• Wasiliana Nasi |
    • Maswali |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Complains |
Karatu District Council
Karatu District Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Karatu

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Dhamira na Dira
    • Historia
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Fedha na Biashara
      • Ujenzi
      • Afya
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
    • Vitengo
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma Zetu
  • Madiwani
  • Miradi
    • TASAF
    • BOOST
  • Machapisho
    • Hali ya Uwekezaji
      • Business License Form
  • Kituo cha Habari
    • Video
    • Habari
    • Hotuba kwa Vyombo vya Habari
    • Maktaba ya Picha

MHE, THERESIA AFANYA ZIARA KATIKA VITUO VYA AFYA

Posted on: July 1st, 2019

Mkuu wa wilaya ya Karatu Mhe. Theresia Mahongo amefanya ziara katika kata ya Kansay na kutembelea zahanati ya Ng’aibara na Zahanati ya Laja. Amekagua miundo mbinu ya zahanati hizo, pamoja na kuangalia, hali ya upatikanaji wa dawa katika zahanati hizo. zahanati ya Ng'aibara inatarajiwa kufanyiwa ukarabati wa majengo katika kipindi cha mwaka huu wa fedha unaonza sasa.

Mhe. Theresia amemuomba mwenyekiti wa kijiji cha Ng'aibara kutumia vizuri fedha walizopewa na Global fund ili zinufaishe wananchi waliolengwa. Amesema zahanati hiyo ikiboreshwa wagonjwa watakuwa wakipata rufaa  wanakwenda hospitali ya wilaya. Amewapongeza wananchi kwa kujenga jengo lenye ubora ambalo bado halijamalizika kupauliwa. Mhe. Theresia amesema  mfumo wa kuomba dawa umebadilika kila kituo kinaandika mahitaji ya dawa inazohitaji kwenye kituo hivyo ni vyema kituo kikaagiza dawa kulingana na Mahitaji ya kituo. Amesema bajeti ya afya ilikuwa billion 36 kipindi cha nyuma lakini sasa hivi bajeti ya afya  imeongezeka na imefikia takribani billion 270 kwa mwaka. Kituo hicho awali  kilipata nyota sifuri kwa kuwa na huduma duni. Lakini sasa mabadiliko makubwa yamefanyika katika zahanati ya Ng’aibara ikiwa ni pamoja na kuweka daktari mmoja na muuguzi.


Mkuu wa wilaya akikagua jengo la watumishi zahanati ya Ng'aibara

Mganga mkuu wa wilaya Mustafa Waziri amesema kituo hicho cha Ng’aibara kimepewa kiasi cha 154,208,000. Fedha hizo 25 %  zitatumika kulipa mafundi na iliyobakia ni kwa kujenga miundo mbinu na kukarabati zahanati hiyo. Shughuli hizo za ukarabati wa kituo cha afya zinahusisha; ujenzi wa vyoo, nyumba ya mtumishi, kuweka uzio wa wavu, na ujenzi wa maabara. Lakini pia kuweka umeme katika kituo hicho na kujenga na kuweka miundo mbinu ya maji.

Dkt. Mustafa amesema changamoto ya zahanati hiyo ni watu kutopenda kuhudhuria na kupata huduma za afya katika kituo vya afya. Ametoa rai kwa wakinamama wajawazito kwenda kujifungulia katika vituo vya afya. Karatu ina  47% ya wakinamama wanaojifungulia katika vituo vya afya kati ya 60% inayotakiwa na serikali. Ameomba pia  wajumbe wa kituo hicho kuhamasisha watu kupata bima ya afya iliyoboreshwa ambayo ni shilingi 30000 watu sita kwa kaya. Ambayo na serikali nayo inatoa fedha kiasi cha 30000 kwa kila aiyechangia mfuko wa bima ya afya. Dkt. Mustafa amesema bima ya afya inasaidia hospitali kuongeza uwezo wa kupata dawa kadri ya mahitaji ya kituo husika.

Matangazo

  • Matokeo ya upimaji wa Kitaifa kidoto cha pili January 07, 2024
  • Halmashauri ya Wilaya ya Karatu Uchaguzi wa Wanafunzi wa kidato cha kwanza, 2024 December 18, 2023
  • Matokeo ya Darasa la Nne January 07, 2024
  • NAFASI ZA KAZI 2024 April 21, 2024
  • Angalia Zote

Taarifa Mpya

  • MILIONI 400 ZATOLEWA KARATU, KUJENGA MABWENI NA MADARASA EYASI SEKONDARI

    January 30, 2025
  • WASIMAMIZI WAASWA KUSIMAMIA VIAPO VYAO KUELEKEA UCHAGUZI WA SERIKALI ZA MITAA 2024.

    November 23, 2024
  • JESHI LA AKIBA MKAWE WAZALENDO KWA TAIFA

    November 23, 2024
  • HALMASHAURI YAZINDUA KITABU CHA MPANGO MKAKATI WA UKUSANYAJI MAPATO.

    November 19, 2024
  • Angalia Zote

Video

DC KOLIMBA ATATUA KERO TARAFA YA EYASI KARATU
Video Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fursa za Uwekezaji

Viunganishi Linganifu

  • Tovuti ya Wizara ya Fedha na Mipango
  • Jamvi la Habari
  • Tovuti ya Tamisemi
  • Tovuti ya Serikali
  • Sekretarieti ya Ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Location Map

Wasiliana Nasi

    Karatu District Council

    Sanduku la Posta: P.O Box 190

    Simu: +255 272970648

    Simu ya Mkononi: 0754773947

    Barua Pepe: ded@karatudc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Haki Miliki @ 2017 Halmashauri ya Wilaya ya Karatu.Haki zote zimehifadhiwa