• Wasiliana Nasi |
    • Maswali |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Complains |
Karatu District Council
Karatu District Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Karatu

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Dhamira na Dira
    • Historia
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Fedha na Biashara
      • Ujenzi
      • Afya
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
    • Vitengo
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma Zetu
  • Madiwani
  • Miradi
    • TASAF
    • BOOST
  • Machapisho
    • Hali ya Uwekezaji
      • Business License Form
  • Kituo cha Habari
    • Video
    • Habari
    • Hotuba kwa Vyombo vya Habari
    • Maktaba ya Picha

MIL 61 ZAZINDUA ZAHANATI YA MARERA

Posted on: October 13th, 2020

NA TEGEMEO KASTUS

Wananchi wa kijiji cha Marera wamepata tumaini jipya baada ya ujenzi wa zahanati  ya Marera ulioanza mwaka 2011 kukamilika. Zahanati hiyo inatarajia kutoa huduma za afya kwa kaya 462 zenye wakazi 2635, wazo la kujenga zahanati limetokana na umbali mrefu kutoka kijiji cha Marera mpaka kituo cha afya Karatu na gharama za juu za huduma afya katika kituo cha afya cha Rhotia kinachosimamiwa na kanisa katoliki.

Hayo yamesemwa Mkuu wa wilaya ya Karatu Mh. Abbas Kayanda wakati wa uzinduzi wa zahanati ya Marera. Ujenzi wa zahanati hiyo, wananchi wamechangia nguvu kazi million 14,775,700 Wadau wa maendeleo wamechangia Million 1 Halmashauri Million 45,876,000. Mh. Kayanda kipekee amempongeza  Afisa mtendaji wa kijiji pamoja na Mwenyekiti wa kijiji cha Marera kwa kazi nzuri ya kusimamia na kumalizia ujenzi wa zahanati ya Marera. Ujenzi huo wa zahanati umeenda sambamba na ujenzi wa nyumba ya watumishi, amesema zahanati ya Marera imepata watumishi watatu, afisa tabibu mmoja, mhudumu wa afya na nesi. Ameomba wananchi wa kijiji cha Marera kuwapa ushirikiano mzuri wafanyakazi hao wa afya walioletwa katika zahanati hiyo, katika utendaji  wa majukumu yao ya kazi.

Mkuu wa wilaya ya Karatu Mh. Abbas Kayanda akifungua zahanati ya Marera

Mh. Kayanda amesema ujenzi wa zahanati ya Marera, umeonesha wazi kwamba wananchi wakiamua wanaweza kuleta maendeleo wenyewe. Amesema lengo la serikali ni kuhakikisha kila kijiji kinakuwa na zahanati na kila kata inakuwa na kituo cha afya na kila wilaya inakuwa na hospitali ya wilaya. Zahanati ya Marera imesajiliwa na itaanza kupata mgao wa dawa kutoka Msd.

Mh. Kayanda amesema Rais wa awamu ya tano wa  Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mh. Dkt. John Pombe Magufuli ameweka vipaombele katika kuboresha sekta ya afya, kuboresha sekta elimu, kuboresha sekta ya maji na miundo mbinu. Amesema vituo vya afya vya serikali vinatoa matibabu kwa wazee wa zaidi ya miaka 60 bure, kwa mtoto wa chini ya miaka 5 na mama mjamzito bure. Lakini pia kwa wilaya ya Karatu serikali imetoa kiasi cha billion 1 kwa ajili ya ukamilishaji wa majengo ya hospitali ya wilaya ambayo ujenzi ulishaanza awali na ujenzi wa majengo mapya mengine manne.

Mkuu wa wilaya ya Karatu Mh. Abbas Kayanda akikagua kichomea taka katika zahanati ya Marera

Mh. Kayanda amesema serikali imekuja na mfumo wa bima ya afya iliyoboreshwa ambao ukitoa shilling 30,000 kwa watu sita  wa kaya moja wanapata huduma za afya kwa kipindi cha mwaka mzima. Ameomba wananchi kujiunga na mfuko huo, amesema kuumwa mtu hupangi ila kuumwa kuna kuja wakati wowote na unaweza kuumwa kipindi ambacho huna fedha. Amesema ni vyema wananchi kujiunga na mfuko wa bima ya afya iliyoboreshwa kwa sababu inasadia mwananchi kupata huduma wakati wowote.

Mh. Kayanda amesema kwa upande wa elimu serikali inatoa million 53 kila mwezi kwa uendeshaji wa shule ya msingi na million 73 zinatolewa kwa ajili ya uendeshaji wa shule za sekondari wilayani Karatu. Amesema jukumu la mzazi limebaki kununua sare za shule daftari la mtoto na kalamu, amesema hayo ndio mabadiliko yanayofanywa na serikali kwa wananchi.

Muonekano wa jengo la zahanati kwa nje

Matangazo

  • Matokeo ya upimaji wa Kitaifa kidoto cha pili January 07, 2024
  • Halmashauri ya Wilaya ya Karatu Uchaguzi wa Wanafunzi wa kidato cha kwanza, 2024 December 18, 2023
  • Matokeo ya Darasa la Nne January 07, 2024
  • KIKAO CHA BARAZA LA MADIWANI 2024 May 11, 2024
  • Angalia Zote

Taarifa Mpya

  • MAAFISA UANDIKISHAJI WALA KIAPO KARATU

    May 14, 2025
  • DED HOKORORO ASHIRIKI KIKAO CHA ALAT WILAYA YA MERU

    May 15, 2025
  • MADAKTARI BINGWA WA SAMIA AWAMU YA TATU WATUA KARAU

    May 12, 2025
  • KARATU WASAPOTIJUHUDI ZA RAIS SAMIA WATANGAZA UTALII WA NDANI

    May 11, 2025
  • Angalia Zote

Video

DC KOLIMBA ATATUA KERO TARAFA YA EYASI KARATU
Video Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fursa za Uwekezaji

Viunganishi Linganifu

  • Tovuti ya Wizara ya Fedha na Mipango
  • Jamvi la Habari
  • Tovuti ya Tamisemi
  • Tovuti ya Serikali
  • Sekretarieti ya Ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Location Map

Wasiliana Nasi

    Karatu District Council

    Sanduku la Posta: P.O Box 190

    Simu: +255 272970648

    Simu ya Mkononi: 0754773947

    Barua Pepe: ded@karatudc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Haki Miliki @ 2017 Halmashauri ya Wilaya ya Karatu.Haki zote zimehifadhiwa