• Wasiliana Nasi |
    • Maswali |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Complains |
Karatu District Council
Karatu District Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Karatu

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Dhamira na Dira
    • Historia
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Fedha na Biashara
      • Ujenzi
      • Afya
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
    • Vitengo
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma Zetu
  • Madiwani
  • Miradi
    • TASAF
    • BOOST
  • Machapisho
    • Hali ya Uwekezaji
      • Business License Form
  • Kituo cha Habari
    • Video
    • Habari
    • Hotuba kwa Vyombo vya Habari
    • Maktaba ya Picha

LAZIMA TUANZE KUTENGA MAENEO KWA AJILI YA MALISHO YAMIFUGO

Posted on: October 19th, 2020

NA TEGEMEO KASTUS

Uongozi wa kijiji cha chemchem wahimizwa kuanza kutenga maeneo kwa ajili ya malisho ya mifugo . Kutengwa maeneo kwa ajili ya malisho ya mifugo kutasaidia ufugaji wenye tija na unaolenga kupata mifugo yenye afya bora.

Hayo yamesemwa na Mkuu wa wilaya ya Karatu Mh. Abbas Kayanda wakati akizindua maonesho ya tatu ya uogeshaji wa mifugo yenye kauli mbiu ‘kuogesha kwa afya na ufugaji wenye tija”.  Uzinduzi huo umefanyika kiwilaya katika kijiji cha Chemchem kata ya Rhotia. Amesema lazima wafugaji waanze kutenga maeneo kwa ajili ya malisho ili kusaidia mifugo kupata chakula wakati wote. Nasikutenga tu bali kufuata maelekezo ya kitaalamu kujua ni aina gani za nyasi zina


zofaa kupandwa kwa ajili ya kulisha mifugo katika maeneo ambayo yatakuwa yametengwa ili kuwa na ufugaji wenye tija.

Mkuu wa wilaya ya Karatu Mh. Abbas Kayanda akiwa katika zoezi ka uogeshaji wa mifugo kijiji cha Chemchem

Mh. Kayanda ametoa wito kwa wafugaji  kuacha ufugaji huria na badala yake kufanya ufugaji wa kisasa. Wafugaji tunapaswa kuongeza ubora wa bidhaa zetu ili tuweze kupata soko zuri na kuinua hali ya maisha yetu. Amesema serikali kwa kulitambua hilo ndio maana imeanzisha uogeshaji wa mifugo.  Kuogesha mifugo inasaidia kukinga mifugo na maradhi lakini pia inasaidia mfugo kuwa na afya bora. Serikali imeenda mbali ndio maana  imetaka kuwe na kamati za usimamizi wa majosho.

Mh. Kayanda amesema  kuogesha mifugo haimaanishi kuogesha ng’ombe peke yake tunatakiwa tuogeshe ng’ombe mbuzi kondoo na hata punda. Amesema ukiogesha baadhi ya mifugo na kuacha mifugo mingine tatizo la magonjwa litaendelea kuwepo. Mifugo ambayo haijaogeshwa ni rahisi kuaambukiza mifugo iliyoogeshwa. Wafugaji lazima wazingatie usafi wa zizi la ngombe, zizi   linatakiwa kufanyiwa usafi na kupigwa dawa ili kuuwa mazalia ya kupe, amesema kama mifugo itaoshwa na kurudishwa kwenye zizi ambalo halikufanyiwa usafi na kupigwa dawa bado tatizo linakuwa halijatatuliwa.

Mh. Kayanda ameelekeza Maafisa Mifugo kukaa karibu na wafugaji na kuwapa elimu  juu ya ufugaji wa kisasa. Lakini pia kutoa elimu ya namna wafugaji wanaweza kutenga sehemu ya maeneo yao ya kilimo kwa ajili ya malisho. Amesema  Elimu ya ufugaji wa kisasa itawasaidia wafugaji kunufaika na mifugo yao na kuboresha hali ya maisha kuanzia kipato cha mtu mmoja mmoja na familia kwa ujumla.

Mh Kayanda amewaambia wafugaji wa kijiji cha Chemchem ikifika wakati wa kuchangia fedha kwa ajili  kununua dawa za majosho wawe tayari kuchangia. Kila mfugaji atakayechangia ahakikishe anapewa risiti. Amesema risiti itaondoa changamoto za ubadhilifu wa fedha kwenye uendeshaji wa Majosho.

Awali Afisa mifugo wa wilaya ya Karatu ndg. Denis Buberwa amesema kuna lita 162 zilizogawiwa na serikali kwa ajili ya zoezi la  kuogesha wa mifugo wilayani Karatu. Amesema Madawa ya kuogesha mifugo yanakuja kwa mwaka mara mbili.  Wilaya ya karatu  mpaka sasa ina jumla ya majosho 15.

Matangazo

  • Matokeo ya upimaji wa Kitaifa kidoto cha pili January 07, 2024
  • Halmashauri ya Wilaya ya Karatu Uchaguzi wa Wanafunzi wa kidato cha kwanza, 2024 December 18, 2023
  • Matokeo ya Darasa la Nne January 07, 2024
  • NAFASI ZA KAZI 2024 April 21, 2024
  • Angalia Zote

Taarifa Mpya

  • MILIONI 400 ZATOLEWA KARATU, KUJENGA MABWENI NA MADARASA EYASI SEKONDARI

    January 30, 2025
  • WASIMAMIZI WAASWA KUSIMAMIA VIAPO VYAO KUELEKEA UCHAGUZI WA SERIKALI ZA MITAA 2024.

    November 23, 2024
  • JESHI LA AKIBA MKAWE WAZALENDO KWA TAIFA

    November 23, 2024
  • HALMASHAURI YAZINDUA KITABU CHA MPANGO MKAKATI WA UKUSANYAJI MAPATO.

    November 19, 2024
  • Angalia Zote

Video

DC KOLIMBA ATATUA KERO TARAFA YA EYASI KARATU
Video Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fursa za Uwekezaji

Viunganishi Linganifu

  • Tovuti ya Wizara ya Fedha na Mipango
  • Jamvi la Habari
  • Tovuti ya Tamisemi
  • Tovuti ya Serikali
  • Sekretarieti ya Ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Location Map

Wasiliana Nasi

    Karatu District Council

    Sanduku la Posta: P.O Box 190

    Simu: +255 272970648

    Simu ya Mkononi: 0754773947

    Barua Pepe: ded@karatudc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Haki Miliki @ 2017 Halmashauri ya Wilaya ya Karatu.Haki zote zimehifadhiwa