• Wasiliana Nasi |
    • Maswali |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Complains |
Karatu District Council
Karatu District Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Karatu

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Dhamira na Dira
    • Historia
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Fedha na Biashara
      • Ujenzi
      • Afya
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
    • Vitengo
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma Zetu
  • Madiwani
  • Miradi
    • TASAF
    • BOOST
  • Machapisho
    • Hali ya Uwekezaji
      • Business License Form
  • Kituo cha Habari
    • Video
    • Habari
    • Hotuba kwa Vyombo vya Habari
    • Maktaba ya Picha

MHE.GAMBO ATEMBELEA MACHIMBO YA MADINI MURUS

Posted on: August 29th, 2019

Mkuu wa mkoa wa arusha Mhe. Mrisho Gambo ameendelea na ziara yake ya kikazi wilayani Karatu. Mkuu wa mkoa ametembelea na kukagua eneo la madini ya dhahabu katika kijiji cha Endagem lilopo katika kitongoji cha Murus tarafa ya Endabash. Pamoja na kutembelea soko la madini liliopo kata ya Endabash ambalo uuzaji wa madini unafanyika siku ya alhamisi.

Mhe. Gambo amejionea shughuli za madini namna zinavyofanyika katika eneo hilo na akazungumza na wachimbaji wadogo wadogo wa dhahabu. Mhe. Mrisho Gambo amesema eneo hilo licha ya kuwa na watu waliokata leseni zaidi 500 lakini kwa ukubwa wa shughuli za uchimbaji wa madini haioneshi kama kuna idadi hiyo ya watu. Mkuu wa mkoa amesema hata mazingira ya uchimbaji siyo rafiki sana, amesema bado uchimbaji unafanyika kwa njia ambazo siyo za kisasa. Mhe. ametoa maelekezo eneo hilo kutengenezwa eneo la maliwato, lakini pia ametoa maelekezo kwa meneja wa Tanesco kufanya upembuzi yakinifu kuona namna ya kuleta umeme katika eneo hilo. Jambo litakalosaidia shughuli za uchimbaji wa madini, hasa katika mitambo inayotumia nishati ya umeme katika uchambuaji madini. (uchenjuaji wa madini)

Mhe. Theresia Mahongo Mkuu wa wilaya ya karatu amesema barabara ya kuelekea kijiji cha Endagem itaendelea kuboreshwa ili iweze kuwa nzuri na kupitika kwa urahisi. Amesema ukarabati tayari umeshaanza hasa katika maeneo korofi ya barabara. Barabara hiyo inahitaji fedha nyingi hasa kutokana na kuwepo kwa makorongo makubwa. Mhe. Mahongo amesema wakati wa mvua kwenye migodi huwa kunatokea majanga mengi, amewaomba wachimbaji   kutoa taarifa haraka pindi matatizo yanapojitokeza.

Mkuu wa Mkoa wa arusha akipata maelekezo kutoka kwa mchimbaji juu hatua za usafishaji mpaka kupata madini.

Naye Muwakilishi wa afisa madini Mkazi ndugu Gabriel Senge amesema kuna maeneo takribani matano ya uchimbaji wa madini. Tangu mwaka 2002 kulikuwa na uchimbaji mkubwa wa shughuli za madini Endagem. Hivyo kuvutia wachimbaji wengi kuja na kujishughulisha na kazi za uchimbaji wa madini. Hiyo ilivutia watu wengi kukata leseni lakini katikati kukatokea mdororo wa shughuli za uchimbaji na mashimo ya migodi kuanguka. Ndugu Gabriel amesema hata bei ya dhahabu ilishuka na kuchangia pia shughuli za uchimbaji kupungua.

 Ndugu Gabriel amesema kwa sasa bei ya madini ya dhahabu imeimarika na hata kiasi kinachopatikana cha madini kinanufaisha wachimbaji wadogo. Amesema kuna hati 302 za madai ya leseni na asilimia kubwa ya hati hizo za madai zinatoka katika eneo la Endabash. Hati hizo nyingi zinaisha muda wake mwaka huu na kuna ambazo zimeshaisha muda wake tangu mwezi wa kwanza. Amesema wameandika ombi la kufuta leseni 100 kwenda kwa Mtendaji mkuu wa tume ya madini. Ombi lao likiridhiwa hati hizo zitafutwa,  muwakilishi wa afisa madini ameomba wananchi hasa wachimbaji wadogo kuomba leseni kupitia maafisa madini wakazi na wataalamu wengine walio katika wilaya ambao wanaweza kuwasaidia. Ndugu Gabriel amesema upo mfumo wa njia za mtandao (online) kwa kutumia GPS unaoweza kuonesha kama eneo  limekatiwa leseni au halina leseni.

Mwenyekiti wa wachimbaji ndugu Afred Mwaswenya amesema kitaalamu kutoka shimo moja hadi jingine kunatakiwa kuachwe mita 10. Amesema zamani watu walikuwa hawafuati utaratibu huo ndio maana 2002 mashimo mengi yalianguka katika eneo hilo. Amesema  kuna miamba  0.1, 0.2. 0.3 ya madini ya dhahabu yanayopatikana Endagem. Ndugu Mwaswenya amesema kwa sasa wanaweza kupata gramu100 mpaka 150 kwa mwezi. Ndugu afred ameshukuru kwa ujio wa mkuu wa mkoa kwenye machimbo ya Murus amesema kwenye machimbo hayo wanachangamoto ya upatikanaji wa maji. Amesema nyenzo wanazotumia kwenye uchimbaji si nzuri, amemuomba mkuu wa mkoa kupitia wizara ya madini kuwapa fedha hata kama ni kwa mkopo ili isaidie katika ununuzi wa vifaa vya kisasa vya uchimbaji wa madini.

Matangazo

  • Matokeo ya upimaji wa Kitaifa kidoto cha pili January 07, 2024
  • Halmashauri ya Wilaya ya Karatu Uchaguzi wa Wanafunzi wa kidato cha kwanza, 2024 December 18, 2023
  • Matokeo ya Darasa la Nne January 07, 2024
  • NAFASI ZA KAZI 2024 April 21, 2024
  • Angalia Zote

Taarifa Mpya

  • MILIONI 400 ZATOLEWA KARATU, KUJENGA MABWENI NA MADARASA EYASI SEKONDARI

    January 30, 2025
  • WASIMAMIZI WAASWA KUSIMAMIA VIAPO VYAO KUELEKEA UCHAGUZI WA SERIKALI ZA MITAA 2024.

    November 23, 2024
  • JESHI LA AKIBA MKAWE WAZALENDO KWA TAIFA

    November 23, 2024
  • HALMASHAURI YAZINDUA KITABU CHA MPANGO MKAKATI WA UKUSANYAJI MAPATO.

    November 19, 2024
  • Angalia Zote

Video

DC KOLIMBA ATATUA KERO TARAFA YA EYASI KARATU
Video Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fursa za Uwekezaji

Viunganishi Linganifu

  • Tovuti ya Wizara ya Fedha na Mipango
  • Jamvi la Habari
  • Tovuti ya Tamisemi
  • Tovuti ya Serikali
  • Sekretarieti ya Ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Location Map

Wasiliana Nasi

    Karatu District Council

    Sanduku la Posta: P.O Box 190

    Simu: +255 272970648

    Simu ya Mkononi: 0754773947

    Barua Pepe: ded@karatudc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Haki Miliki @ 2017 Halmashauri ya Wilaya ya Karatu.Haki zote zimehifadhiwa