• Wasiliana Nasi |
    • Maswali |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Complains |
Karatu District Council
Karatu District Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Karatu

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Dhamira na Dira
    • Historia
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Fedha na Biashara
      • Ujenzi
      • Afya
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
    • Vitengo
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma Zetu
  • Madiwani
  • Miradi
    • TASAF
    • BOOST
  • Machapisho
    • Hali ya Uwekezaji
      • Business License Form
  • Kituo cha Habari
    • Video
    • Habari
    • Hotuba kwa Vyombo vya Habari
    • Maktaba ya Picha

MAAFISA WAANDIKISHAJI WAPEWA NASAHAA

Posted on: July 15th, 2019

Semina ya wataalamu wa BVR na Maafisa wasaidizi waandikishaji imefanyika katika ukumbi wa Karatu sekondari. Semina hiyo ya siku mbili imelenga kuwajengea uwezo maafisa waandikishaji wasaidizi utayari wa kufanya  maboresho ya daftari la mpiga kura, zoezi linategemea kuanza siku chache  zijazo 18/7/2019.

Mgeni rasmi wa mafunzo hayo Ndugu Abbas Kayanda katibu tawala wa wilaya ya Karatu;  alyefungua semina hiyo, amesema zoezi hilo ni muhimu sana kwa wataalamu wa BVR na maafisa wasaidizi. Tunataka wilaya ya Karatu iwe wilaya ya kwanza kufanya vizuri katika zoezi la uandikishaji kwa mkoa wa arusha. Amesema atakuwa anapita katika maeneo mbalimbali ya vituo kujionea utekelezaji wa zoezi hilo. Tusikubali kushindwa na wilaya nyingine, kwa sababu tumefanya maandalizi mazuri kwa ajili ya utekelezaji wa zoezi hili.

      Picha ni wataalamu wanaotarajiwa kufanya zoezi la BVR wakiskiliza hotuba ya mgeni rasmi.

Ndugu Kayanda amewaasa waandikishaji juu ya kutunza vifaa hivyo, amesema kupewa mashine ni kupewa dhamana. Tukiharibu mashine hizi inatia doa kwa sababu zinategemewa kutumika sehemu nyingine baada ya zoezi kumalizika Karatu. Hifadhi mashine sehemu salama, kwa sababu chochote kikitokea cha uharibifu kwenye mashine ya BVR KIT utawajibishwa. Amesema si vyema kuwajibishana kwa vitu visivyo na msingi sana. Nimatumaini yetu kwamba vifaa hivyo vitatunzwa ili viende vikatumike sehemu nyingine.

Ndugu Kayanda amehimiza ushirikiano katika utendaji kazi wa zoezi la maboresho ya daftari la wapiga kura. Amesema tusiende tukaanza kutunishiana misuli kuonesha nani ni mkubwa katika kazi tunayoenda kufanya, siyo lengo la kazi hii. Amesema bila ushirikiano hatuwezi kufanya vizuri wenyewe, na busara lazima itumike wakati wa utekelezaji wa zoezi hilo. Amesema katika zoezi hilo kutakuwa na mawakala wa vyama vya siasa; ambao wanaruhusiwa kuwepo ili kuona zoezi hili namna gani linavyoenda, amewaomba wataalamu hao kuwapa ushirikiano. Amesema wapeni ushirikiano ili waone namna gani zoezi hili linafanyika katika hali ya uwazi. Amesema mawakala wa siasa hawaruhusiwi kuingilia kazi ambazo mnazifanya, wala kukupangia kitu unachopaswa kukifanya. Wapo mawakala wa vyama vya siasa huwa wanajifanya wanajua zaidi kuliko wewe uliyepewa kazi hiyo. Amesema mawakala wa siasa wanapaswa kusema, kama kuna shida yeyote ili aweze kusaidiwa lakini si kuingilia utaratibu unaofanywa katika uandikishaji.


Moja ya mwandikishaji akitafakari jambo

Ndugu Kayanda amesema katika utekelezaji wa zoezi hilo la maboresho ya daftari la mpiga kura, amewaasa watendaji hao kutoa vipaombele kwa  wagonjwa, wazee, kinamama wajawazito, na walemavu. Amehimiza busara kutumika katika zoezi hilo kwa sababu linahusu mstakabali wa watu katika upande wa demokrasia. Uzoefu unaonesha katika kazi hizi hasa siku za mwanzo, watu huwa hawajitokezi wengi, lakini  hiyo siyo sababu ya kufunga kituo lazima tufanye kazi kwa kuzingatia maelekezo.

Afisa Mwandikishaji Ndugu Waziri Mourice amesema kuna ziada ya watu 4  kila kata, ili dharura ikitokea kwa mmoja wa waandikishaji nafasi iliyoachwa wazi ijazwe na waandikishaji hao wa ziada. amesema kutakuwa na watu wa BVR KIT 56  na waandikishaji wasaidizi 56. Maafisa hao wamehudhuriwa mafunzo hayo ya Maafisa waandikishahji na kuapishwa kiapo cha kutunza siri na kiapo cha kutokuwa mwanachama wa kisiasa. Amesema kufanya hivyo kuna wafanya waandikishaji kuwa huru kufanya shughuli za serikali kwa uhuru bila mfungamano na chama cha siasa. Ndugu Waziri Mourice amesema wataalamu wa BVR KIT na Maafisa waandikishaji watakaojihusisha na zoezi hilo ni 556 ukijumlisha na wale maafisa wa ziada.


Umakini wa kusikiliza wakati mgeni rasmi anazungumza.

Matangazo

  • Matokeo ya upimaji wa Kitaifa kidoto cha pili January 07, 2024
  • Halmashauri ya Wilaya ya Karatu Uchaguzi wa Wanafunzi wa kidato cha kwanza, 2024 December 18, 2023
  • Matokeo ya Darasa la Nne January 07, 2024
  • NAFASI ZA KAZI 2024 April 21, 2024
  • Angalia Zote

Taarifa Mpya

  • MILIONI 400 ZATOLEWA KARATU, KUJENGA MABWENI NA MADARASA EYASI SEKONDARI

    January 30, 2025
  • WASIMAMIZI WAASWA KUSIMAMIA VIAPO VYAO KUELEKEA UCHAGUZI WA SERIKALI ZA MITAA 2024.

    November 23, 2024
  • JESHI LA AKIBA MKAWE WAZALENDO KWA TAIFA

    November 23, 2024
  • HALMASHAURI YAZINDUA KITABU CHA MPANGO MKAKATI WA UKUSANYAJI MAPATO.

    November 19, 2024
  • Angalia Zote

Video

DC KOLIMBA ATATUA KERO TARAFA YA EYASI KARATU
Video Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fursa za Uwekezaji

Viunganishi Linganifu

  • Tovuti ya Wizara ya Fedha na Mipango
  • Jamvi la Habari
  • Tovuti ya Tamisemi
  • Tovuti ya Serikali
  • Sekretarieti ya Ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Location Map

Wasiliana Nasi

    Karatu District Council

    Sanduku la Posta: P.O Box 190

    Simu: +255 272970648

    Simu ya Mkononi: 0754773947

    Barua Pepe: ded@karatudc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Haki Miliki @ 2017 Halmashauri ya Wilaya ya Karatu.Haki zote zimehifadhiwa