• Wasiliana Nasi |
    • Maswali |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Complains |
Karatu District Council
Karatu District Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Karatu

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Dhamira na Dira
    • Historia
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Fedha na Biashara
      • Ujenzi
      • Afya
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
    • Vitengo
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma Zetu
  • Madiwani
  • Miradi
    • TASAF
    • BOOST
  • Machapisho
    • Hali ya Uwekezaji
      • Business License Form
  • Kituo cha Habari
    • Video
    • Habari
    • Hotuba kwa Vyombo vya Habari
    • Maktaba ya Picha

MARERA, WANANCHI WAMKALIA KOONI MWENYEKITI WA KIJIJI

Posted on: March 11th, 2021

Na Tegemeo Kastus

Serikali inafanya utaratibu wa kurasimisha maeneo kwa wananchi ili waweze kupata uwezo kutumia hati zao za kumiliki ardhi kupata mikopo. Watu wanaongezeka lakini eneo la ardhi linabaki kuwa lile lile hivyo ni vyema kuhifadhi na kuendeleza maeneo yetu badala ya kukimbilia kuyauza.Kadhia ya migogoro mingi ya ardhi kwa wananchi inachochewa na kukosekana uwazi kwa uongozi wa Halmashauri ya kijiji cha Marera katika uuzaji wa maeneo ya kijiji.

Hayo yamesemwa na Mkuu wa wilaya ya Karatu Mh. Abbas Kayanda alipokuwa akitatua kero za wananchi katika kata ya Rhotia na baadae kufanya mkutano wa hadhara aliozungumza na wananchi. Ameelekeza  taasisi ya kuzuia na kupambana  na rusha (Takukuru) kufanya uchunguzi kwa uongozi wa Halmashauri ya kijiji cha Marera. Baada ya malalamiko  mengi   kuelekezwa kwa Mwenyekiti wa kijiji cha Marera na mabalozi wanaotuhumiwa kufanya udalali wa kuuza viwanja kwa njia za udanganyifu jambo linaloibua migogoro mingi ya ardhi katika kijiji cha Marera.

Mwanachi akiwa amesimama na bango wakati wa mkutano wa hadhara uliofanyika kijiji cha Rhotia Kati

Mh. Kayanda amesema asilimia 99 ya malalamiko ya wananchi ni mgogoro ya ardhi, amessema changamoto za migogoro ya ardhi zisipotatuliwa haraka zitasababisha uvunjifu wa amani. Amesema kila kiongozi Marera atakayebainika baada ya uchunguzi kufanyika kula fedha za wananchi au kujinufaisha atazirejesha fedha hizo. Amesema Takukuru watachunguza taarifa za mapato na matumizi za kijiji cha Marera pamoja na kiasi cha shilingi million tano ambazo zimekosa mchanganuo na vielelezo vyote vya malalamiko hayo vilivyotolewa na wananchi vimewasilishwa  Takukuru tayari kwa kufanyiwa uchunguzi.

Akizungumzia malalamiko ya mabango yaliooneshwa na wanachi kuonesha kutokuwa  na imani na Mwenyekiti wa kijiji cha Marera. Mh. Kayanda amesema wananchi wanapaswa kuandika orodha ya majina pamoja na saini zao zitakazoonesha nia ya kutokuwa na imani na  Mwenyekiti kisha mkutano Mkuu wa Halmashauri ya kijiji utaitishwa. Amesema utaratibu kumuondoa madarakani lazima ufuatwe kama ulivyofutwa wakati wa kumuweka madarakani.

Mh.Kayanda amewaasa viongozi wa serikali waliopewa dhamana ya kuwatumikia wananchi ni vyema wakakubali kutoa ufafanuzi wa kina juu ya mambo wanayoulizwa na wananchi. Amesema huwezi kuwa kiongozi; wananchi wasikuhoji, uongozi ni pamoja na kutoa taarifa zinazowahusu wananchi kwa kina na kwa wakati,  ili kuonesha dhana ya utawala bora. Viongozi wapo kwa niaba ya wananchi, katika kuongoza huwezi kukwepa maswali kutoka kwa wananchi.

Mh. Abbas Kayanda (kulia) Katika ofisi ya kijiji cha Rhotia akitatua kero za wananchi

Akizungumzia kuhusu swala gharama za maji kuwa juu katika kata ya Rhotia Mh. Abbas Kayanda amesema ametoa maelekezo kwa Mwenyekiti wa bodi ya maji Rhotia kupanga bei upya ya maji ili kutimiza dhana ya serikali ya kumtua mama ndoo kichwani. Amesema bei elekezi iliyowekwaa na serikali ni shilingi 1700 kwa unit moja ya maji. Amesema haipendezi wananchi kulalamika bei ya juu ya maji, ameongeza kusema Ruwasa katika bajeti ya maji ya mwaka ujao wa fedha 2021-2022 imepanga kurekebisha miundo mbinu ya maji Rhotia.  Hivyo ukarabati huo utasaidia kuondoa miundo mbinu chakavu na kuimarisha upatikanaji wa maji kwa wananchi. Amesema  lazima sasa bodi ifikirie namna ya kuongeza usambazaji wa maji kwa watu badala na kuweka bei ya juu katika kila unity moja ya maji inayotumiwa.

Wananchi wakizungumzia kuhusu kero ya maji ndg. Ramadhani Iddi amesema walikuwa wanalipa kiasi cha shilingi 2000 kwa unit moja ya maji ili kuwezesha maji kupatikana muda wote lakini matokeo yake uhaba wa maji ndio umeongezeka. Amesema swala la bei ya maji limekuwa likipigwa danadana jambo ambalo limekuwa likitoa picha mbaya kwa wananchi.

Matangazo

  • Matokeo ya upimaji wa Kitaifa kidoto cha pili January 07, 2024
  • Halmashauri ya Wilaya ya Karatu Uchaguzi wa Wanafunzi wa kidato cha kwanza, 2024 December 18, 2023
  • Matokeo ya Darasa la Nne January 07, 2024
  • KIKAO CHA BARAZA LA MADIWANI 2024 May 11, 2024
  • Angalia Zote

Taarifa Mpya

  • MAAFISA UANDIKISHAJI WALA KIAPO KARATU

    May 14, 2025
  • DED HOKORORO ASHIRIKI KIKAO CHA ALAT WILAYA YA MERU

    May 15, 2025
  • MADAKTARI BINGWA WA SAMIA AWAMU YA TATU WATUA KARAU

    May 12, 2025
  • KARATU WASAPOTIJUHUDI ZA RAIS SAMIA WATANGAZA UTALII WA NDANI

    May 11, 2025
  • Angalia Zote

Video

DC KOLIMBA ATATUA KERO TARAFA YA EYASI KARATU
Video Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fursa za Uwekezaji

Viunganishi Linganifu

  • Tovuti ya Wizara ya Fedha na Mipango
  • Jamvi la Habari
  • Tovuti ya Tamisemi
  • Tovuti ya Serikali
  • Sekretarieti ya Ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Location Map

Wasiliana Nasi

    Karatu District Council

    Sanduku la Posta: P.O Box 190

    Simu: +255 272970648

    Simu ya Mkononi: 0754773947

    Barua Pepe: ded@karatudc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Haki Miliki @ 2017 Halmashauri ya Wilaya ya Karatu.Haki zote zimehifadhiwa