• Wasiliana Nasi |
    • Maswali |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Complains |
Karatu District Council
Karatu District Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Karatu

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Dhamira na Dira
    • Historia
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Fedha na Biashara
      • Ujenzi
      • Afya
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
    • Vitengo
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma Zetu
  • Madiwani
  • Miradi
    • TASAF
    • BOOST
  • Machapisho
    • Hali ya Uwekezaji
      • Business License Form
  • Kituo cha Habari
    • Video
    • Habari
    • Hotuba kwa Vyombo vya Habari
    • Maktaba ya Picha

MIPANGO YA AFISA ELIMU IMEANZA KUJIBU

Posted on: July 12th, 2019

Afisa elimu sekondari amepongeza shule za sekondari za kidato cha tano na sita kwa matokeo mazuri waliyopata katika mitihani yao ya taifa. Matokeo hayo yanaashiria kuna jitihada madhubuti za kuinua taaluma zinafanyika katika shule hizo. Amesema hayo katika ziara ya kutembelea shule za sekondari kujionea utendaji kazi wa walimu juu ya maelekezo aliyowapatia.

Bi, Kalista Maina amesema ziara hizo ndio kwanza zimeanza, lazima Karatu tusogee mbele  kupitia mikakati tuliojiwekea. Amesema amefurahi kuona shule ya sekondari Karatu haina ufaulu wa daraja sifuri kuwa na wanafunzi zaidi ya 200 ni jambo la kipekee. Amesema shule kama Ganako sekondari wameishia ufaulu wa daraja la tatu hakuna daraja la nne wala daraja sifuri. Amesema Anagamazo nao wamefanya vizuri na matokeo yanatoa mwelekeo wa njia tunayopaswa kuifuata. Bi, Maina amesema hao wameshaanza kujitambua, sasa ni wakati wa kidato cha nne nao kufuata mwelekea huo.


afisa elimu sekondari akiwa katika ukaguzi wa utendaji kazi wa walimu


Bi. Maina amesema alihudhuria mahafali ya shule ya Agamazo akawapa Mikakati ya mbinu 25 za kutumia ili kuinua ufaulu wa kitaaluma. Amesema  wameipokea vizuri  na wanaifanyia kazi, kwa sababu nimeona mwelekeo wa matokeo yao. Ameongeza kusema mikakati aliyotoa, kwa mwalimu mfuatiliaji lazima atapata matokeo chanya.

Afisa elimu taalumu Ndugu Robert Sijaona amesema matokeo ya kidato cha sita ufaulu wa kitaaluma umepanda. Amesema hiyo inatokana na mipango ya idara ya elimu iliyopanga katika kuinua kiwango cha taaluma. Amesema kwa Karatu sekondari kuna wanafunzi waliopata daraja la kwanza 91 wanafunzi waliopata daraja la pili 170 na daraja la tatu 99 na wanafunzi waliopata daraja la nne wako 10. Amesema Ganako sekondari kuna wanafunzi 11 waliopata ufaulu wa daraja la kwanza wanafunzi waliopata ufaulu wa daraja la pili 14 na ufaulu wa daraja la tatu wanafunzi 6. Amesema shule ya Floriani ina wanafunzi 8 waliopata daraja la kwanza, na wanafunzi 53 wamepata ufaulu wa daraja la pili, wanafunzi waliopata ufaulu wa daraja la tatu 61 na ufaulu wa daraja la nne ni wanafunzi 4 na wanafunzi 3 wamepata daraja sifuri.

Picha za matukio mbalimbali wakati wa ukaguzi wa ziara ya Afsa elimu

Ndugu Sijaona amesema ukiangalia uwiano huo wa ufaulu kuna ongezeko la ufaulu wa wanafunzi wa daraja la kwanza, la pili na la tatu ambao ni wengi kuliko waliopata daraja la nne na daraja sifuri. Ndugu Sijaona amesema shule ya Floriani ni shule inayochukua michepuo ya sayansi  michepuo ya CBG na CBA. Ndugu Sijaona amesema Florian nayo bado inaendelea kusogea juu kwa ufaulu wa kitaaluma tofauti na wakati shule inaanzishwa, uhaba wa walimu wa  masomo ya sayansi ulikuwa unasumbua maendeleo ya kitaaluma ya shule hiyo. Amesema kulikuwa na uhaba wa walimu wanaofundisha somo la kemia, tangu walimu wapelekwe shuleni, ufaulu umezidi kuimarika.

 Picha za matukio wakati wa ziara ya afisa elimu 

Matangazo

  • Matokeo ya upimaji wa Kitaifa kidoto cha pili January 07, 2024
  • Halmashauri ya Wilaya ya Karatu Uchaguzi wa Wanafunzi wa kidato cha kwanza, 2024 December 18, 2023
  • Matokeo ya Darasa la Nne January 07, 2024
  • NAFASI ZA KAZI 2024 April 21, 2024
  • Angalia Zote

Taarifa Mpya

  • MILIONI 400 ZATOLEWA KARATU, KUJENGA MABWENI NA MADARASA EYASI SEKONDARI

    January 30, 2025
  • WASIMAMIZI WAASWA KUSIMAMIA VIAPO VYAO KUELEKEA UCHAGUZI WA SERIKALI ZA MITAA 2024.

    November 23, 2024
  • JESHI LA AKIBA MKAWE WAZALENDO KWA TAIFA

    November 23, 2024
  • HALMASHAURI YAZINDUA KITABU CHA MPANGO MKAKATI WA UKUSANYAJI MAPATO.

    November 19, 2024
  • Angalia Zote

Video

DC KOLIMBA ATATUA KERO TARAFA YA EYASI KARATU
Video Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fursa za Uwekezaji

Viunganishi Linganifu

  • Tovuti ya Wizara ya Fedha na Mipango
  • Jamvi la Habari
  • Tovuti ya Tamisemi
  • Tovuti ya Serikali
  • Sekretarieti ya Ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Location Map

Wasiliana Nasi

    Karatu District Council

    Sanduku la Posta: P.O Box 190

    Simu: +255 272970648

    Simu ya Mkononi: 0754773947

    Barua Pepe: ded@karatudc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Haki Miliki @ 2017 Halmashauri ya Wilaya ya Karatu.Haki zote zimehifadhiwa