• Wasiliana Nasi |
    • Maswali |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Complains |
Karatu District Council
Karatu District Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Karatu

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Dhamira na Dira
    • Historia
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Fedha na Biashara
      • Ujenzi
      • Afya
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
    • Vitengo
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma Zetu
  • Madiwani
  • Miradi
    • TASAF
    • BOOST
  • Machapisho
    • Hali ya Uwekezaji
      • Business License Form
  • Kituo cha Habari
    • Video
    • Habari
    • Hotuba kwa Vyombo vya Habari
    • Maktaba ya Picha

MPANGO WA SERIKALI NI UFAULU WA ASILIMIA TISINI

Posted on: April 19th, 2021

Na Tegemeo Kastus

Ufaulu wa shule za msingi mkoa wa Arusha unatakiwa kuanzia alama zaidi ya tisini na kuendelea kwa mitihani ya kitaifa. Mkurugenzi na Afisa elimu Msingi mnapaswa kulisimamia, lakini wazazi msimamie na mhakikishe watoto wanamahudhurio mazuri. Walimu mjipange katika kufundisha ili tuongeze kiwango cha ufaulu ili tusogee kwenda mbele baaada ya kuwa wa nafasi ya pili kitaifa kwa ufaulu mzuri.

Hayo yamesemwa na Mkuu wa mkoa wa Arusha Mh. Iddi Kimanta katika uzinduzi wa madarasa nane yaliojengwa na wadau wa maendeleo wa world vision katika shule ya msingi Endabash na madarasa mawili katika shule shikizi ya Endabash Salmay ikiwa ni pamoja na kuweka madawati. Ujenzi huo umegharimu kiasi cha zaidi ya million 558 ukijumuisha ujenzi wa vyoo vya watoto wakiume na wakike: ujenzi wa jengo la utawala, jengo la maktaba, ujenzi wa jengo wa jiko la kisasa na ukarabati wa madarasa matatu na mwaka huu wanatarajia kujenga madarasa mawili katika shule shikizi ya Endabash Salmay

Mh. Iddi Kimanta (katikati) akikagua miundo mbinu ya maji katika shule ya msingi Endabash

Mh. Kimanta amewapongeza shirika la world vision, amesema kuwa na mdau wa maendeleo wa namna hii lazima wananchi wajue kwamba ni fursa ya maendeleo, amesema wananchi wanatakiwa kutumia fursa hiyo kwa kuwaunga mkono shirika la world vision kwa kuwezesha utoaji wa elimu bora. Amesema namna ya kuwaunga mkono kwa wazazi ni lazima watoe mahitaji ya muhimu kwa wanafunzi ili waweze kusoma kwa bidii. Mh. Kimanta amewapongeza pia shirika la world vision kwa kusadia kujenga shule ya shikizi ya Salmay, amesema shule hiyo shikizi ya Endabash Salmay itasaidia kuondoa msongamano wa wanafunzi katika kijiji cha Endabash.

Akitoa salamu Mkuu wa wilaya ya karatu Mh. Abbas Kayanda  amesema shirika la world Vision limekuwa likisaidai katika miradi ya afya elimu na maji, amesema kwa mwaka huu wa fedha wametenga kiasi cha billion moja na million mianane kwa mradi wa maji Endesh na miradi mingine ya afya katika Tarafa ya Eyasi. Mh, Kayanda ameomba wananchi kuendelea kuunga mkono jitihada zinazofanywa na shirika la world vision, amesema serikali ya wilaya ya Karatu itaendelea kuwapa ushirikiano na kuwaunga mkono katika kazi wanazoendelea kuzifanya.

Mh. Iddi Kimanta akikagua miundo mbinu ya madarasa iliyojengwa na shirika la world vison katika shule ya msingi Endabash.

