• Wasiliana Nasi |
    • Maswali |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Complains |
Karatu District Council
Karatu District Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Karatu

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Dhamira na Dira
    • Historia
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Fedha na Biashara
      • Ujenzi
      • Afya
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
    • Vitengo
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma Zetu
  • Madiwani
  • Miradi
    • TASAF
    • BOOST
  • Machapisho
    • Hali ya Uwekezaji
      • Business License Form
  • Kituo cha Habari
    • Video
    • Habari
    • Hotuba kwa Vyombo vya Habari
    • Maktaba ya Picha

KITUO CHA AFYA KAMBI YA SIMBA WAMEJIPANGA VIZURI

Posted on: March 30th, 2021

Na Tegemeo Kastus

Usimamizi na utoaji wa huduma za afya katika kituo cha afya Kambi ya simba umezidi kuimarika, hasa katika upatikanaji wa dawa na huduma za kitabibu zinazotolewa katika kituo hicho. Wananchi waliokuwa wakipokea huduma katika kituo hicho wamesema malalamiko ya ukosekanaji wa dawa kwa sasa hakuna.

Hayo yamebainika katika ziara ya Mkuu wa wilaya Mh.Abbas Kayanda alipotembelea kata ya Mbulumbulu kujionea hali ya utoaji wa huduma za afya ikiwa ni pamoja upatikanaji wa dawa. Mh. Kayanda ameoneshwa kuridhishwa na utendaji mzuri wa watendaji wa afya katika kituo hicho na ameelekeza magari ya dharura (ambulance) yaliyowekwa katika vituo vya afya kwa ajili ya kusaidia wagonjwa yabaki katika vituo vya afya husika badala ya kufanya shughuli nyingine.

Dkt. Jackline Nlula (kushoto) akimuonesha Mkuu wa wilaya Mh. Abbas Kayanda (kulia) vifaa tiba vinavyopatikana kituo cha afya Kambi ya simba.

Mh. Kayanda amesema gari linatakiwa kuwa (stand by) wakati wowote kwa ajili ya kusaidia wagonjwa, amesema kituo cha afya Kambi ya simba ni muhimu sana kwa wananchi wa Mbulumbulu kwa sababu kinapunguza umbali mrefu wa kwenda Karatu mjini kupata huduma za afya. Amehimiza watendaji wa afya kuweka utaratibu mzuri wa kuagiza dawa kabla hazijaisha ili wananchi waendelee kupata huduma. Sambamba na hilo Mh. Kayanda amehimiza wananchi kulipia bima za afya ili kujengea uwezo wa upatikanaji wa dawa katika zahanati na vituo vya afya. Serikali inatoa huduma za afya kwa watoto wa chini ya miaka mitano bure kinamama wajawazito na wazee wasiojiweza  bure ni sera ambayo serikali inaitekeleza katika kusaidia wananchi wake. Lazima wananchi tuoneshe uzalendo kwa kuisaidia serikali katika kuboresha miundo mbinu ya utoaji wa huduma za afya kwa kuchangia katika Ichf iliyoboreshwa inayowezesha watu 6 katika familia kulipia 30000 kwa mwaka.

Picha katika matukio mbalimbali wakati Mh. Abbas Kayanda akifanya ukaguzi kituo cha afya Kambi ya Simba

Katika hatua nyingine Mh. Kayanda amesikiliza kero katika ofisi ya kijiji cha Kambi ya simba ikiwa ni utaratibu aliojiwekea wa kusikiliza na kutatua kero za wananchi katika ngazi ya kata. Amewaelekeza watendaji kuhakikisha mashauri ya migogoro ya ardhi wanayaelekeza katika vyombo vilivyokasimiwa madaraka hayo, ili shauri likimalizika kusikilizwa katika vyombo liwe limeisha kwa mujibu wa sheria. Amesema kufanya hivyo kunasaidia watendaji wa serikali kusimamia maamuzi yaliyofanywa kulingana na hukumu ilivyoandikwa kisheria.

Mh. Kayanda amesema kufanya hivyo kutasaidia kupunguza kero za mashauri ya ardhi, amesema ni makosa kwa mtendaji kujadili hukumu iliyotolewa na mahakama au baraza la ardhi. Watendaji wanapaswa kushughulikia mashauri ya maswala ya ardhi kwa kuzingatia miongozo ya sheria badala ya kutumia utashi binafsi.

Naye Afisa Ardhi Mteule ndg. Faraji Rushagama amesema waziri wa ardhi ametoa fomu maalumu kwa ajili ya wananchi kuzijaza katika ngazi ya kata ili Mashauri ya ardhi yawe katika mpango taarifa (database) ili kujua mwenendo wa mashauri yote ya ardhi. Watendaji wa ardhi wapate nafasi ya kuyafanyia kazi mashauri yaliyondani ya uwezo wao au kuyapeleka katika vyombo vya maamuzi ili yapate nafasi ya kuanza kuchambuliwa na kutolewa maamuzi ya kisheria.

Matangazo

  • Matokeo ya upimaji wa Kitaifa kidoto cha pili January 07, 2024
  • Halmashauri ya Wilaya ya Karatu Uchaguzi wa Wanafunzi wa kidato cha kwanza, 2024 December 18, 2023
  • Matokeo ya Darasa la Nne January 07, 2024
  • KIKAO CHA BARAZA LA MADIWANI 2024 May 11, 2024
  • Angalia Zote

Taarifa Mpya

  • MAAFISA UANDIKISHAJI WALA KIAPO KARATU

    May 14, 2025
  • DED HOKORORO ASHIRIKI KIKAO CHA ALAT WILAYA YA MERU

    May 15, 2025
  • MADAKTARI BINGWA WA SAMIA AWAMU YA TATU WATUA KARAU

    May 12, 2025
  • KARATU WASAPOTIJUHUDI ZA RAIS SAMIA WATANGAZA UTALII WA NDANI

    May 11, 2025
  • Angalia Zote

Video

DC KOLIMBA ATATUA KERO TARAFA YA EYASI KARATU
Video Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fursa za Uwekezaji

Viunganishi Linganifu

  • Tovuti ya Wizara ya Fedha na Mipango
  • Jamvi la Habari
  • Tovuti ya Tamisemi
  • Tovuti ya Serikali
  • Sekretarieti ya Ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Location Map

Wasiliana Nasi

    Karatu District Council

    Sanduku la Posta: P.O Box 190

    Simu: +255 272970648

    Simu ya Mkononi: 0754773947

    Barua Pepe: ded@karatudc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Haki Miliki @ 2017 Halmashauri ya Wilaya ya Karatu.Haki zote zimehifadhiwa