• Wasiliana Nasi |
    • Maswali |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Complains |
Karatu District Council
Karatu District Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Karatu

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Dhamira na Dira
    • Historia
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Fedha na Biashara
      • Ujenzi
      • Afya
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
    • Vitengo
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma Zetu
  • Madiwani
  • Miradi
    • TASAF
    • BOOST
  • Machapisho
    • Hali ya Uwekezaji
      • Business License Form
  • Kituo cha Habari
    • Video
    • Habari
    • Hotuba kwa Vyombo vya Habari
    • Maktaba ya Picha

MILLION 210 ZATOLEWA NA SERIKALI, UJENZI WA MAABARA KARATU

Posted on: October 6th, 2020

NA TEGEMEO KASTUS

Serikali imetoa takribani million 210 kwa ajili ya ujenzi wa maabara katika shule za sekondari wilayani Karatu. Fedha hizo zimetoka katika mfuko wa EP4R,  Maabara hizo zitajengwa shule ya sekondari Domel, Mang’ola, Qurus, Getamock,  Baray Khusumay, Diego na Kansay sekondari.

Hayo yamesemwa na Mkuu wa wilaya ya Karatu Mh. Abbas Kayanda alipokuwa anazungumza na walimu wakuu, Maafisa watendaji wa vijiji, Kata na watumishi wa afya katika tarafa ya Mbulumbulu katika mkutano uliofanyika shule ya sekondari Diego. Mkuu wa wilaya alitumia kikao hicho  kusikiliza changamoto mbalimbali wanazokabiliana watumishi  hao katika maeneo  ya  kazi. Aidha serikali itaendelea kuimarisha miundo mbinu ya afya na elimu hatua kwa hatua.

Mkuu wa wilaya ya Karatu Mh. Abbas Kayanda akiwa katika kikao na watumishi

Mh. Kayanda amesema katika kukabiliana na tatizo la uhaba wa walimu, bado serikali inaendelea kuajiri walimu, na pia Halmashauri itagawa walimu waliopo katika shule ambazo hazina walimu kabisa, mathalani kama shule ina walimu wa hesabu au phyisics wawili basi mmoja aende shule isiyo na mwalimu hata mmoja wa masomo hayo. Mh. Kayanda amesema upo umuhimu wa kuwapongeza walimu wanaofanya vizuri katika ufundishaji na ufaulishaji. Amesema jambo hilo litawaongezea ari walimu katika kutekeleza majukumu yao ya kila siku.

Mh. Kayanda ametoa maelekezo kwa   Maafisa watendaji wa kijiji; kata, na tarafa kujenga tabia kutembelea taasisi zinazowazunguka katika maeneo yao ya kiutendaji, ili kubaini changamoto na kuzitatua ikiwa ni pamoja na kuzitolea taarifa wilayani changamoto ambazo ziko  nje ya uwezo wao ili ziweze kupatiwa ufumbuzi. Amesema watendaji wanapaswa kufuatilia na kuchukua hatua za kisheria  kwa wanafunzi waliopewa mimba. Maafisa hao watendaji wanapaswa kufuatilia na kuchukua hatua kwa wanafunzi watoro kwa kuhakikisha wanarejea shuleni.

Mh. Kayanda amesema serikali imefanya ukarabati na ujenzi wa   miundo mbinu katika kituo cha afya Kambi ya simba kwa gharama ya zaidi ya million 500. Amesema serikali imepeleka vifaa na  vifaa tiba katika kituo cha afya kambi ya simba vienye thamani ya zaidi ya million 200  na sasa upo mkakati wa kuchimba kisima cha maji  ili kusaidia kituo cha afya kambi ya simba kuwa na maji ya uhakika muda wote. Mh.Kayanda amesema  serikali imetoa fedha million 400 Kituo cha afya Endabash kwa ajili ya ujenzi na ukarabati na ujenzi, kituo hicho cha afya pia kimepokea vifaa na vifaa tiba . Mh. Kayanda ameomba watumishi kuthamini na kutunza miundo mbinu inayojengwa katika sekta ya afya na elimu.

Matangazo

  • Matokeo ya upimaji wa Kitaifa kidoto cha pili January 07, 2024
  • Halmashauri ya Wilaya ya Karatu Uchaguzi wa Wanafunzi wa kidato cha kwanza, 2024 December 18, 2023
  • Matokeo ya Darasa la Nne January 07, 2024
  • KIKAO CHA BARAZA LA MADIWANI 2024 May 11, 2024
  • Angalia Zote

Taarifa Mpya

  • MAAFISA UANDIKISHAJI WALA KIAPO KARATU

    May 14, 2025
  • DED HOKORORO ASHIRIKI KIKAO CHA ALAT WILAYA YA MERU

    May 15, 2025
  • MADAKTARI BINGWA WA SAMIA AWAMU YA TATU WATUA KARAU

    May 12, 2025
  • KARATU WASAPOTIJUHUDI ZA RAIS SAMIA WATANGAZA UTALII WA NDANI

    May 11, 2025
  • Angalia Zote

Video

DC KOLIMBA ATATUA KERO TARAFA YA EYASI KARATU
Video Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fursa za Uwekezaji

Viunganishi Linganifu

  • Tovuti ya Wizara ya Fedha na Mipango
  • Jamvi la Habari
  • Tovuti ya Tamisemi
  • Tovuti ya Serikali
  • Sekretarieti ya Ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Location Map

Wasiliana Nasi

    Karatu District Council

    Sanduku la Posta: P.O Box 190

    Simu: +255 272970648

    Simu ya Mkononi: 0754773947

    Barua Pepe: ded@karatudc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Haki Miliki @ 2017 Halmashauri ya Wilaya ya Karatu.Haki zote zimehifadhiwa