• Wasiliana Nasi |
    • Maswali |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Complains |
Karatu District Council
Karatu District Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Karatu

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Dhamira na Dira
    • Historia
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Fedha na Biashara
      • Ujenzi
      • Afya
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
    • Vitengo
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma Zetu
  • Madiwani
  • Miradi
    • TASAF
    • BOOST
  • Machapisho
    • Hali ya Uwekezaji
      • Business License Form
  • Kituo cha Habari
    • Video
    • Habari
    • Hotuba kwa Vyombo vya Habari
    • Maktaba ya Picha

MRADI ULIOBUNIWA, UNATIJA KWA WIZARA YA MALIASILI NA UTALII

Posted on: July 21st, 2019

Waziri mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Kassim Majaliwa amefanya ziara wilayani Karatu. Katika ziara hiyo Waziri Mkuu Mhe. Majaliwa ameweka jiwe la msingi katika kituo cha ukaguzi wa utalii Bashay na amefungua kituo hicho cha utalii pamoja na kukabidhi gari kwa jeshi la polisi litakalotumika kuwaongoza watalii kutoka (airport) uwanja wa ndege na kwenda kwenye hifadhi za utalii.

Waziri Mkuu Mhe.Kasim Majaliwa amepongeza ubunifu wa mkuu wa mkoa wa Arusha kwa kujenga vituo hivyo vinne vya utalii. Amesema ujenzi wa vituo hivyo unatija kwa wizara ya maliasili na utalii. Amesema kituo hicho ni kizuri kina mambo mengi na faida nyingi sana. Mhe. Kassim Majaliwa amempongeza pia wakuu wa wilaya na watendaji kwa kazi nzuri, amesema swala la utalii limepewa kipaombele kikubwa sana. Waziri Mkuu amesema serikali kupitia Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli ametoa maelekezo sahihi aliyoyachambua kwenye ilani ya  chama cha mapinduzi ambacho kinataka serikali isimamie; ipange  itekeleze, na ijiridhishe sekta ya utalii inaendelea nchini ili faida zipatikane.

Mhe. Majaliwa amesema kuna utalii wa aina mbili, wa sisi wenyewe watanzania kwenda maeneo ya vivutio na wageni kutoka nje kuja kuona vivutio. Nchi yetu imebahatika kuwa na vivutio vingi sana, amesema tunafukwe nyingi na nzuri za mito na maziwa na bahari. Maeneo tuliyonayo ya vivutio ya Ngorongoro, Manyara Serengeti na mbuga nyingine. Mhe Kassim Majaliwa amesema vivutio vyote,  serikali imeamua kuviratibu vizuri ili utalii uweze kufanyika.

Mhe.Kasim Majaliwa amesema serikali imenunua ndege 8, sita zimeingia ndege ya saba inakuja mwezi wa 10 na ndege ya 8 inakuja mwezi wa kwanza mwakani. Amesema Mhe. Rais Dkt. John Pombe Magufuli amenunua ndege nyingine 3,  amesema ndege zilizopo chini zinaruka na kwenda kila mkoa na wananchi wanasafiri kwa kutumia ndege zao. Mhe. Kassim Majaliwa amesema sasa wameanza kuwaita watalii na kwenda kuwachukua kwa ndege. Amesema ndege zetu zimeanza safari za kwenda India, China, Zambia, Ethiopia, Zimbabwe na Afrika ya kusini, amesema malengo yetu ni kuwavuta watalii kuja Tanzania moja kwa moja. Amesema zamani watalii walikuwa wanadanganywa kuhusu vivutio vyetu.

Mhe. Kasim Majaliwa amesema watu wengi wanakuja hapa Karatu, Arusha lazima tutumie kituo hicho kuweka vivutio ambavyo watalii watapenda kuviona na kununua. Amesema eneo lilobaki kwenye kituo wananchi wapate fursa wakae na wafanye shughuli zao za kitalii. Waziri mkuu amemshukuru, Mzee Joseph na mama Joseph kwa kutoa eneo la kiwanja kwa ajili ya kituo cha utalii. Amewapongeza wadau wa utalii kwa ujenzi wa kituo hicho cha utalii, amesema wamefanya kazi nzuri sana. Amesema hao ndio wanatoa taarifa nzuri kwa Tanzania na kufanya wageni wapende kuja Tanzania. Waziri mkuu amesema TATO na mawakala wote wa utalii wamefanya kazi kubwa sana. Amesema TATO wameleta watalii kutoka nchini Izrael  1000  kwa mara moja na wote wamekuja Karatu. Kuna watalii kutoka China ambao tayari wameshafika 360,  na wiki ijayo wanakuja watalii wengine tena kutoka china watu 300 na  watalii kutoka chini Izrael wapatao 400. 

