• Wasiliana Nasi |
    • Maswali |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Complains |
Karatu District Council
Karatu District Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Karatu

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Dhamira na Dira
    • Historia
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Fedha na Biashara
      • Ujenzi
      • Afya
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
    • Vitengo
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma Zetu
  • Madiwani
  • Miradi
    • TASAF
    • BOOST
  • Machapisho
    • Hali ya Uwekezaji
      • Business License Form
  • Kituo cha Habari
    • Video
    • Habari
    • Hotuba kwa Vyombo vya Habari
    • Maktaba ya Picha

MANG’OLA TUACHE KUCHOMA MOTO VYANZO VYA MAJI

Posted on: May 26th, 2019

Mkuu wa wilaya ya karatu Mhe. Theresia Mahongo amewakataza wananchi wa Tarafa ya Eyasi kuchoma moto katika chanzo cha maji Qangdend. amesema chanzo hicho kikiharibika wananchi wa mang’ola hawataendelea tena na shughuli za kilimo. Tangu juzi kuna moto unawaka katika chanzo hicho cha maji.

Mhe. Theresia amesema hayo katika sherehe za waguzi zilizofanyika katika kituo cha afya Mbuga Nyekundu. Wanaofanya hivyo ni sawa na kuwachoma sindano ya sumu, amesema yale matete na miti yanazuia jua kufyonza maji moja kwa moja. Ameomba watu wanaowafahamu watu wanaochoma moto watoe taarifa ili hatua kali za kisheria ziweze kuchukuliwa dhidi yao. Kanda hii ya umwagiliaji kuna vijiji saba tunategemea chanzo kile cha maji ambacho kitakauka, serikali inapigania kuongeza maji kwa kuchimba visima ili maji yajitosheleze kwa kilimo cha umwagiliajia Mang’ola.

Mhe. Theresia amemuelekeza Katibu Tarafa kukaa na wenyeviti wa kijiji kutafuta ufumbuzi kwanini chanzo kile hakitunzwi. Mhe.Theresia amewataka pia JUWAMABOYE kuchagua uongozi mpya baada ya uongozi wa sasa kumaliza kipindi chake. Amesema kwa sasa kuchagua uongozi kwa ngazi ya kijiji umekamilika hivyo amewataka kumalizia kuchagua uongozi huo ili ukamilike ndani ya mwezi wa sita. Mhe. Theresia amesema amesikitishwa sana baada ya kusikia kwamba zinahitajika million kumi, Mhe. Theresia amesema sisi ni watumishi wa umma amehoji kiasi hicho cha fedha ni kwa ajili ya matumizi gani ? Mh. Theresia amesema kazi hiyo ni lazima ifanyike.

Mhe. Theresia amesema ni marufuku kwa wafanyabishara kufunga rumbesa, amesema kufanya hivyo ni kuwanyonya wakulima. amewataka wakulima kukataa kufunga rumbesa, amesema wakulima wanalima kwa gharama kubwa halafu wanapata faida kidogo. Wakulima wanachangia kwa kiasi kikubwa uchumi wa Karatu. Mhe. Theresia amemuagiza Katibu tarafa kuwakamata watu wanaojaza rumbesa, na amesema kutakuwa na kizuizi cha kukagua katika geti la manyara na kuweka kizuizi pia barabara ya Mbulumbulu. Mhe Mahongo amesema kuliko kujaza rumbesa bora waende wakahifadhi mazao kwenye ghala, ili kusubiri bei imarike. Amesema serikali inapigana kutafuta masoko ya mazao, na wameshazungumza na Rais wa IFAD juu kupata soko zuri la vitunguu na wakati alipofanya ziara wilayani Karatu.

Matangazo

  • Matokeo ya upimaji wa Kitaifa kidoto cha pili January 07, 2024
  • Halmashauri ya Wilaya ya Karatu Uchaguzi wa Wanafunzi wa kidato cha kwanza, 2024 December 18, 2023
  • Matokeo ya Darasa la Nne January 07, 2024
  • KIKAO CHA BARAZA LA MADIWANI 2024 May 11, 2024
  • Angalia Zote

Taarifa Mpya

  • MAAFISA UANDIKISHAJI WALA KIAPO KARATU

    May 14, 2025
  • DED HOKORORO ASHIRIKI KIKAO CHA ALAT WILAYA YA MERU

    May 15, 2025
  • MADAKTARI BINGWA WA SAMIA AWAMU YA TATU WATUA KARAU

    May 12, 2025
  • KARATU WASAPOTIJUHUDI ZA RAIS SAMIA WATANGAZA UTALII WA NDANI

    May 11, 2025
  • Angalia Zote

Video

DC KOLIMBA ATATUA KERO TARAFA YA EYASI KARATU
Video Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fursa za Uwekezaji

Viunganishi Linganifu

  • Tovuti ya Wizara ya Fedha na Mipango
  • Jamvi la Habari
  • Tovuti ya Tamisemi
  • Tovuti ya Serikali
  • Sekretarieti ya Ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Location Map

Wasiliana Nasi

    Karatu District Council

    Sanduku la Posta: P.O Box 190

    Simu: +255 272970648

    Simu ya Mkononi: 0754773947

    Barua Pepe: ded@karatudc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Haki Miliki @ 2017 Halmashauri ya Wilaya ya Karatu.Haki zote zimehifadhiwa