• Wasiliana Nasi |
    • Maswali |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Complains |
Karatu District Council
Karatu District Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Karatu

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Dhamira na Dira
    • Historia
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Fedha na Biashara
      • Ujenzi
      • Afya
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
    • Vitengo
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma Zetu
  • Madiwani
  • Miradi
    • TASAF
    • BOOST
  • Machapisho
    • Hali ya Uwekezaji
      • Business License Form
  • Kituo cha Habari
    • Video
    • Habari
    • Hotuba kwa Vyombo vya Habari
    • Maktaba ya Picha

MAMLAKA YA NGORONGORO YAONGEZA NGUVU UHIFADHI WA MAZINGIRA

Posted on: March 3rd, 2021

Na Tegemeo Kastus

Kuna baadhi ya maeneo ambayo wananchi wamejenga makazi ya kuishi  ambayo awali yalikuwa ni mapitio ya wanyama. Halmashauri kwa kunashirikiana na Mamlaka ya hifadhi ya bonde la Ngorongoro tunaendelea kuhakikisha tunawarudisha wanyamapori katika eneo la hifadhi.

Hayo yamesemwa na Mgeni rasmi Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Karatu Ndg. Waziri Mourice katika kilele cha siku ya wanyamapori kilichofanyika katika eneo linalojengwa Hospitali ya wilaya katika kijiji cha Changarawe. Ndg. Mourice ameomba mamlaka kuendelea kushirikiana na Halmashauri ili kuendelea kukabiliana na wanyama wanaoingia katika makazi ya watu. Kuwaondoa wanyama kwa wakati kunasaidia kutoleta madhara katika makazi ya watu lakini kunaondoa wanyamapori katika  hatari ya ujangili.

Kaimu Mhifadhi wa Mamlaka ya Ngorongoro Dkt. Christopher Timbuka akipanda mti katika eneo linalojengwa Hospitali ya wilaya ya Karatu.

Ndg. Mourice ameomba mamlaka ya bonde la Ngorongoro kuweka wenye mpango wa  bajaeti swala la matumizi bora ya ardhi katika kata zinazopakana na hifadhi. Amesema tukiwaelimisha wananchi, wakaingia katika mpango wa matumizi bora ya ardhi itasaidia kuondoa mivutano kati ya wananchi na mamlaka ya hifadhi ya Ngorongoro. Amesema tukiwatunza hawa wanyama vizuri inasaidia shughuli za utalii kuongezeka na tunazidi kupata fedha za utalii.

Ndg. Waziri Mourice ameshukuru kwa fedha takribani million 800 zilizotolewa na mamlaka ya hifadhi ya bonde la ngorongo katika kusaidia miradi mbalimbali ya maendeleo. Amesema kati ya fedha hizo mamlaka imetoa kiasi cha million 600 kwa kujenga majengo matatu ya hospitali ya wilaya ambayo yako katika hatua mabalimbali za ujenzi, jengo la wagonjwa wa nje, jengo la utawala  na jengo la Maabara.

Ndg. Mourice amesema mamlaka imetoa miche ya miti zaidi ya 14000  katika Halmashauri ya Karatu bure katika miche hiyo miche 3000 imetolewa kwa ajili ya kupanda eneo linalojengwa Hospitali ya wilaya ya Karatu. Zoezi la upandaji wa miti limefanyika likiongozwa na kauli mbiu ya misitu na maisha endelevu ya watu na maliasili.

Makamu Mwenyekiti wa Halamshauri ya Karatu Mh. John Bayo akipanda mti katika eneo linalojengwa hospitali ya wilaya.

Ndg. Mourice amesema kupanda miti kunasaidia kuendeleza jitihada za kutunza mazingira  kwenye eneo linalojengwa hospitali ya wilaya. katika kuendeleza ujirani mwema Mamlaka ya bonde la Ngorongoro inatoa mikopo kupitia Geopark. Mambo haya yasingewezekana kama tusingekuwa tumepakana  na mamlaka ya bonde la ngorongo katika Halmashauri ya wilaya ya Karatu.

