• Wasiliana Nasi |
    • Maswali |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Complains |
Karatu District Council
Karatu District Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Karatu

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Dhamira na Dira
    • Historia
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Fedha na Biashara
      • Ujenzi
      • Afya
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
    • Vitengo
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma Zetu
  • Madiwani
  • Miradi
    • TASAF
    • BOOST
  • Machapisho
    • Hali ya Uwekezaji
      • Business License Form
  • Kituo cha Habari
    • Video
    • Habari
    • Hotuba kwa Vyombo vya Habari
    • Maktaba ya Picha

MOURICE; LAZIMA TUSIMAMIE UJENZI WA SOKO UKAMILIKE

Posted on: August 10th, 2019

Kamati ya siasa ya chama cha mapinduzi imetembelea mradi wa soko kuu la mjini Karatu, mradi ambao umefika katika hatua za upauzi. Sambamba na ukaguzi huo kamati hiyo imetoa muda kwa Halmashauri kukamilisha ujenzi kwa wakati ili kupunguza adha wanazopata wafanyabishara wa soko hilo.

Mwenyekiti wa chama cha mapinduzi wilayaya Karatu ndugu Lucian Akonay amesema kuna taarifa kwamba soko hilo limetelekezwa na aliyepewa mkataba ndugu Anatory Construction amepewa mkataba wa kujenga soko kuu la mjini. Mkandarasi amekuwa na tabia ya kuondoka nje ya mradi mara kwa mara na kasi ya kupauwa soko hilo ni ndogo jambo linalokwamisha  Wafanyabiashara ambao wanakaa sehemu ambayo si salama kufanya shughuli zao za biashara na kuna taarifa kwamba aliyepewa kazi ya kupaua soko hilo ameshindwa kutokana na ukadiriaji wa chini wa kazi. Ndugu Lucian amesema lazima tufanye maamuzi kwa maslahi ya wananchi ili mradi huo ukamilike kwa wakati.

Awali mkurugenzi mtendaji ndugu Waziri Morice amesema Anatory construction ilipewa tenda ya uzabuni wa vifaa katika soko hilo napia wamepewa tenda ya upauzi wa soko. Shughuli za ujenzi wa soko kuu mjini Karatu unatumia force accounts, amesema tenda ya upauzi inayohusisha Anatory constructions muda wake wa makubaliano umeisha tarehe 8/8/2019. Ndugu waziri amesema hata hivyo wakala huyo wa ujenzi alishaandikiwa barua ya onyo juu ya  uwezekano wa kuvunjwa mkataba wake kutokana na kutokuwepo eneo la kazi bila taarifa ya mwajiri.

Picha ya juu ikionesha upauaji wa soko

 Ndugu waziri amesema lazima ujenzi wa soko uendelee hata ikibidi kwa makubaliano na mafundi ili ujenzi uende kasi baada mkandarasi aliyepewa kazi ya upauzi Anatory constructions muda wake kufika kikomo kabla ya kufikia malengo ya mkataba. Ameongeza kusema anatambua wafanyabiashara waliokuwa wanafanya shughuli zao za biashara katika eneo hilo wanapata taabu sana hasa kipindi cha masika, malengo ni kukamilisha haraka kabla kipindi cha masika hakijawadia.

Injinia wa ujenzi wa Halmashauri  ndugu Venance Malamla katika taarifa yake kwa kamati ya siasa amesema Mradi wa soko hilo ulitarajiwa kugharimu kiasi cha million 540  kwa makisio ya awali. Kutokana na mapungufu ya fedha mradi umegawanywa katika hatua mbili za ujenzi, hatua ya kwanza ilikuwa ujenzi wa nguzo na kupauwa jengo lote ambayo ingegharimu million 222. Hatua ya pili ni ujenzi wa sakafu, kujenga meza, kujenga ukuta wa nje kuweka miundo mbinu ya maji. Ujenzi wa soko ulianza mwezi wa tano mwaka 2018 na ulitarajia kukamilika mwezi wa sita 2019

Matangazo

  • Matokeo ya upimaji wa Kitaifa kidoto cha pili January 07, 2024
  • Halmashauri ya Wilaya ya Karatu Uchaguzi wa Wanafunzi wa kidato cha kwanza, 2024 December 18, 2023
  • Matokeo ya Darasa la Nne January 07, 2024
  • KIKAO CHA BARAZA LA MADIWANI 2024 May 11, 2024
  • Angalia Zote

Taarifa Mpya

  • MAAFISA UANDIKISHAJI WALA KIAPO KARATU

    May 14, 2025
  • DED HOKORORO ASHIRIKI KIKAO CHA ALAT WILAYA YA MERU

    May 15, 2025
  • MADAKTARI BINGWA WA SAMIA AWAMU YA TATU WATUA KARAU

    May 12, 2025
  • KARATU WASAPOTIJUHUDI ZA RAIS SAMIA WATANGAZA UTALII WA NDANI

    May 11, 2025
  • Angalia Zote

Video

DC KOLIMBA ATATUA KERO TARAFA YA EYASI KARATU
Video Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fursa za Uwekezaji

Viunganishi Linganifu

  • Tovuti ya Wizara ya Fedha na Mipango
  • Jamvi la Habari
  • Tovuti ya Tamisemi
  • Tovuti ya Serikali
  • Sekretarieti ya Ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Location Map

Wasiliana Nasi

    Karatu District Council

    Sanduku la Posta: P.O Box 190

    Simu: +255 272970648

    Simu ya Mkononi: 0754773947

    Barua Pepe: ded@karatudc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Haki Miliki @ 2017 Halmashauri ya Wilaya ya Karatu.Haki zote zimehifadhiwa