• Wasiliana Nasi |
    • Maswali |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Complains |
Karatu District Council
Karatu District Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Karatu

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Dhamira na Dira
    • Historia
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Fedha na Biashara
      • Ujenzi
      • Afya
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
    • Vitengo
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma Zetu
  • Madiwani
  • Miradi
    • TASAF
    • BOOST
  • Machapisho
    • Hali ya Uwekezaji
      • Business License Form
  • Kituo cha Habari
    • Video
    • Habari
    • Hotuba kwa Vyombo vya Habari
    • Maktaba ya Picha

KERO ZA WANANCHI MANUSAY, ZAPATA MAJIBU

Posted on: March 2nd, 2021

Watendaji wa serikali mnapaswa kuhakikisha mnawaelimisha wananchi wanaohitaji kupata ardhi ili wafuate taratibu zote za kupata ardhi katika eneo husika. Kushindwa kufuata taratibu za kupata ardhi kunasababisha  migogoro ya ardhi ambayo hujitokeza baada ya  kutokuelewana.

Hayo yamesemwa na Mkuu wa wilaya ya Karatu Mh, Abbas Kayanda alipokuwa akizungumza na wananchi katika kitongoji cha Manusay katika kijiji cha Endala. Amemuelekeza Mtendaji wa kijiji cha Endala kuhakikisha anasimamia kikamilifu ndani ya siku thelathini madai ya Bi, Benedeta Karama aliyedai eneo lake limetwaliwa kwa nguvu. Amesema lazima tusimamie misingi ya haki na tufuate taratibu na  miongozo katika utendaji wa shughuli za serikali.

Mh. Abbas Kayanda akizungumza na wananchi wa kitongoji cha Manusay 

Mh. Kayanda amemuelekeza Afisa tarafa wa tarafa ya Endabash Bi, Leina Swale kusimamia na kutatua mkwamo wa upatikanaji wa maji katika kijiji cha Endala, kijiji kiliingia makubaliano na Tyrilin safari lodge kwa masharti ya kuwasaidia kupata dp mbili za maji.

Kuhusu baraba Mh. Kayanda amesema barabara ya Endala ipo kwenye mpango wa ukarabati wa Tarura. Amesema mwaka huu wa fedha daraja moja linajengwa na bajeti ya mwaka ujao wa fedha kuna daraja jingine ambalo limeingizwa kwenye bajeti. Serikali inaendelea kutambua umuhimu wa barabara ya endala kwa sababu inaunganisha Endala na meneo mengine ya wilaya ya Karatu.

Katika hatua nyingine Mh. Abbas Kayanda ametembelea eneo la linalodaiwa kuwa linapatikana madini ya dhahabu katika kijiji cha Endala. Mh. Kayanda ameelekeza  uongozi wa serikali ya kijiji kusimamia taratibu ili kila mwenye uhitaji wa kujishughulisha uchimbaji wa madini  aweze kupata leseni inayomuwezesha  kujishughulisha na uchimbaji wa madini. Amesema ni vyema serikali ya kijiji itoe elimu ya kwa wachimbaji wadogo wadogo juu ya umuhimu wa kuwa na leseni.

Mh. Abbas Kayanda akizungumza katika eneo la machimbo katika kijiji cha Endala.

Naye Mwenyekiti wa kijiji cha Endala Ndg. Thomas Dawite amemshukuru Mkuu wa wilaya kwa ziara aliyofanya katika eneo hilo la machimbo madogo madogo.  Amesema wao kama Halmashauri ya kijiji walikuwa wanafurahia fedha ya ushuru waliokuwa wakipata katika machimbo hayo. Amesema sasa watasimamia na kuhakikisha kila mchimabaji anapata leseni ya uchimbaji wa madini.

Ameongeza kusema taratibu zilizowekwa na serikali juu ya ukataji wa leseni zinasaidia wachimbaji kutojiingiza na uchimbaji wa madini kiholela. Amesema utaratibu huo utasaidia pia katika utunzaji wa mazingira kwa sababu hakuna wachimbaji watakaojihusisha na uchimbaji wa madini kiholela bila kujiridhisha upatikanaji wake.

Matangazo

  • Matokeo ya upimaji wa Kitaifa kidoto cha pili January 07, 2024
  • Halmashauri ya Wilaya ya Karatu Uchaguzi wa Wanafunzi wa kidato cha kwanza, 2024 December 18, 2023
  • Matokeo ya Darasa la Nne January 07, 2024
  • NAFASI ZA KAZI 2024 April 21, 2024
  • Angalia Zote

Taarifa Mpya

  • MADAKTARI BINGWA WA SAMIA AWAMU YA TATU WATUA KARAU

    May 12, 2025
  • KARATU WASAPOTIJUHUDI ZA RAIS SAMIA WATANGAZA UTALII WA NDANI

    May 11, 2025
  • MILIONI 400 ZATOLEWA KARATU, KUJENGA MABWENI NA MADARASA EYASI SEKONDARI

    January 30, 2025
  • WASIMAMIZI WAASWA KUSIMAMIA VIAPO VYAO KUELEKEA UCHAGUZI WA SERIKALI ZA MITAA 2024.

    November 23, 2024
  • Angalia Zote

Video

DC KOLIMBA ATATUA KERO TARAFA YA EYASI KARATU
Video Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fursa za Uwekezaji

Viunganishi Linganifu

  • Tovuti ya Wizara ya Fedha na Mipango
  • Jamvi la Habari
  • Tovuti ya Tamisemi
  • Tovuti ya Serikali
  • Sekretarieti ya Ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Location Map

Wasiliana Nasi

    Karatu District Council

    Sanduku la Posta: P.O Box 190

    Simu: +255 272970648

    Simu ya Mkononi: 0754773947

    Barua Pepe: ded@karatudc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Haki Miliki @ 2017 Halmashauri ya Wilaya ya Karatu.Haki zote zimehifadhiwa