• Wasiliana Nasi |
    • Maswali |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Complains |
Karatu District Council
Karatu District Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Karatu

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Dhamira na Dira
    • Historia
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Fedha na Biashara
      • Ujenzi
      • Afya
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
    • Vitengo
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma Zetu
  • Madiwani
  • Miradi
    • TASAF
    • BOOST
  • Machapisho
    • Hali ya Uwekezaji
      • Business License Form
  • Kituo cha Habari
    • Video
    • Habari
    • Hotuba kwa Vyombo vya Habari
    • Maktaba ya Picha

MAUDHUI YA KIPINDI YANATEGEMEA ANDALIO BORA LA SOMO

Posted on: July 12th, 2019

Afisa elimu sekondari ameendelea na ukaguzi wa shule za sekondari upande wa tarafa ya Endabash. Katika ziara hiyo amezungumza na kuwaasa walimu juu ya mbinu za ufundishaji, na ufuatiliaji wa wanafunzi ili kupata matokeo chanya. Shule tatu zilizotembelewa  ni Marang, Orboshan na Kansay.

Bi,Kalista Maina amesema kuwa na andalio la kazi ni muhimu kwa sababu ndio dira inayokuongoza katika ufundishaji. Amesema ni rahisi sana kutoka nje ya malengo uliojiwekea kufundisha somo kama huna andalio la somo. Bi Maina amesema hayo baada ya kukuta walimu hawana maandalio ya masomo na wengine kuandika maandalio hayo kwa kuruka ruka bila kufuata utaratibu. Amesema hapo ndipo makosa ya ufundishaji yanapoanza na matokeo yake wanafunzi wanafeli katika mitihani.

Ameipongeza shule ya Marang kwa kushika nafasi ya 12 kati ya shule 32 za Wilaya  na kwa ngazi ya mkoa imekuwa shule ya 204 kati ya 226. Shule ya Orboshani imekuwa shule ya 8 kati ya 32 ngazi ya  za wilaya na ngazi ya mkoa imekuwa shule 84 kati ya shule 226. Shule ya kansay imekuwa ya 22 kwa ngazi ya wilaya kati ya shule 32 na kwa  ngazi ya mkoa imekuwa 187 kati ya shule 226. Lakini pia amemuelekeza Mkuu wa shule Marang kwenda na mwalimu wa baiolojia kwenda kutoa maelezo kwa mwajiri baada ya kupata “F” masomo yote kwenye mtihani wa Moko. Amesema walimu wa Historia na Geografia wataandika maelekezo kujieleza sababu ya watoto kufanya vibaya masomo yao katika mtihani wa Moko kidato cha nne.

Bi, Maina amebaini walimu wanaofanya kazi kwa muda mrefu bila kupata nafasi ya kuchaguliwa kusimamia mitihani. Amesema lazima kuwe na uwiano sawa wa kuchagua walimu wa kwenda kusimamia mitihani ya taifa. Bi. Maina amekutana na walimu ambao wamekaa miaka zaidi ya saba bila kusimamia mwaka hata mmoja mitihani ya taifa.

Afisa elimu sekondari akiwa anafanya ukaguzi wa vifaa vya kiutendaji vya mwalimu.

Afisa elimu taaluma ndugu Robert Sijaona amesema ualimu ni dhamana ni vyema walimu wakaitambua dhamana waliopewa. Mada za masomo zipo kwa mpangilio maalumu ni lazima  mwalimu afuate utaratibu wa kufundisha. Walimu tuwaelekeze wanafunzi utaratibu mzuri wa kuhifadhi notsi za masomo kidato cha kwanza mpaka kidato cha nne. Hiyo itamsaidia na kumrahisishia mwanafunzi wakati wa kusoma na kujikumbusha. Amesema ni vyema walimu wakakaa vikao siku ya ijumaa ili kujitathimini shughuli za kitaaluma. Hiyo itasaidia katika uwajibikaji ili kupunguza dosari za ufundishaji.

Naye afisa takwimu Sekondari Bi, Brenda Mlay amesema ni vyema walimu  tukubali kuwajibika, kumekuwa na tabia ya walimu kujitokea tu kwenye vituo vya kazi. Ametoa maelekezo kila shule kuwa na daftari  linaonesha taarifa za kutoka kwa mwalimu. Agizo hilo ni kwa walimu wote ili kuzuia ruhusa na kujiondokea kiholela kwa walimu katika vituo vya kazi. Ziara hiyo imebaini baadhi ya walimu kutokuwepo kwenye vituo vya kazi na hakuna fomu walizojaza kuomba ruhusa shuleni na  wilayani.


Afisa akiwa na mwalimu  akiangalia na kukagua mafaili mbalimbali

Matangazo

  • Matokeo ya upimaji wa Kitaifa kidoto cha pili January 07, 2024
  • Halmashauri ya Wilaya ya Karatu Uchaguzi wa Wanafunzi wa kidato cha kwanza, 2024 December 18, 2023
  • Matokeo ya Darasa la Nne January 07, 2024
  • NAFASI ZA KAZI 2024 April 21, 2024
  • Angalia Zote

Taarifa Mpya

  • MILIONI 400 ZATOLEWA KARATU, KUJENGA MABWENI NA MADARASA EYASI SEKONDARI

    January 30, 2025
  • WASIMAMIZI WAASWA KUSIMAMIA VIAPO VYAO KUELEKEA UCHAGUZI WA SERIKALI ZA MITAA 2024.

    November 23, 2024
  • JESHI LA AKIBA MKAWE WAZALENDO KWA TAIFA

    November 23, 2024
  • HALMASHAURI YAZINDUA KITABU CHA MPANGO MKAKATI WA UKUSANYAJI MAPATO.

    November 19, 2024
  • Angalia Zote

Video

DC KOLIMBA ATATUA KERO TARAFA YA EYASI KARATU
Video Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fursa za Uwekezaji

Viunganishi Linganifu

  • Tovuti ya Wizara ya Fedha na Mipango
  • Jamvi la Habari
  • Tovuti ya Tamisemi
  • Tovuti ya Serikali
  • Sekretarieti ya Ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Location Map

Wasiliana Nasi

    Karatu District Council

    Sanduku la Posta: P.O Box 190

    Simu: +255 272970648

    Simu ya Mkononi: 0754773947

    Barua Pepe: ded@karatudc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Haki Miliki @ 2017 Halmashauri ya Wilaya ya Karatu.Haki zote zimehifadhiwa