania kukaa kwenye  makazi ya muajiri basi ni vyema  Muwekezaji akaenda mahakamani kwa  hatua zaidi za kisheria.

 Mhe. Theresia Mahongo ametoa muda wa wiki mbili kwa uongozi wa shamba hilo la Kiran Kuhakikisha wananchi wanaoishi katika nyumba hizo kuwa wameshaondoka.  Amesema mwezi watatu kutakuwa na mvua kubwa zinazotarajiwa kunyesha na ni vyema muwekezaji wa shamba hilo akatafuta nyumba za kuhifadhi wananchi hao mapema ili nyumba hizo mbovu ziweze kubomolewa na kujengwa upya.

Mhe. Mahongo amewahakikishia wananchi hao kwamba watachukua orodha ya majina ya watoto wanaosoma na kuweka utaratibu ambao utasaidia watoto hao  kuendelea na elimu katika maeneo watakayo hamia. Mhe. Mahongo amemuelekeza Afisa Tarafa wa Karatu kusimamia zoezi hilo  la kuhamisha wakazi hao wa shamba la Kiran Estate Oldean.

Meneja Mkuu wa shambala Kiran Ndugu Davinder Singh amesema shamba hilo awali lilikuwa na kesi iliyokaa miaka 20 mahakamani na baada ya kesi kuisha mwaka 2011 shamba lilikuwa na hali mbaya. Amesema baada ya kesi walijikita katika  kufanya ukarabati mkubwa wa shamba,  na ilipofika wakati wa kuomba wananchi wasio na mkataba wa kazi na muwekezaji huyo walikataa kuondoka.

 Ndugu Omari Hamza ambaye naye ni Meneja ameomba ushirikiano kwa wananchi hao ili zoezi la kuwaondoa liweze kuenda vizuri, amesema kuna kipindi walileta trekta kuhamisha wafanyakazi saba lakini walikosa ushirikiano.

Mkuu wa wilaya ya Karatu Mhe. Theresia Mahongo (kulia) akizungumza na mkazi wa Kiran katika ziara yake ya kukagua makazi katika eneo hilo.

Matangazo

  • Matokeo ya upimaji wa Kitaifa kidoto cha pili January 07, 2024
  • Halmashauri ya Wilaya ya Karatu Uchaguzi wa Wanafunzi wa kidato cha kwanza, 2024 December 18, 2023
  • Matokeo ya Darasa la Nne January 07, 2024
  • NAFASI ZA KAZI 2024 April 21, 2024
  • Angalia Zote

Taarifa Mpya

  • MILIONI 400 ZATOLEWA KARATU, KUJENGA MABWENI NA MADARASA EYASI SEKONDARI

    January 30, 2025
  • WASIMAMIZI WAASWA KUSIMAMIA VIAPO VYAO KUELEKEA UCHAGUZI WA SERIKALI ZA MITAA 2024.

    November 23, 2024
  • JESHI LA AKIBA MKAWE WAZALENDO KWA TAIFA

    November 23, 2024
  • HALMASHAURI YAZINDUA KITABU CHA MPANGO MKAKATI WA UKUSANYAJI MAPATO.

    November 19, 2024
  • Angalia Zote

Video

DC KOLIMBA ATATUA KERO TARAFA YA EYASI KARATU
Video Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fursa za Uwekezaji

Viunganishi Linganifu

  • Tovuti ya Wizara ya Fedha na Mipango
  • Jamvi la Habari
  • Tovuti ya Tamisemi
  • Tovuti ya Serikali
  • Sekretarieti ya Ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Location Map

Wasiliana Nasi

    Karatu District Council

    Sanduku la Posta: P.O Box 190

    Simu: +255 272970648

    Simu ya Mkononi: 0754773947

    Barua Pepe: ded@karatudc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Haki Miliki @ 2017 Halmashauri ya Wilaya ya Karatu.Haki zote zimehifadhiwa