Awali katika salamu kwa wananchi Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Karatu Ndg. Waziri Mourice amesema shirika la world vision limetuokoa, kazi waliyoifanya ilipaswa kufanywa na Halmashauri na ingechukua muda mrefu kukamilika. Ndg. Mourice amesema shule ya msingi Endabash sasa hawana kizingizio cha kutofanya vizuri, kutokana na uboreshwaji wa miundo mbinu uliofanywa na world vision.

Msimamizi wa miradi ya world vision Tarafa ya Endabash Ndg.  Goodluck Nnko amesema katika utekelezaji wa miradi ulikabidhiwa andiko lake liliandikwa mwezi wa 10 mwaka 2019 na ulianza kufanya kazi mwezi wa 7 mwaka 2020. Amesema lengo la mradi lilikuwa kutoa mchango katika kuboresha na kuandaa mazingira rafiki kufundishia na kujifunzia. Amesema mradi ulijikita katika kuwezesha upatikanaji wa maji safi, navituo vya vitatu vya kunawia mikono.

Ndg. Nko amesema mradi ulijenga matundu ya vyoo 18 kununu mashine ya photocopy yenye uwezo wa kurudufisha na ku-print aina ya canon, meza na viti 13 na madawati 286. Amesema mradi uliendesha mafunzo kwa kamati ya shule na kuwajengea uwezo katika usimamizi wa elimu na ukusanyaji wa rasilimali. Ndg.  Nnko Amesema mradi utajenga kisima cha maji katika shule shikizi ya Endabash Salamay na kuboresha chumba kimoja cha darasa na kukifanya maktaba kwa kuweka samani na vitabu.

Katika taarifa yake Mkuu wa shule ya Msingi Endabash Mwl. Fredrick Maphie amesema shirika la world vision limewapatia kiasi cha computer 25 za wanafunzi na moja ya mwalimu. Amesema mradi umeongeza ari ya walimu katika ufundishaji na wanafunzi wameweza kuongeza ari ya kupenda kusoma. Amesema  wanafunzi wamefanya kwa mara ya kwanza  mtihani wa nusu mhula uliochapwa.

Matukio mbalimbali katika picha wakati wa kuweka kibao cha uzinduzi shule ya msingi Endabash.

Matangazo

  • Matokeo ya upimaji wa Kitaifa kidoto cha pili January 07, 2024
  • Halmashauri ya Wilaya ya Karatu Uchaguzi wa Wanafunzi wa kidato cha kwanza, 2024 December 18, 2023
  • Matokeo ya Darasa la Nne January 07, 2024
  • NAFASI ZA KAZI 2024 April 21, 2024
  • Angalia Zote

Taarifa Mpya

  • MILIONI 400 ZATOLEWA KARATU, KUJENGA MABWENI NA MADARASA EYASI SEKONDARI

    January 30, 2025
  • WASIMAMIZI WAASWA KUSIMAMIA VIAPO VYAO KUELEKEA UCHAGUZI WA SERIKALI ZA MITAA 2024.

    November 23, 2024
  • JESHI LA AKIBA MKAWE WAZALENDO KWA TAIFA

    November 23, 2024
  • HALMASHAURI YAZINDUA KITABU CHA MPANGO MKAKATI WA UKUSANYAJI MAPATO.

    November 19, 2024
  • Angalia Zote

Video

DC KOLIMBA ATATUA KERO TARAFA YA EYASI KARATU
Video Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fursa za Uwekezaji

Viunganishi Linganifu

  • Tovuti ya Wizara ya Fedha na Mipango
  • Jamvi la Habari
  • Tovuti ya Tamisemi
  • Tovuti ya Serikali
  • Sekretarieti ya Ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Location Map

Wasiliana Nasi

    Karatu District Council

    Sanduku la Posta: P.O Box 190

    Simu: +255 272970648

    Simu ya Mkononi: 0754773947

    Barua Pepe: ded@karatudc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Haki Miliki @ 2017 Halmashauri ya Wilaya ya Karatu.Haki zote zimehifadhiwa