• Wasiliana Nasi |
    • Maswali |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Complains |
Karatu District Council
Karatu District Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Karatu

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Dhamira na Dira
    • Historia
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Fedha na Biashara
      • Ujenzi
      • Afya
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
    • Vitengo
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma Zetu
  • Madiwani
  • Miradi
    • TASAF
    • BOOST
  • Machapisho
    • Hali ya Uwekezaji
      • Business License Form
  • Kituo cha Habari
    • Video
    • Habari
    • Hotuba kwa Vyombo vya Habari
    • Maktaba ya Picha

MIRADI YA MAENDELEO INATEGEMEA MAKUSANYO YA KODI

Posted on: February 23rd, 2021

Na Tegemeo Kastus

Haiwezekani kuendesha Halmashauri bila kukusanya mapato, Mamlaka ya mji mdogo lazima ifahamu inadhamana ya kukusanya mapato. Mambo yote yaliyopitishwa ya utekelezaji wa shughuli za maendeleo yanategemea mapato ya ndani.

Hayo yamesemwa na Mkuu wa wilaya ya Karatu Mh, Abbas Kayanda katika kikao cha baraza la madiwani cha kupitisha bajeti ya mwaka ujao wa fedha. Amesema lazima Mamlaka ya mji mdogo ikusanye mapato ili iweze kujiendesha vizuri na kufikia malengo waliojiwekea kwenye bajeti, kufanya hivyo kunasaidia mamlaka hiyo kuweza kujiendesha. Swala la kukusanya mapato si la madiwani wala watendaji pekeyao linapaswa kufanya kwa umoja. Amesema miradi ya ujenzi wa kituo cha afya kitakacho gharimu million 400, ujenzi wa ukumbi na kuboreshwa uwanja wa michezo yanategemea na jinsi Halmashauri itakavyojitoa kukusanya mapato ya ndani.

Matukio tofauti wakati wa kikao cha baraza la madiwani

Mh. Kayanda amegusia swala la ukusanyaji wa kodi ya majengo ambalo limerudishwa Halmashauri, amesema utekelezwaji wa swala hilo sasa utaanza kwa kuandaa mpango taarifa za majengo kwa kukusanya taarifa za majengo yote yaliyo katika Halmashauri ya Karatu. Zoezi la ukusanyaji wa kodi hiyo ya majengo linatarajiwa kuanza kufanyika mwezi wa nne. Amesema kumekuwa na kususua kwa watu kulipa kodi ya majengo, kodi hiyo inakusanywa na Halmashauri kwa niaba ya serikali kuu. Ametoa wito kwa watendaji kuelimisha wananchi ili waone umuhimu wa kulipia kodi ya majengo. Ameongeza kusema maendeleo ya nchi yeyote yanategemeana na uwezo wa nchi katika kukusanya kodi.

Naye Mwenyekiti wa Halmashauri Mh. John Lucian amesema katika bajeti ya mwaka huu kituo cha afya kilichotengewa million 400 kitajengwa katika kata ya Buger. Amesema wamekubaliana kujenga machinjio ya ng’ombe Karatu ikiwa ni pamoja na ujenzi wa machinjio ya kuku Karatu miradi ambayo ikikamilika itasaidia kuongeza mapato ya Halmashauri.

Mh. Lucian amesema kitaaluma kwa mwaka ujao wa fedha wamelenga kununua mashine za kurudufisha makaratasi “Photocopy Machine” ikiwa ni pamoja na kufanyia ukarabati magari ili kuwezesha maafisa elimu kufanya ufuatiliaji wa maaendeleo ya kitaaluma kwa karibu. Amesema katika bajeti ijayo ya mwaka wa fedha wanafunzi kumi bora wa sekondari na wanafunzi kumi bora wa shule za msingi watatambuliwa na baraza la madiwani.

Mh. Lucian amesema kila afisa elimu amepewa kata yake ya kuilea kitaaluma ili kuongeza kiwango cha ufaulu. Lengo ni kupata mahusiano ya karibu kati walimu na watendaji wa wilayani katika kubaini na kutatua changamoto zinazodidimiza ubora wa elimu.

Madiwani wakiwa katika kikao cha baraza la bajeti

Matangazo

  • Matokeo ya upimaji wa Kitaifa kidoto cha pili January 07, 2024
  • Halmashauri ya Wilaya ya Karatu Uchaguzi wa Wanafunzi wa kidato cha kwanza, 2024 December 18, 2023
  • Matokeo ya Darasa la Nne January 07, 2024
  • KIKAO CHA BARAZA LA MADIWANI 2024 May 11, 2024
  • Angalia Zote

Taarifa Mpya

  • MAAFISA UANDIKISHAJI WALA KIAPO KARATU

    May 14, 2025
  • DED HOKORORO ASHIRIKI KIKAO CHA ALAT WILAYA YA MERU

    May 15, 2025
  • MADAKTARI BINGWA WA SAMIA AWAMU YA TATU WATUA KARAU

    May 12, 2025
  • KARATU WASAPOTIJUHUDI ZA RAIS SAMIA WATANGAZA UTALII WA NDANI

    May 11, 2025
  • Angalia Zote

Video

DC KOLIMBA ATATUA KERO TARAFA YA EYASI KARATU
Video Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fursa za Uwekezaji

Viunganishi Linganifu

  • Tovuti ya Wizara ya Fedha na Mipango
  • Jamvi la Habari
  • Tovuti ya Tamisemi
  • Tovuti ya Serikali
  • Sekretarieti ya Ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Location Map

Wasiliana Nasi

    Karatu District Council

    Sanduku la Posta: P.O Box 190

    Simu: +255 272970648

    Simu ya Mkononi: 0754773947

    Barua Pepe: ded@karatudc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Haki Miliki @ 2017 Halmashauri ya Wilaya ya Karatu.Haki zote zimehifadhiwa