• Wasiliana Nasi |
    • Maswali |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Complains |
Karatu District Council
Karatu District Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Karatu

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Dhamira na Dira
    • Historia
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Fedha na Biashara
      • Ujenzi
      • Afya
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
    • Vitengo
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma Zetu
  • Madiwani
  • Miradi
    • TASAF
    • BOOST
  • Machapisho
    • Hali ya Uwekezaji
      • Business License Form
  • Kituo cha Habari
    • Video
    • Habari
    • Hotuba kwa Vyombo vya Habari
    • Maktaba ya Picha

MIPANGO HUENDANA NA TAKWIMU SAHIHI ZA WATU

Posted on: May 7th, 2021

NA TEGEMEO KASTUS

Maendeleo yeyote katika nchi yanapangwa kutokana na takwimu za watu, serikali inajenga miundo mbinu ya maendeleo kutokana na takwimu ya idadi ya watu. Takwimu ndio inasaidia kujua mahitaji ya watu kulingana na umri. Hivyo kujua idadi sahihi ya wakazi inarahisha katika kupanga mikakati endelevu  ya kimaendeleo ikiwa ni pamoja na kutengeneza sera zinazoendana na mahitaji ya jamiii.

Hayo yamesemwa na mkuu wa wilaya ya Karatu Mh. Abbas Kayanda alipokuwa anafungua mafunzo ya  siku tatu ya kuandaa watendaji watakao shiriki katika zoezi la kusajili watoto wenye umri wa chini ya miaka mitano. Usajili wa uandikishaji wa watoto wenye umri wa chini ya miaka mitano unafanywa na RITA kwa kushirikiana na shirika la UNICEF na zoezi hili lilianza nchini Tanzania tangu mwaka 2013. Usajili huo unatarajiwa kufanyika kwa muda wa siki 90, Mh. Kayanda ametoa rai kwa watendaji kufanya zoezi hilo kwa ukamilifu wake. Amesema kazi ifanyike kulingana na maelekezo ya wataalamu.

Mh. Abbas Kayanda (kulia) akizungumza na watendaji wakati wa ufunguzi wa mafunzo

Mh. Kayanda amesema serikali inataka kuwa mpango taarifa wa watoto wenye umri wa chini ya miaka mitano, amesema katika wilaya ya Karatu watoto zaidi ya 40259 wanatarajiwa kusajiliwa. Amesema kila mtoto mwenye umri wa chini ya miaka mitano anapaswa kusajiliwa, Amesema kwa watoto wa chini ya miaka mitatu tunatarjia kushirikiana na wasimamizi wa vituo vya afya kupata takwimu za watoto wanaokuja kupata huduma za chanjo. Amesema kwa watoto walio juu ya umri wa miaka mitatu na mitano watendaji ndio watakuwa na jukumu la kupita katika maeneo yao ya kiutendaji  ili kuhamashisha wazazi wawasajili watoto.

Amesema takwimu hizo zitasadia serikali katika mpango wake wa elimu bure lakini katika matibabu kwa watoto wenye umri chini ya miaka mitano. Mh. Kayanda amesema ni vyema watendaji wa zoezi hilo waheshimu viapo watakavyoapa wakati wa utekelezaji wa zoezi hilo.

Matukio mbalimbali katika picha wakati wa ufunguzi wa semina 

Matangazo

  • Wasimamizi, Wasaidizi, na Makarani wa Vituo October 06, 2025
  • Halmashauri ya Wilaya ya Karatu Uchaguzi wa Wanafunzi wa kidato cha kwanza, 2024 December 18, 2023
  • Matokeo ya Darasa la Nne January 07, 2024
  • KIKAO CHA BARAZA LA MADIWANI 2024 May 11, 2024
  • Angalia Zote

Taarifa Mpya

  • RC MAKALLA AISHAURI TUME YA TAIFA YA UMWAGILIAJI KUFANYA MAAMUZI KWA MKANDARASI BWAWA LA EYASI.

    September 23, 2025
  • WAKULIMA MANG’OLA WAMSHUKURU RAIS SAMIA KWA MRADI WA UMWAGILIAJI

    September 23, 2025
  • WENYE SIFA WATAKIWA KUOMBA MIKOPO HALMASHAURI

    September 24, 2025
  • UKUSANYAJI WA MAPATO UNAZIDI KUONGEZEKA KARATU

    September 24, 2025
  • Angalia Zote

Video

DC KOLIMBA ATATUA KERO TARAFA YA EYASI KARATU
Video Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fursa za Uwekezaji

Viunganishi Linganifu

  • Tovuti ya Wizara ya Fedha na Mipango
  • Jamvi la Habari
  • Tovuti ya Tamisemi
  • Tovuti ya Serikali
  • Sekretarieti ya Ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Location Map

Wasiliana Nasi

    Karatu District Council

    Sanduku la Posta: P.O Box 190

    Simu: +255 272970648

    Simu ya Mkononi: 0754773947

    Barua Pepe: ded@karatudc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Haki Miliki @ 2017 Halmashauri ya Wilaya ya Karatu.Haki zote zimehifadhiwa