• Wasiliana Nasi |
    • Maswali |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Complains |
Karatu District Council
Karatu District Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Karatu

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Dhamira na Dira
    • Historia
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Fedha na Biashara
      • Ujenzi
      • Afya
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
    • Vitengo
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma Zetu
  • Madiwani
  • Miradi
    • TASAF
    • BOOST
  • Machapisho
    • Hali ya Uwekezaji
      • Business License Form
  • Kituo cha Habari
    • Video
    • Habari
    • Hotuba kwa Vyombo vya Habari
    • Maktaba ya Picha

MALIMBIKIZO YA WALINZI SOKONI, KULIPWA NA HALMASHAURI

Posted on: June 30th, 2019

Mkurugenzi mtendaji wa Halmashauri ya wilaya ya Karatu ndugu Waziri Mourice, amefanya mkutano na wafanyabiashara wa soko kuu la Karatu. Mkutano huo wa kawaida ulilenga kutoa taarifa za ujenzi wa soko pamoja na  kuzungumza changamoto zinazowakabili wafanyabiashara  ambao wamehama kupisha ujenzi wa soko unaoendelea.

Ndugu Waziri Mourice amewaahidi wafanyabiashara hao kufuatilia kwa karibu ujenzi wa soko hilo. Katika makubaliano ya awali soko lilitakiwa kumalizika kupauliwa tarehe 8 mwezi wa 7 mwaka huu. Mkurugenzi amesema mpaka kufika muda huo upauzi utakuwa bado haujamalizika lakini ameahidi kusimamia kidete swala la upauzi wa soko.  Mwaka mpya wa fedha unaoanza Halmashauri imetenga kiasi cha shilingi million 100 katika ujenzi wa soko. Ndugu Waziri amesema haridhishwi wafanyabishara hao kukaa nje ya soko kwa sababu hata halmashauri  inakosa mapato kutokana na ujenzi kutokamilika.

Ndugu Waziri Mourice ametumia nafasi hiyo kuwaomba wafanyabiashara ambao hawajachukua vitambulisho vya ujasiriamali kuchukua bila shuruti. Amesema hakuna mtu anayepaswa kutoa ushuru wa shilingi 300 tena na badala yake wachukue vitambulisho vya ujasiriamali. Ndugu Waziri Mourice ameahidi kuwalipa walinzi madai yao ya mshahara wa miezi mitatu. Walinzi hao mkataba wao wa kufanya kazi unaisha mwaka huu wa fedha, amesema walinzi hao wawili watalipwa madai yao na Halmashauri pamoja na mlinzi mwingine wa buchani ambaye naye anadai malimbikizo ya miezi saba ya mshahara. Katika kikao hicho wananchi walikubaliana kutafuta namna ya kutafuta walinzi wa kulinda vibanda vyao na kuwalipa kupitia viongozi wao.

Wafanyabishara wenyewe watapanga kiasi cha kuwalipa walinzi hao bila kuhusisha Halmashauri. Ndugu Waziri Mourice amewatoa hofu wafanyabishara amesema pindi soko litakapokamilika watarudi kwenye soko hilo kwa sabababu Halmashauri ina majina ya wafanyabishara waliokuwepo awali. Lakini pia hata viongozi wa wafanyabiashara wa soko hilo wanayo orodha ya majina ya wafanyabishara wenye uhalali wa kurudi kupata sehemu za biashara katika soko hilo. Ndugu waziri Mourice amesema katika ujenzi wa meza hizo za ndani watachukua maoni kutoka kwa wafanyabiashara ili sehemu za biashara zikae kwa namna iliyobora.

Awali katika mkutano huo wafanyabiashara kutoka soko la chini walimuelezea Mkurugenzi adhaa ya maji wanayopata. Bi, Flora  Mgaza amesema soko la chini liko katika mkondo wa maji hivyo mvua zinaponyesha, eneo linakuwa siyo rafiki kwao na kwa wateja kufanya biashara. Ameomba soko likamilike kabla ya masika nyingine haijafika ili waweze kuepuka adha wanayopata wakati wa masika. Pia amesema soko la chini lina magofu ambayo watu hawafanyi biashara jambo linaloleta ugumu hasa wakati ulinzi muda wa usiku. Mfanyabiashara huyo amesema zipo fununu watu kutaka kutumia mwanya wa magofu ya vibanda hivyo kuja kupata nafasi ya vibanda vyao pindi soko jipya litakapokamilika.

Matangazo

  • Matokeo ya upimaji wa Kitaifa kidoto cha pili January 07, 2024
  • Halmashauri ya Wilaya ya Karatu Uchaguzi wa Wanafunzi wa kidato cha kwanza, 2024 December 18, 2023
  • Matokeo ya Darasa la Nne January 07, 2024
  • NAFASI ZA KAZI 2024 April 21, 2024
  • Angalia Zote

Taarifa Mpya

  • MILIONI 400 ZATOLEWA KARATU, KUJENGA MABWENI NA MADARASA EYASI SEKONDARI

    January 30, 2025
  • WASIMAMIZI WAASWA KUSIMAMIA VIAPO VYAO KUELEKEA UCHAGUZI WA SERIKALI ZA MITAA 2024.

    November 23, 2024
  • JESHI LA AKIBA MKAWE WAZALENDO KWA TAIFA

    November 23, 2024
  • HALMASHAURI YAZINDUA KITABU CHA MPANGO MKAKATI WA UKUSANYAJI MAPATO.

    November 19, 2024
  • Angalia Zote

Video

DC KOLIMBA ATATUA KERO TARAFA YA EYASI KARATU
Video Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fursa za Uwekezaji

Viunganishi Linganifu

  • Tovuti ya Wizara ya Fedha na Mipango
  • Jamvi la Habari
  • Tovuti ya Tamisemi
  • Tovuti ya Serikali
  • Sekretarieti ya Ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Location Map

Wasiliana Nasi

    Karatu District Council

    Sanduku la Posta: P.O Box 190

    Simu: +255 272970648

    Simu ya Mkononi: 0754773947

    Barua Pepe: ded@karatudc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Haki Miliki @ 2017 Halmashauri ya Wilaya ya Karatu.Haki zote zimehifadhiwa