• Wasiliana Nasi |
    • Maswali |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Complains |
Karatu District Council
Karatu District Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Karatu

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Dhamira na Dira
    • Historia
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Fedha na Biashara
      • Ujenzi
      • Afya
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
    • Vitengo
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma Zetu
  • Madiwani
  • Miradi
    • TASAF
    • BOOST
  • Machapisho
    • Hali ya Uwekezaji
      • Business License Form
  • Kituo cha Habari
    • Video
    • Habari
    • Hotuba kwa Vyombo vya Habari
    • Maktaba ya Picha

KUTUMIA FEDHA MBICHI NI MAKOSA

Posted on: January 27th, 2021

Na Tegemeo Kastus

Mtendaji yeyote wa serikali haruhusiwi kutumia fedha za makusanyo yeyote alizokusanya bila kupeleka fedha hizo bank kwenye akaunti ya serikali. Hiyo inasaidia watendaji wa serikali kuepuka matumizi mabaya ya fedha za serikali kwenye shughuli za miradi ya maendeleo.

Hayo yamesemwa na Mkuu wa wilaya ya Karatu Mh. Abbas Kayanda alipofanya ziara katika shule ya msingi Gidbaso kukagua ujenzi wa vyumba viwili vya madarasa na ofisi ya walimu vinavyojengwa na serikali ya kijiji na wananchi katika kata ya Endamarariek. Amesema lazima watendaji wafuate sheria na taratibu za kutumia fedha baada ya kuziweka fedha hizo kwenye akaunti maalumu ya kuhifadhi  fedha. Kutumia fedha bila kuzipeleka benki ni makosa kwa sababu  si utaratibu wa matumizi ya fedha za serikali.

Mh. Abbas Kayanda akizungumza na kamati ya ujenzi na wananchi katika shule ya Msingi Gidbaso

Mh. Kayanda amesema kitendo cha mtendaji wa kijiji cha Gidbaso kutumia fedha kwa ajili ujenzi wa madarasa bila  kuzipeleka benki kunasababisha kukosekane kwa uwazi wa mapato na matumizi. Ameagiza taasisi ya kuzuia na kupambana na rushwa (TAKUKURU) kufanya uchunguzi wa mapato na matumizi ya fedha zilizokusanywa na kijiji kwa ajili ya ujenzi wa vyumba vya madarasa.

 Katika hatua nyingine Mh. Kayanda amewapongeza wananchi wa kijiji cha Gidbaso kwa mwamuko wa kuchangia miradi ya maendeleo katika kijiji chao. Amehimiza wananchi kuendelea kuchangia ujenzi wa vyumba vya madarasa ili kuweza kufikia kiwango cha million 9 walizojiwekea, ambazo  mpaka sasa wameshachangia kiasi cha million 5.5 na ujenzi wa madarasa upo katika hatua ya ujenzi wa msingi. Amesema hakuna fedha  itakayochangwa na wananchi ambayo itapotea, maendeleo ya wananchi wa Gidibaso yataletwa na wana-Gidibaso wenyewe.

Sambamba na hilo Mh. Kayanda amemuelekeza Afisa Mtendaji kata wa kata ya Endamarariek kufuatilia mapato na matumizi ya fedha zilizochangwa na wazazi kwa ajili ya walimu wa muda waliokuwa wanafundisha shuleni hapo ili kujiridhisha kama kweli walimu hao walilipwa au hawakulipwa.  Amesema katika taarifa hiyo iainishe walimu hawakulipwa mwezi gani na fedha zilizokusanywa ni kiasi gani ?

Awali Ndg. Izrael  Tluway mkazi wa Gidbaso ameeleza kufurahishwa na ziara iliyofanywa  na mkuu wa wilaya amesema ziara hiyo imewapa ari ya kuongeza kasi ya ujenzi wa madarasa. Ndg Tluway amemuomba mkuu wa wilaya kufuatilia  madai ya malipo ya  walimu wa muda kwa sababu ya  kukosekana kwa uwazi wa taarifa za walimu hao wa muda  katika shule ya msingi Gidbaso hivyo kushindwa kulipwa kwa wakati stahiki zao. Amesema walimu hao wamekuwa wakilalamika kutolipwa fedha zao kwa wakati na hivyo kushindwa kuendelea kufundisha.


Mh. Abbas Kayanda akizungumza na  wananchi

Matangazo

  • Matokeo ya upimaji wa Kitaifa kidoto cha pili January 07, 2024
  • Halmashauri ya Wilaya ya Karatu Uchaguzi wa Wanafunzi wa kidato cha kwanza, 2024 December 18, 2023
  • Matokeo ya Darasa la Nne January 07, 2024
  • NAFASI ZA KAZI 2024 April 21, 2024
  • Angalia Zote

Taarifa Mpya

  • MILIONI 400 ZATOLEWA KARATU, KUJENGA MABWENI NA MADARASA EYASI SEKONDARI

    January 30, 2025
  • WASIMAMIZI WAASWA KUSIMAMIA VIAPO VYAO KUELEKEA UCHAGUZI WA SERIKALI ZA MITAA 2024.

    November 23, 2024
  • JESHI LA AKIBA MKAWE WAZALENDO KWA TAIFA

    November 23, 2024
  • HALMASHAURI YAZINDUA KITABU CHA MPANGO MKAKATI WA UKUSANYAJI MAPATO.

    November 19, 2024
  • Angalia Zote

Video

DC KOLIMBA ATATUA KERO TARAFA YA EYASI KARATU
Video Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fursa za Uwekezaji

Viunganishi Linganifu

  • Tovuti ya Wizara ya Fedha na Mipango
  • Jamvi la Habari
  • Tovuti ya Tamisemi
  • Tovuti ya Serikali
  • Sekretarieti ya Ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Location Map

Wasiliana Nasi

    Karatu District Council

    Sanduku la Posta: P.O Box 190

    Simu: +255 272970648

    Simu ya Mkononi: 0754773947

    Barua Pepe: ded@karatudc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Haki Miliki @ 2017 Halmashauri ya Wilaya ya Karatu.Haki zote zimehifadhiwa