• Wasiliana Nasi |
    • Maswali |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Complains |
Karatu District Council
Karatu District Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Karatu

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Dhamira na Dira
    • Historia
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Fedha na Biashara
      • Ujenzi
      • Afya
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
    • Vitengo
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma Zetu
  • Madiwani
  • Miradi
    • TASAF
    • BOOST
  • Machapisho
    • Hali ya Uwekezaji
      • Business License Form
  • Kituo cha Habari
    • Video
    • Habari
    • Hotuba kwa Vyombo vya Habari
    • Maktaba ya Picha

MAJI NI RASILIMALI MUHIMU

Posted on: June 12th, 2019

Kiongozi wa mbio za mwenge wa uhuru kitaifa ndugu Mzee mkongea Alli, amesema mwenge wa uhuru uliasisiwa na Baba wa taifa mwalimu Julius Kambarage Nyerere. Mwaka huu ni mwaka wa ishirini tangu Baba wa taifa alipofariki. Amesema kwa kuenzi mchango wake  ndio maana wamedhamiria kufanya kazi bila kuchoka.

Ndugu Mkongea amesema pia wataendelea kupigana na adui ujinga maradhi na umaskini.Ndugu Mkongea amesema kauli mbiu ya mwenge mwaka huu ni “maji ni haki ya kila mtu, tutunze vyanzo vyake tukumbuke  kushiriki uchaguzi wa serikali za mitaa”  Ndugu Mzee Mkongea amesema maji ni rasilimali muhimu sana. Kupitia ilani ya chama cha mapinduzi (2015-2020) kufikia mwaka 2020 itahakikisha wananchi wanaoishi vijijini wanapata maji kwa asilimia themanini na tano. Ndugu Mkongea amesema miradi ipatayo 1659 imeweza kukamilishwa kwa upande wa vijijini. Ndugu Mkongea amesema wananchi wanoishi mjini ifikapao 2020 watapata maji kufikia aslimia tisini na tano. Miradi ipatayo 124 imekamilishwa kwa wakati kwa kipindi cha (2016-2018) sera za kimkakati za kuchimba visima virefu na vikubwa ambavyo vimegharimu shilingi billion kumi na nane za Kitanzania.


Ndugu Mkongea amesema mwezi wa kumi serikali inaingia kwenye uchaguzi wa serikali za mitaa. Amewaomba wananchi kujitokeza kwa wingi kusikiliza sera za wagombea na kupiga kura. Amewaomba wananchi kujitokeza kugombea na pia amesihi wananchi kuchagua viongozi bora wenye hofu ya mungu. Viongozi wa serikali za mitaa wanachangia katika shughuli za maendeleo kutunza mazingira. Serikali za mitaa zinachangia sana katika kutunza ulinzi na usalama. Ndugu Mkongea amesema kwenye uchaguzi kuna kushinda na kushindwa ni vyema atakayeshindwa kukubali matokeo na kutoa ushirikiano kwa aliyeshinda.

Ndugu Mkongea amesema bado swala la maambukizi ya ukimwi   ni changamoto, wastani wa maambukizi ni asilimia nne nukta saba. Mkoa unaongoza kwa maambukizi ni mkoa wa Njombe 11.4%  na  mkoa wa Iringa unafuata 11.3 % mkoa wa Mbeya unafuata  9.3%  na mkoa wa Mwanza unafuata 7.2 %. Ndugu Mkongea amesema maambuki mapya kwa mwaka ni watu 81000 na kwa sasa kuna watu wanasadikiwa1400,000 wanaishi na virusi vya ukimwi. Ndugu Mkongea amesema mambukizi ya ukimwi ni changamoto kwa nchi. Ameombwa wananchi kujitokeza kupima amesema ukibainika utapewa ushauri nasaha. Ameombwa wananchi wasiwanyanyapae watu walioadhirika na ukimwi amesema kuishi na virusi vya ukimwi siyo mwisho wa maisha.

Ndugu Mkongea amesema mwenge bado unaendelae na mapambano dhidi ya madawa ya kulevya. Ameomba wananchi kushirikiana pamoja, dhidi ya vita hiyo ya madawa ya kulevya chini ya kauli mbiu, Tujenge maisha yetu, jami yetu, Utu wetu, bila matumizi ya dawa za kulevya. Ndugu Mkongea amesema bado mbio za mwenge zinaendeleza  mapambano dhidi ya rushwa chini ya kauli mbiu kataa rushwa jenga Tanzania. Mwenge wa uhuru unaendelea na mapambano dhidi ya malaria chini ya kauli mbiu mimi niko tayari kutokomeza malaria, wewe je ?

Matangazo

  • Matokeo ya upimaji wa Kitaifa kidoto cha pili January 07, 2024
  • Halmashauri ya Wilaya ya Karatu Uchaguzi wa Wanafunzi wa kidato cha kwanza, 2024 December 18, 2023
  • Matokeo ya Darasa la Nne January 07, 2024
  • KIKAO CHA BARAZA LA MADIWANI 2024 May 11, 2024
  • Angalia Zote

Taarifa Mpya

  • MAAFISA UANDIKISHAJI WALA KIAPO KARATU

    May 14, 2025
  • DED HOKORORO ASHIRIKI KIKAO CHA ALAT WILAYA YA MERU

    May 15, 2025
  • MADAKTARI BINGWA WA SAMIA AWAMU YA TATU WATUA KARAU

    May 12, 2025
  • KARATU WASAPOTIJUHUDI ZA RAIS SAMIA WATANGAZA UTALII WA NDANI

    May 11, 2025
  • Angalia Zote

Video

DC KOLIMBA ATATUA KERO TARAFA YA EYASI KARATU
Video Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fursa za Uwekezaji

Viunganishi Linganifu

  • Tovuti ya Wizara ya Fedha na Mipango
  • Jamvi la Habari
  • Tovuti ya Tamisemi
  • Tovuti ya Serikali
  • Sekretarieti ya Ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Location Map

Wasiliana Nasi

    Karatu District Council

    Sanduku la Posta: P.O Box 190

    Simu: +255 272970648

    Simu ya Mkononi: 0754773947

    Barua Pepe: ded@karatudc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Haki Miliki @ 2017 Halmashauri ya Wilaya ya Karatu.Haki zote zimehifadhiwa