 Waziri Mkuu Mhe.Kassim Majaliwa akiliwasha gari la waongoza utalii ambalo amelikabidhi kwa jeshi la polisi.

Mhe. Waziri Mkuu amesema serikali mwaka huu imeanza kuondoa kodi kwa waddau wa watalii ili wapate faida na wazidi kuwekeza. Amesema kufanya hivyo itasaidia wananchi kunufaika na Halmashauri kunufaika na shughuli za utalii pia.  Mhe. Kassim Majaliwa ametoa wito kwa wananchi kuzidi kuchangamkia fursa za utalii na kuzidi kuboresha miundo mbinu ya hotel na tuhakikishe usalama wa watalii wanapokuwa katika safari zao za utalii.

Awali Mkuu wa Mkoa wa Arusha Mhe. Mrisho Gambo katika taarifa yake kwa Waziri Mkuu amesema; watu TATO wamefadhili askari kwenda kusoma kozi maalum ya kujifunza lugha, ili waweze kuhudumia watalii kwenye kituo cha utalii. Amesema kuna kituo  kimejengwa KATITI wilaya ya Arumeru ambacho Halmsahuri ya wilaya hiyo walitoa eneo kwa ajili ya ujenzi wa kituo na kimejengwa kwa 90% na watu wa TATO, kituo kingine kinajengwa wilaya Longido na Halmshauri ya wilaya hiyo imetoa kiwanja, kituo kingine kimejengwa Monduli, Halmashauri ya wilaya ya Monduli imetoa kiwanja katika eneo la Makuyuni. Mhe. Mrisho Gambo amesema awali kabla ya ujenzi wa vituo hivyo watalii walikuwa wanasimamishwa kwa ukaguzi zaidi mara 20, jambo ambalo lilileta malalamiko kwa watalli wengi.

Mhe. Mrisho Gambo amesema watu wa Mamlaka ya hifadhi ya Ngorongo wamejitolea kutoa wafanyakazi wa kudumu watakao fanya usafi katika maliwato ya kituo cha utalii Karatu. Mamlaka ya hifadhi ya Ngorongoro itaweka kituo cha kutoa taarifa  za utalii na kutakuwa na mtaalam atakayejihusisha na kutoa taarifa za utalii za hifadhi zetu katika kituo cha ukaguzi wa utalii Karatu. Mhe. Gambo amesema kuna wadau wa utalii wamejitolea kusaidia huduma ya internet kwa vituo vyote 4 vya ukaguzi wa utalii jambo ambalo litarahisisha utendaji kazi wa vituo.

Matangazo

  • Matokeo ya upimaji wa Kitaifa kidoto cha pili January 07, 2024
  • Halmashauri ya Wilaya ya Karatu Uchaguzi wa Wanafunzi wa kidato cha kwanza, 2024 December 18, 2023
  • Matokeo ya Darasa la Nne January 07, 2024
  • NAFASI ZA KAZI 2024 April 21, 2024
  • Angalia Zote

Taarifa Mpya

  • MILIONI 400 ZATOLEWA KARATU, KUJENGA MABWENI NA MADARASA EYASI SEKONDARI

    January 30, 2025
  • WASIMAMIZI WAASWA KUSIMAMIA VIAPO VYAO KUELEKEA UCHAGUZI WA SERIKALI ZA MITAA 2024.

    November 23, 2024
  • JESHI LA AKIBA MKAWE WAZALENDO KWA TAIFA

    November 23, 2024
  • HALMASHAURI YAZINDUA KITABU CHA MPANGO MKAKATI WA UKUSANYAJI MAPATO.

    November 19, 2024
  • Angalia Zote

Video

DC KOLIMBA ATATUA KERO TARAFA YA EYASI KARATU
Video Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fursa za Uwekezaji

Viunganishi Linganifu

  • Tovuti ya Wizara ya Fedha na Mipango
  • Jamvi la Habari
  • Tovuti ya Tamisemi
  • Tovuti ya Serikali
  • Sekretarieti ya Ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Location Map

Wasiliana Nasi

    Karatu District Council

    Sanduku la Posta: P.O Box 190

    Simu: +255 272970648

    Simu ya Mkononi: 0754773947

    Barua Pepe: ded@karatudc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Haki Miliki @ 2017 Halmashauri ya Wilaya ya Karatu.Haki zote zimehifadhiwa