• Wasiliana Nasi |
    • Maswali |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Complains |
Karatu District Council
Karatu District Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Karatu

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Dhamira na Dira
    • Historia
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Fedha na Biashara
      • Ujenzi
      • Afya
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
    • Vitengo
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma Zetu
  • Madiwani
  • Miradi
    • TASAF
    • BOOST
  • Machapisho
    • Hali ya Uwekezaji
      • Business License Form
  • Kituo cha Habari
    • Video
    • Habari
    • Hotuba kwa Vyombo vya Habari
    • Maktaba ya Picha

MADIWANI WATATU SASA RASMI CCM

Posted on: April 3rd, 2019

Katibu Muenezi wa Chama Cha Mapinduzi Taifa, na Mlezi wa Chama Cha Mapinduzi mkoa wa Arusha Ndugu Humphrey Polepole leo amewapokea madiwani watatu waliojiuzulu unachama  katika Chama Cha Demokrasia Maendeleo wilayani Karatu.

Hafla ya kuwapokea na kuwaapisha ilifanyika ndani ya ofisi za ccm wilayani Karatu, madiwani waliojiuzulu ni Lazaro Bajuta kutoka kata ya Ganako, Benedicto Modaha kutoka kata ya Daa na Amani Hotay kutoka kata ya Mbulumbulu pamoja na Ndugu John  Zakaria.

Ndugu Polepole amewapongeza madiwani hao kwa kuwapa Chama cha Mapinduzi heshima kubwa. Sambamba na kuwapokea wanachama hao wapya Ndugu Polepole ametoa maelekezo ya Chama Cha Mapinduzi kwa serikali, amesema Karatu kumekuwa na mamlaka mbili za maji KAVIWASU na KARUWASA. KAVIWASU inatoza unit moja ya maji ni Tsh.3000 na KARUWASA inatoza  Unit moja Tsh.1750. Si haki kwa watu kutozwa bei tofauti kwa maji yale yale, amesema baada ya mchakato unaoendelea sasa mamlaka zote za maji zitakuwa chini ya serikali ya Jamhuri ya Mungano wa Tanzania. Ndugu Polepole ameelekeza uchaguzi wa KAVIWASU uliokuwa ufanyike tarehe 19 mwezi huu usimame na wasubiri maelekezo ya wizara ya maji. Serikali inapokea maelekezo ya chama cha mapinduzi na hayo aliyoyaelekeza ni maelekezo ya Chama Cha Mapinduzi.

Ndugu Lazaro Bajuta aliyekuwa makamu mwenyekiti wa Halmashauri ya wilaya ya Karatu: amesema kuhama kwao chama ni utashi wao binafsi, amesema ameona mlima aliokuwa akiupanda ambao haupandiki. Amesema juhudi ya serikali ya chama cha mapinduzi katika utekelezaji wa mambo mbalimbali  mazuri zimekuwa wazi kwa wananchi lakini baadhi ya watu wamekuwa wakibeza.  Amesema amerudi nyumbani na hahitaji ushirika kwenye maamuzi yake binafsi, ametoka kwao kwa sababu hakuwa wakwao. Amesema kituo cha afya Mbulumbulu serikali imetoa milioni 500,   kituo cha afya Endabash serikali imetoa milioni 400. Hiyo ni baadhi ya miradi ambayo imegharamiwa na kutekelezwa na serikali ya awamu ya tano  kwa kipindi cha miaka mitatu chini ya uongozi wa Mhe. Rais Dkt. John Pombe Magufuli.

Ndugu Benedicto Modaha ambaye alikuwa diwani wa Daa, amesema baada ya  uchaguzi mkuu Arusha ilikuwa na mbunge mmoja wa CCM aliyekuwa akitoka wilaya ya Ngorongoro. Leo kuna wabunge wawili tuu wa upinzani mkoa wa Arusha. Baada ya uchaguzi mkuu wilaya ya Karatu ilikuwa madiwani wa Chadema kumi na wanne Ccm, lakini  hivi sasa Chadema imebaki na madiwani wanne katika Halmashauri ya Karatu


Ndugu Polepole kushoto akiongoza  wanachama wapya wa Chama cha mapinduzi  mkono wa kulia  kula kiapo cha utii, cha kukitumikia Chama cha Mapinduzi.

Matangazo

  • Matokeo ya upimaji wa Kitaifa kidoto cha pili January 07, 2024
  • Halmashauri ya Wilaya ya Karatu Uchaguzi wa Wanafunzi wa kidato cha kwanza, 2024 December 18, 2023
  • Matokeo ya Darasa la Nne January 07, 2024
  • KIKAO CHA BARAZA LA MADIWANI 2024 May 11, 2024
  • Angalia Zote

Taarifa Mpya

  • MAAFISA UANDIKISHAJI WALA KIAPO KARATU

    May 14, 2025
  • DED HOKORORO ASHIRIKI KIKAO CHA ALAT WILAYA YA MERU

    May 15, 2025
  • MADAKTARI BINGWA WA SAMIA AWAMU YA TATU WATUA KARAU

    May 12, 2025
  • KARATU WASAPOTIJUHUDI ZA RAIS SAMIA WATANGAZA UTALII WA NDANI

    May 11, 2025
  • Angalia Zote

Video

DC KOLIMBA ATATUA KERO TARAFA YA EYASI KARATU
Video Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fursa za Uwekezaji

Viunganishi Linganifu

  • Tovuti ya Wizara ya Fedha na Mipango
  • Jamvi la Habari
  • Tovuti ya Tamisemi
  • Tovuti ya Serikali
  • Sekretarieti ya Ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Location Map

Wasiliana Nasi

    Karatu District Council

    Sanduku la Posta: P.O Box 190

    Simu: +255 272970648

    Simu ya Mkononi: 0754773947

    Barua Pepe: ded@karatudc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Haki Miliki @ 2017 Halmashauri ya Wilaya ya Karatu.Haki zote zimehifadhiwa