• Wasiliana Nasi |
    • Maswali |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Complains |
Karatu District Council
Karatu District Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Karatu

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Dhamira na Dira
    • Historia
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Fedha na Biashara
      • Ujenzi
      • Afya
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
    • Vitengo
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma Zetu
  • Madiwani
  • Miradi
    • TASAF
    • BOOST
  • Machapisho
    • Hali ya Uwekezaji
      • Business License Form
  • Kituo cha Habari
    • Video
    • Habari
    • Hotuba kwa Vyombo vya Habari
    • Maktaba ya Picha

LAZIMA TUTUNZE VYANZO VYA MAJI

Posted on: August 7th, 2020

NA TEGEMEO KASTUS

Wananchi wanaolima ndani ya mita 60 kwenye chanzo cha maji, wamepewa muda wa kuondoka kwa hiari yao wenyewe. Ili kuendelea kulinda vyanzo vya maji kwa kizazi cha sasa na kizazi cha baadae. Kuhifadhi vyanzo cha maji  ni jambo la kisheria.

Hayo yamesema na mkuu wa wilaya ya Karatu Mh. Abbas Kayanda, wakati akizungumza na wananchi katika mkutano wa hadhara Mbuganyekundu. Amesema awali wananchi wanaojihusisha na kilimo kwenye vyanzo vya maji ambavyo viliwekewa mipaka (becon)  mwezi wa pili na  zoezi hilo kuzinduliwa na mkuu wa mkoa,   walikaa kwenye mikutano na kukubaliana mwisho wa kulima ni mwezi wa saba tarehe 12 mwaka huu. Mh. Kayanda ameagiza mpaka kufika siku ya jumatatu wawe wameondoka wenyewe kwenye maeneo hayo kwa hiari yao.

Mh. Abbas Kayanda katika matukio tofauti wakati wa mkutano wa hadhara na wananchi wa Mbuga nyekundu Mang'ola.

Mh. Kayanda amesema kumekuwa na tabia kwa baadhi ya wananchi kufanya fujo pindi changamoto kwenye mikondo ya umwagiliaji inapotokea. Amesema wananchi wanapaswa kufuata utaratibu wa kuwasilisha malalamiko nasikujikusanya na kufanya fujo. Amesema mkiwakilisha changamoto kwa uongozi wa mikondo ya umwagiliaji watawasIlisha kwenye uongozi wa Jumuiya ya watumia maji bonde dogo la Eyasi (JUWAMABOE) na wataitatua.

Mkuu wa wilaya ya Karatu Mh. Abbas Kayanda akizungumza wananchi wakati wa mkutano wa hadhara Mbuganyekundu Mang'ola.

 Mh. Kayanda ameelekeza uongozi wote wa JUWAMABOE kukaa  kikao na kutatua tatizo la umwagiliaji  masaa tisa ambalo linalamikiwa  na watumiaji mikondo ya umwagiliaji maji Mbuga nyekundu. Amesema ni vyema Juwamaboe kukaa na kutumia busara katika kutatua mvutano huo wa masaa tisa ya umwagiliaji.

katika mkutano huo Mh. Kayanda amegusia swala la kuchangia maendeleo amesema lazima wananchi wajitolee kuchangia ujenzi wa miradi ya maendeleo. Kuna michango ya ujenzi wa maabara kituo cha mbuga nyekundu na kijiji kinadaiwa kuchangia million 13 na hazijatolewa. Amesema katika ujenzi wa bweni shule ya sekondari Baray,  kijiji cha Mbuga nyekundu kinadaiwa million 6. Miradi hii ni ya kwetu sisi sote

Matangazo

  • Matokeo ya upimaji wa Kitaifa kidoto cha pili January 07, 2024
  • Halmashauri ya Wilaya ya Karatu Uchaguzi wa Wanafunzi wa kidato cha kwanza, 2024 December 18, 2023
  • Matokeo ya Darasa la Nne January 07, 2024
  • NAFASI ZA KAZI 2024 April 21, 2024
  • Angalia Zote

Taarifa Mpya

  • MILIONI 400 ZATOLEWA KARATU, KUJENGA MABWENI NA MADARASA EYASI SEKONDARI

    January 30, 2025
  • WASIMAMIZI WAASWA KUSIMAMIA VIAPO VYAO KUELEKEA UCHAGUZI WA SERIKALI ZA MITAA 2024.

    November 23, 2024
  • JESHI LA AKIBA MKAWE WAZALENDO KWA TAIFA

    November 23, 2024
  • HALMASHAURI YAZINDUA KITABU CHA MPANGO MKAKATI WA UKUSANYAJI MAPATO.

    November 19, 2024
  • Angalia Zote

Video

DC KOLIMBA ATATUA KERO TARAFA YA EYASI KARATU
Video Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fursa za Uwekezaji

Viunganishi Linganifu

  • Tovuti ya Wizara ya Fedha na Mipango
  • Jamvi la Habari
  • Tovuti ya Tamisemi
  • Tovuti ya Serikali
  • Sekretarieti ya Ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Location Map

Wasiliana Nasi

    Karatu District Council

    Sanduku la Posta: P.O Box 190

    Simu: +255 272970648

    Simu ya Mkononi: 0754773947

    Barua Pepe: ded@karatudc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Haki Miliki @ 2017 Halmashauri ya Wilaya ya Karatu.Haki zote zimehifadhiwa