• Wasiliana Nasi |
    • Maswali |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Complains |
Karatu District Council
Karatu District Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Karatu

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Dhamira na Dira
    • Historia
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Fedha na Biashara
      • Ujenzi
      • Afya
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
    • Vitengo
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma Zetu
  • Madiwani
  • Miradi
    • TASAF
    • BOOST
  • Machapisho
    • Hali ya Uwekezaji
      • Business License Form
  • Kituo cha Habari
    • Video
    • Habari
    • Hotuba kwa Vyombo vya Habari
    • Maktaba ya Picha

MHE:LAZARO BAJUTA AIBUKA KIDEDEA KWENYE UCHAGUZI WA MAKAMU MWENYEKITI

Posted on: September 19th, 2018

Mwenyekiti wa Baraza la Madiwani, Mhe. Jubilate Gerson Mnyenye ameongoza kikao cha pili cha baraza la madiwani kilichofanyika leo katika ukumbi wa Halmashauri. Katika kikao hicho mihutasari ya vikao vya tarehe 27 na 28 april ilisoma na kuthibitishwa.

Kikao hicho kilimchagua Mhe.Lazaro Simoni Bajuta Diwani wa kata ya Ganako kuwa Makamu Mwenyekiti wa Halmashauri ambaye alipata kura 12 kati ya 19 na kura 7 alipata mpinzani wake Mhe. Lazaro Emanuel Gege Diwani wa Mang’ola. Pia wajumbe wa kamati ya Elimu Afya na Maji walimchagua Mhe. John Lucian Mahu, Diwani wa Endamarariek kuwa mwenyekiti wa kamati hiyo,wajumbe wa kamati  ya Uchumi, Ujenzi na Mazingira na ikamchagua Mhe. Josephat Martin Margwe  Diwani kata ya  Oldeani kuwa mwenyekiti wa kamti hiyo.

Katika kikao hicho taarifa ya Kamati ya Kudhibiti Ukimwi, kamati ya Elimu Afya na Maji, kamati ya Uchumi Ujenzi na Mazingirana kamati ya Fedha Uongozi  na Mipango zilipokelewa.

Mhe. John Lucian Mahu, mwenyekiti wa kamati Elimu ya Afya na Maji alisema kuna mpango wa kuziandikia barua ya kuzipongeza shule zilizofanya vizuri mitihani ya Taifa  na kuziandikia barua ya kujieleza kwa shule zilizofanya vibaya. Pamoja na hilo kamati yake inataka umeme ufike sehemu zote zenye vyanzo vya maji ili kupunguza gharama za maji. Mhe. John alisema kamati yake pia ina pambana na madada poa katika mji mdogo wa Karatu na imefanikiwa kukamata wakina dada 23 ambao kati yao 2 ni wanafunzi wa sekondari Welwel. Alisema tatizo linalosumbua zoezi hilo ni wazazi ambao hutetea watoto wao kwamba hawana tabia hizo.

Mhe Willy Qambaro Mbunge wa Karatu ambaye lichangia katika kamati hiyo aliomba Mkurgenzi Mtendaji kusambaza walimu wa kike katika shule za pembezoni iliwaweze kuwasaidia watoto wa kike katika shule hizo ambazo nyingi zina walimu wa kiume peke yake. Kamati hiyo  pia iliomba Wenyeviti wa vijiji, Watendaji wakishirikiana na Madiwani wawahimize wazazi watoe chakula ili wanafunzi wapate chakula wakiwa shuleni.

Matangazo

  • Matokeo ya upimaji wa Kitaifa kidoto cha pili January 07, 2024
  • Halmashauri ya Wilaya ya Karatu Uchaguzi wa Wanafunzi wa kidato cha kwanza, 2024 December 18, 2023
  • Matokeo ya Darasa la Nne January 07, 2024
  • KIKAO CHA BARAZA LA MADIWANI 2024 May 11, 2024
  • Angalia Zote

Taarifa Mpya

  • MAAFISA UANDIKISHAJI WALA KIAPO KARATU

    May 14, 2025
  • DED HOKORORO ASHIRIKI KIKAO CHA ALAT WILAYA YA MERU

    May 15, 2025
  • MADAKTARI BINGWA WA SAMIA AWAMU YA TATU WATUA KARAU

    May 12, 2025
  • KARATU WASAPOTIJUHUDI ZA RAIS SAMIA WATANGAZA UTALII WA NDANI

    May 11, 2025
  • Angalia Zote

Video

DC KOLIMBA ATATUA KERO TARAFA YA EYASI KARATU
Video Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fursa za Uwekezaji

Viunganishi Linganifu

  • Tovuti ya Wizara ya Fedha na Mipango
  • Jamvi la Habari
  • Tovuti ya Tamisemi
  • Tovuti ya Serikali
  • Sekretarieti ya Ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Location Map

Wasiliana Nasi

    Karatu District Council

    Sanduku la Posta: P.O Box 190

    Simu: +255 272970648

    Simu ya Mkononi: 0754773947

    Barua Pepe: ded@karatudc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Haki Miliki @ 2017 Halmashauri ya Wilaya ya Karatu.Haki zote zimehifadhiwa