• Wasiliana Nasi |
    • Maswali |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Complains |
Karatu District Council
Karatu District Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Karatu

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Dhamira na Dira
    • Historia
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Fedha na Biashara
      • Ujenzi
      • Afya
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
    • Vitengo
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma Zetu
  • Madiwani
  • Miradi
    • TASAF
    • BOOST
  • Machapisho
    • Hali ya Uwekezaji
      • Business License Form
  • Kituo cha Habari
    • Video
    • Habari
    • Hotuba kwa Vyombo vya Habari
    • Maktaba ya Picha

KILELE CHA JUMA LA MAZINGIRA CHAFANYIKA KIPEKEE

Posted on: June 5th, 2019

Siku ya mazingira imeadhimishwa wilayani Karatu, kwa wadau wa siku ya mazingira kuokota taka pembezoni mwa barabara kuu. Zoezi la kuokota taka limeanza geti la Ngorongoro mpaka geti la Manyara likiongozwa na Afisa Mazingira ndugu Gadiye John.

Siku hii ya kilele cha juma la mazingira imeambatana na sikukuu ya Iddi pamoja na hali ya baridi kali na manyunyu hali iliyosababisha umande. Upekee wa siku hii ni namna Afisa mazingira alivyohamasisha kwa gari la matangazo, lakini pia kutumia usafiri binafsi kusomba taka na kuungwa mkono na wadau wa mazingira. Madhari ya barabara yalivyobadilika baada ya kufanya usafi wa kuondoa uchafu.

Ndugu Gadiye amesema leo ni  kilele cha juma la wiki ya mazingira. Tumeamua kuanza kufanya usafi kuanzia lango la mamlaka ya Ngorongoro kuelekea lango la mamlaka ya hifadhi ya ziwa Manyara. Amesema changamoto za mazingira ni kubwa ndio maana watu wamejitokeza, wadau walioalikwa ni theleathini na saba ambao ni hotel mbalimbali za kitalii lakini pia mamlaka ya hifadhi ya Ngorongoro na mamlaka ya hifadhi ya ziwa Manyara. Amesema eneo lilofanyiwa usafi wa mazingira ni takribani km 35.

Ndugu Gadiye amesema wamehamasisha wananchi kwa kupitisha gari la matangazo juu ya kilele cha juma la Mazingira. Lakini pia kuhamasisha watu kuacha kutumia mifuko ya plastiki na wamehamasika kufanya usafi katika maeneo yao ya makazi. Amesema mwananchi  akivunja sheria ya utunzaji mazingira sheria ziko wazi kwa sababu elimu imetolewa kuanzia ngazi ya kitongoji hadi eneo la katikati ya mji. Sheria zinazotumika ni sheria ya uhifadhi Mazingira ya mwaka 2004. Kuna sheria ndogo ya wilaya ya Karatu ya uhifadhi wa mazingira ambazo mtuhumiwa akipatikana na hatia anaweza kutozwa kiasi cha 50000 kama adhabu au kifungo cha miezi mitatu mpaka sita.

Ndugu Gadiye amesema zoezi la uhifadhi wa mazingira ni endelevu ndio maana hata taka zilizokusanywa ni kiasi kidogo. lakini pia upo mpango wa kuweka alama za kukataza kutupa taka hovyo sehemu mablimbali za mji lakini pia kutengeneza tangazo litakalokaa kwenye madirisha ya magari. Lengo ni kutoa uelewa mkubwa wananchi juu ya utunzaji wa mazingira na kuacha kutelekeza taka hovyo.

Wadau wakiotoka taka pembezoni wa barabara licha ya hali ya baridi kali.

Wadau wakiendelea na zoezi la kuokota taka katika barabara kuu wilayani Karatu.

Wadau wakikusanya taka na kuweka kwenye gari tayari kwenda kutupwa. 

Matangazo

  • Matokeo ya upimaji wa Kitaifa kidoto cha pili January 07, 2024
  • Halmashauri ya Wilaya ya Karatu Uchaguzi wa Wanafunzi wa kidato cha kwanza, 2024 December 18, 2023
  • Matokeo ya Darasa la Nne January 07, 2024
  • KIKAO CHA BARAZA LA MADIWANI 2024 May 11, 2024
  • Angalia Zote

Taarifa Mpya

  • MAAFISA UANDIKISHAJI WALA KIAPO KARATU

    May 14, 2025
  • DED HOKORORO ASHIRIKI KIKAO CHA ALAT WILAYA YA MERU

    May 15, 2025
  • MADAKTARI BINGWA WA SAMIA AWAMU YA TATU WATUA KARAU

    May 12, 2025
  • KARATU WASAPOTIJUHUDI ZA RAIS SAMIA WATANGAZA UTALII WA NDANI

    May 11, 2025
  • Angalia Zote

Video

DC KOLIMBA ATATUA KERO TARAFA YA EYASI KARATU
Video Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fursa za Uwekezaji

Viunganishi Linganifu

  • Tovuti ya Wizara ya Fedha na Mipango
  • Jamvi la Habari
  • Tovuti ya Tamisemi
  • Tovuti ya Serikali
  • Sekretarieti ya Ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Location Map

Wasiliana Nasi

    Karatu District Council

    Sanduku la Posta: P.O Box 190

    Simu: +255 272970648

    Simu ya Mkononi: 0754773947

    Barua Pepe: ded@karatudc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Haki Miliki @ 2017 Halmashauri ya Wilaya ya Karatu.Haki zote zimehifadhiwa