• Wasiliana Nasi |
    • Maswali |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Complains |
Karatu District Council
Karatu District Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Karatu

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Dhamira na Dira
    • Historia
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Fedha na Biashara
      • Ujenzi
      • Afya
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
    • Vitengo
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma Zetu
  • Madiwani
  • Miradi
    • TASAF
    • BOOST
  • Machapisho
    • Hali ya Uwekezaji
      • Business License Form
  • Kituo cha Habari
    • Video
    • Habari
    • Hotuba kwa Vyombo vya Habari
    • Maktaba ya Picha

MIRADI YA MABILIONI YA FEDHA YATEMBELEWA NA MWENGE ARUSHA

Posted on: June 13th, 2019

Mwenge wa uhuru umemaliza mbio zake katika mkoa wa Arusha na kukabidhiwa mkoa wa Manyara. Kaimu mkuu wa mkoa wa Arusha mhe. Iddi Kimanta amesema mwenge wa uhuru umetembelea; umeweka jiwe la msingi, kufungua na kuzindua miradi 57 yenye thamani ya shilingi billion mia tano sabini na nane milioni mitatu na sitini na laki tisa na arobaini na tano elfu na senti hamsini.

Miradi kumi na nne kati ya kumi na tano imewekewa jiwe la msingi,miradi minne imefunguliwa na miradi kumi na mbili imezinduliwa. Mhe. Kimanta amesema miradi ishirini na sita itembelewa na kukaguliwa ili kuona maendeleo yake. Miradi iliyotembelewa ilikuwa ni ya sekta ya maji, afya, ujenzi wa barabara, elimu, utawala, kilimo, uvuvi na uhifadhi wa mazingira. Miradi miwili kati ya Hamsini na saba ilibainika kuwa na kasoro, mmoja ulikuwa ni wa kuwekewa jiwe la msingi na mwingine ulikuwa wa kutembelewa na kukaguliwa, yote ikiwa ni miradi ya maji.

Mhe. Kimanta amesema kiongozi wa mbio za mwenge ametoa maelekezo kwa miradi hiyo na Mhe. Kimanta amesema mkoa umeshaanza kuyafanyia kazi maelekezo ya kiongozi wa mbio za mwenge kitaifa. Amesema baada ya wiki mbili maelekezo yatakuwa yamefanyiwa kazi na taarifa hiyo kupewa mkimbiza mwenge. Mhe. Kimanta amesema miradi iliyowekewa mawe ya msingi wakati wa mbio za mwenge itafuatiliwa ili ikamilike kwa wakati na kwa viwango vinavyolingana na thamani ya fedha. Mhe Kimanta amesema miradi iliyozinduliwa na kufunguliwa  kwa matumizi mkoa utahakikisha miradi hiyo itatumika malengo yaliyokusudiwa  inatunza na kuenziwa kwa tija kwa miaka mingi ijayo.

Kaimu mkuu wa mkoa wa Arusha Mhe. Iddi Kimanta amesema mwenge wa uhuru umeeendelea kusisitiza mapambano dhidi ya rushwa. Mwenge wa uhuru umeendelea kugusia juu ya athari za ugonjwa wa ukimwi, viongozi wa mbio za mwenge wamewaomba wananchi kuepuka tabia hatarishi kama ngono zembe ambazo zinaongeza maambukizi mapya ya ukimwi. Katika mikesha ya  mbio za Mwenge wa uhuru, huduma za afya pamoja na ushauri nasaha zilikuwa zinatolewa. Mbio za mwenge wa uhuru umetoa elimu juu ya madawa ya athari ya dawa za kulevya, kupima vimelea vya malaria uchunguzi wa magonjwa yasiyoambukiza huduma ya lishe.

Jumla ya unit za damu zilizochangiwa ni 134 walijitokeza kupima ukimwi 2323 wanaume 1570 wanawake753 waliokutwa na maambukizi ni 23 sawa 0.99%. walijitokeza kupima malaria ni watu 802 na wanaume 521 wanawake 281 waliokutwa na malaria ni watu 2. Mhe.Kimanta amewapongeza wakimbiza mbio za mwenge kitaifa wakiongozwa na Ndugu Mzee Mkongea Alli kwa kazi nzuri katika mbio za mwenge Arusha amesema wamekuwa wawazi na wakweli.

Kiongozi wa mbio za mwenge Ndugu Mzee Mkongea Alli ameshukuru uongozi wa mkoa wa Arusha kwa ushirikiano mkubwa.  Lakini ameshukuru wananchi kwa muitikio walitoa kwenye mbio za mwenge mkoani Arusha. Ndugu Mkongea amesema ameona mambo mengi mazuri, wameona miundo mbinu ya madarasa, afya, na maji. lakini katika kipengele cha asilimia kumi ya kutoa mikopo kwa wananchi kimeendana  na matakwa.

Matangazo

  • Matokeo ya upimaji wa Kitaifa kidoto cha pili January 07, 2024
  • Halmashauri ya Wilaya ya Karatu Uchaguzi wa Wanafunzi wa kidato cha kwanza, 2024 December 18, 2023
  • Matokeo ya Darasa la Nne January 07, 2024
  • KIKAO CHA BARAZA LA MADIWANI 2024 May 11, 2024
  • Angalia Zote

Taarifa Mpya

  • MAAFISA UANDIKISHAJI WALA KIAPO KARATU

    May 14, 2025
  • DED HOKORORO ASHIRIKI KIKAO CHA ALAT WILAYA YA MERU

    May 15, 2025
  • MADAKTARI BINGWA WA SAMIA AWAMU YA TATU WATUA KARAU

    May 12, 2025
  • KARATU WASAPOTIJUHUDI ZA RAIS SAMIA WATANGAZA UTALII WA NDANI

    May 11, 2025
  • Angalia Zote

Video

DC KOLIMBA ATATUA KERO TARAFA YA EYASI KARATU
Video Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fursa za Uwekezaji

Viunganishi Linganifu

  • Tovuti ya Wizara ya Fedha na Mipango
  • Jamvi la Habari
  • Tovuti ya Tamisemi
  • Tovuti ya Serikali
  • Sekretarieti ya Ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Location Map

Wasiliana Nasi

    Karatu District Council

    Sanduku la Posta: P.O Box 190

    Simu: +255 272970648

    Simu ya Mkononi: 0754773947

    Barua Pepe: ded@karatudc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Haki Miliki @ 2017 Halmashauri ya Wilaya ya Karatu.Haki zote zimehifadhiwa