• Wasiliana Nasi |
    • Maswali |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Complains |
Karatu District Council
Karatu District Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Karatu

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Dhamira na Dira
    • Historia
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Fedha na Biashara
      • Ujenzi
      • Afya
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
    • Vitengo
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma Zetu
  • Madiwani
  • Miradi
    • TASAF
    • BOOST
  • Machapisho
    • Hali ya Uwekezaji
      • Business License Form
  • Kituo cha Habari
    • Video
    • Habari
    • Hotuba kwa Vyombo vya Habari
    • Maktaba ya Picha

MKAZO WAWEKWA MATUMIZI MAZURI YA FEDHA

Posted on: February 22nd, 2021

Na Tegemeo Kastus

Fedha zinazotolewa na Halmashauri kwa ajili  ya miradi ya maendeleo, Madiwani wa maeneo husika wapewe taarifa kwenye kata zao. Ukiwapa taarifa madiwani kiasi cha fedha zilizotengwa kwa ajili ya maendeleo kwenye kata zao inakuwa ni rahisi kuzifuatilia na kuzisimamia kwa karibu.

Hayo yamesemwa na Mwenyekiti wa Halmashauri Mh. John Lucian wakati akifunga kikao cha kawaida cha baraza la madiwani. kilicholenga kufanya mapitio ya bajeti ya mwaka elfu mbili kumi na tisa na elfu mbili na shirini kwa kipindi cha miezi sita iliyopita. Amesema fedha asilimia arobaini kwa ajili ya maendeleo ya miradi ziende haraka kwenye maeneo husika. Amesema serikali imetoa fedha kiasi cha billion moja kwa ajili ya ujenzi wa majengo manne ya hospitali ya wilaya ameomba kuwe na kamati yenye  uwazi katika usimamizi wa majengo. Amesema atateuwa madiwani wanne ambao kila diwani atasimamia ujenzi wa jengo lake. Amesema kuna fedha kiasi cha million mia na hamsini za ukarabati wa zahanati tatu lazima usimamizi wa hali ya juu ufanyike kuanzia kwa diwani wa eneo husika na viongozi wa chini.

Watendaji wakiwa katika kikao cha kawaida cha baraza la madiwani.

Mh. Lucian akizungumzia kuhusu mikopo inayotolewa na Halmashauri amesema ni vyema vikundi vikafanyiwa uchunguzi. Amesema kujiridhisha kunasaidia fedha kutopotea kwenye vikundi, amesema ikiwezekana fedha zitumike kununa vifaa vya uzalishaji badala ya kuwapa wanakikundi fedha hiyo itasaidia kupunguza matumizi mabaya ya fedha.

Naye Mkurugenzi Mtendaji Ndg. Waziri Mourice akizungumza katika baraza hilo amesema vikundi hupewa fedha na Halmashauri ikiwa ni pamoja na muda wa miezi miwili kama kipindi cha matazamio kabla ya kuanza kurejesha mikopo. Amesema vikundi vya kinamama vinaongoza kwa kurejesha mikopo isiyo na riba kwa wakati kulinganisha na vikundi vya vijana.

Ndg.Waziri Mourice amesema vikundi vya vijana vinachangamoto ya kugawanyika pindi wanapopokea fedha. Hiyo husababisha vikundi kupitia wakati mgumu  kuzirejesha fedha hizo.  Amesema ni vyema sasa vikundi viwe vinaanza kutambuliwa kwenye ngazi ya kata husika. 

Katika hatua nyingine Mh. Rehema amesema kuna umuhimu wa kuwashirikisha kwa karibu watendaji wa vijiji na watendaji wa kata katika kusaidia kusajili vikundi. amesema kama watendaji wa kata na vijiji wakihusishwa kwa karibu ni rahisi kufuatilia mikopo ya vikundi katika kata  na vijiji vyao.


waheshimiwa Madiwani katika matukio tofauti wa kati wa baraza la Madiwani

Matangazo

  • Matokeo ya upimaji wa Kitaifa kidoto cha pili January 07, 2024
  • Halmashauri ya Wilaya ya Karatu Uchaguzi wa Wanafunzi wa kidato cha kwanza, 2024 December 18, 2023
  • Matokeo ya Darasa la Nne January 07, 2024
  • KIKAO CHA BARAZA LA MADIWANI 2024 May 11, 2024
  • Angalia Zote

Taarifa Mpya

  • MAAFISA UANDIKISHAJI WALA KIAPO KARATU

    May 14, 2025
  • DED HOKORORO ASHIRIKI KIKAO CHA ALAT WILAYA YA MERU

    May 15, 2025
  • MADAKTARI BINGWA WA SAMIA AWAMU YA TATU WATUA KARAU

    May 12, 2025
  • KARATU WASAPOTIJUHUDI ZA RAIS SAMIA WATANGAZA UTALII WA NDANI

    May 11, 2025
  • Angalia Zote

Video

DC KOLIMBA ATATUA KERO TARAFA YA EYASI KARATU
Video Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fursa za Uwekezaji

Viunganishi Linganifu

  • Tovuti ya Wizara ya Fedha na Mipango
  • Jamvi la Habari
  • Tovuti ya Tamisemi
  • Tovuti ya Serikali
  • Sekretarieti ya Ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Location Map

Wasiliana Nasi

    Karatu District Council

    Sanduku la Posta: P.O Box 190

    Simu: +255 272970648

    Simu ya Mkononi: 0754773947

    Barua Pepe: ded@karatudc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Haki Miliki @ 2017 Halmashauri ya Wilaya ya Karatu.Haki zote zimehifadhiwa