Naye Makamu Mwenyekiti wa Halmashauri Mh. John Bayo ameomba Mamlaka ya hifadhi ya bonde la Ngorongoro kuwapa mafunzo vijana 50 ili wasaidie kufukuza wanyama pori wanaojitokeza sana katika Maeneo la kambi ya nyoka, Tloma  maeneo ya Kata oldean Kata Daa kata ya Rhotia. Amesema wanyama wanaoingia kwenye makazi ya watu husababisha wanafunzi wa maeneo hayo kuwa na maendeleo mabaya kitaaluma. Hali inayosababishwa na kukosa kuhudhuria shule mara kwa mara kutokana na muingiliano wa wanyama katika maeneo ya makazi ya watu.

Akizungumza juu ya zoezi la upandaji wa miti kaimu mhifadhi wa Mamlaka ya hifadhi ya  Bonde la  Ngorongo Dkt. Christopher Timbuka amesema faida za kupanda miti zimesaidia sana kupunguza utegemezi wa  bidhaa za misitu. Amesema kesi za wananchi kuingia ndani ya hifadhi zimepungua akitolea mfano kata ya Mbulumbulu amesema wananchi wamepanda miti inayosaidia kuwapatia mbao na kuni.

Dkt. Timbuka amesema Mamlaka ya Hifadhi ya bonde la Ngorongoro katika jitihada za kuzuia athari zinazoweza kuletwa mabadiliko ya tabia ya nchi, Mamlaka imejikita katika kuongezea uwezo msitu wa kufyoza na kuhifadhi hewa ya ukaa kwa kurudishia msitu uoto wa asili ulioathirika kutokana na shughuli mbalimbali za kibinadamu zisizorafiki kwa mazingira.

Ameongeza kusema  Mamlaka ya hifadhi ya Ngorongoro imeweza  kuzuia uchomaji ovyo wa misitu kuzuia uchomaji wa mikaa, kuzuia mifugo wasio ruhusiwa ndani ya hifadhi, na  kuzuia ukataji ovyo wa misitu kama ilivyokuwa kipindi cha nyuma na kujikita katika kulinda vyanzo vya maji.


Wananchi wa vijiji vya Changarawe na Dofa wakishiriki kupanda miti kwenye eneo linalojengwa hospitali ya wilaya.

Matangazo

  • Matokeo ya upimaji wa Kitaifa kidoto cha pili January 07, 2024
  • Halmashauri ya Wilaya ya Karatu Uchaguzi wa Wanafunzi wa kidato cha kwanza, 2024 December 18, 2023
  • Matokeo ya Darasa la Nne January 07, 2024
  • NAFASI ZA KAZI 2024 April 21, 2024
  • Angalia Zote

Taarifa Mpya

  • MILIONI 400 ZATOLEWA KARATU, KUJENGA MABWENI NA MADARASA EYASI SEKONDARI

    January 30, 2025
  • WASIMAMIZI WAASWA KUSIMAMIA VIAPO VYAO KUELEKEA UCHAGUZI WA SERIKALI ZA MITAA 2024.

    November 23, 2024
  • JESHI LA AKIBA MKAWE WAZALENDO KWA TAIFA

    November 23, 2024
  • HALMASHAURI YAZINDUA KITABU CHA MPANGO MKAKATI WA UKUSANYAJI MAPATO.

    November 19, 2024
  • Angalia Zote

Video

DC KOLIMBA ATATUA KERO TARAFA YA EYASI KARATU
Video Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fursa za Uwekezaji

Viunganishi Linganifu

  • Tovuti ya Wizara ya Fedha na Mipango
  • Jamvi la Habari
  • Tovuti ya Tamisemi
  • Tovuti ya Serikali
  • Sekretarieti ya Ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Location Map

Wasiliana Nasi

    Karatu District Council

    Sanduku la Posta: P.O Box 190

    Simu: +255 272970648

    Simu ya Mkononi: 0754773947

    Barua Pepe: ded@karatudc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Haki Miliki @ 2017 Halmashauri ya Wilaya ya Karatu.Haki zote zimehifadhiwa