• Wasiliana Nasi |
    • Maswali |
    • Barua Pepe za Watumishi |
    • Complains |
Karatu District Council
Karatu District Council

Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Karatu

  • Mwanzo
  • Kuhusu Sisi
    • Dhamira na Dira
    • Historia
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Idara
      • Fedha na Biashara
      • Ujenzi
      • Afya
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
    • Vitengo
  • Fursa za Uwekezaji
  • Huduma Zetu
  • Madiwani
  • Miradi
    • TASAF
    • BOOST
  • Machapisho
    • Hali ya Uwekezaji
      • Business License Form
  • Kituo cha Habari
    • Video
    • Habari
    • Hotuba kwa Vyombo vya Habari
    • Maktaba ya Picha

MRADI WA MAJI KUANZA MWEZI WA KUMI

Posted on: July 1st, 2019

Mkuu wa wilaya ya Karatu ameahidi kupeleka huduma ya maji kwenye kijiji cha Laja na vijiji vya jirani. Mhe. Theresia amesema hayo katika mkutano na wanakijiji wa kijiji cha Laja alipokuwa akisikiliza kero za wananchi. Mkutano huo ulihusisha wataalamu na wajumbe wa kijiji na wananchi wa kijiji cha Laja uliolenga kutatua kero za wananchi.

Mhe. Theresia amesema anafahamu adhaa ya maji wanayopata wananchi wa kijiji cha Laja na  vijiji vya jirani. Amesema serikali kwa kushirikiana na wadau wa maendeleo wa shirika la world vision wataanza kujenga miundo mbinu ya maji mwezi wa kumi mwaka huu. Mhe. Theresia amewahakikishia wananchi wa Laja mradi  wa maji utaanza kwa wakati. Amewaomba wananchi kushiriki kwa  kujitolea kuchimba mitaro wakati wa ujenzi wa miundo mbinu ya maji.

Wananchi wakiwa katika mkutano kijiji cha Laja

Mhe. Theresia amewahimiza wananchi kupenda kupata matibabu hospitali, amesema amepewa taarifa kijiji cha Laja kwamba wakinamama wajawazito wanaogopa kwa sababu kuna tabibu na wauguzi wa kiume. Mhe. Theresia amesema serikali italeta mhudumu wa kike, lakini bado wanapaswa kwenda hospital ili wapatiwe huduma ya kitabibu. Matabibu na wauguzi wa kiume wamesomea kazi ya kutoa tiba, hivyo amewaasa  wakinamama wajawazito  kuanza kwenda hospitali mapema.  Mhe. Theresia amesema kitanda cha kujifungulia kilikuwa kibovu katika zahanati ya Laja lakini sasa kinafanya kazi vizuri. Mhe Theresia amesema wakinamama waanze kuhudhuria Hospitali kuanzia wiki kumi na mbili, ili kufahamu maendeleo ya ujauzito wake na kuona kama mtoto amekaa sawa.

Mhe. Theresia ametumia mkutano huo kuwakumbusha wananchi juu ya uchaguzi wa serikali za mitaa, amewaomba wananchi kuendelea kulinda amani na utulivu. Amewahimiza wananchi kuchagua viongozi bora na siyo bora viongozi. Mhe.Theresia amewaomba wananchi kujitokeza kupiga kura katika uchaguzi huo. Mhe. Theresia amewaomba wananchi kutochagua viongozi wanaotoa rushwa. Amesema daftari la kupiga kura litaboreshwa, amesema wananchi waliofikisha umri wa miaka 18, wajitokeze kuandikishwa na wananchi waliobadili makazi, waende na wabadili taarifa zao. Mhe. Theresia amesema taarifa za  marekebisho kwa daftari la kupiga kura zitatolewa na mkurugenzi mtendaji wa wilaya.

Awali katika kikao hicho ndugu Emmanuel Mganga  na Bi, Julielth Daudi wamesema kijiji cha Laja na vijiji vya jirani vina adha ya  maji. Wamesema kijiji cha Laja kuna kisima ambacho kimechimbwa mda mrefu lakini kimeshindwa kutoa maji. Wananchi wamedai kijiji cha Laja kina josho la mifugo lakini nalo limeshindwa kufanya kazi kwa kukosa huduma ya maji ya kuweka katika josho.


Wananchi wakiwa wanasikiliza mKutano

Matangazo

  • Matokeo ya upimaji wa Kitaifa kidoto cha pili January 07, 2024
  • Halmashauri ya Wilaya ya Karatu Uchaguzi wa Wanafunzi wa kidato cha kwanza, 2024 December 18, 2023
  • Matokeo ya Darasa la Nne January 07, 2024
  • NAFASI ZA KAZI 2024 April 21, 2024
  • Angalia Zote

Taarifa Mpya

  • MILIONI 400 ZATOLEWA KARATU, KUJENGA MABWENI NA MADARASA EYASI SEKONDARI

    January 30, 2025
  • WASIMAMIZI WAASWA KUSIMAMIA VIAPO VYAO KUELEKEA UCHAGUZI WA SERIKALI ZA MITAA 2024.

    November 23, 2024
  • JESHI LA AKIBA MKAWE WAZALENDO KWA TAIFA

    November 23, 2024
  • HALMASHAURI YAZINDUA KITABU CHA MPANGO MKAKATI WA UKUSANYAJI MAPATO.

    November 19, 2024
  • Angalia Zote

Video

DC KOLIMBA ATATUA KERO TARAFA YA EYASI KARATU
Video Zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fursa za Uwekezaji

Viunganishi Linganifu

  • Tovuti ya Wizara ya Fedha na Mipango
  • Jamvi la Habari
  • Tovuti ya Tamisemi
  • Tovuti ya Serikali
  • Sekretarieti ya Ajira

World visitors tracker

world map hits counter

Visitors Counter

writingMasterThesis

Location Map

Wasiliana Nasi

    Karatu District Council

    Sanduku la Posta: P.O Box 190

    Simu: +255 272970648

    Simu ya Mkononi: 0754773947

    Barua Pepe: ded@karatudc.go.tz

Other Contacts

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Haki Miliki @ 2017 Halmashauri ya Wilaya ya Karatu.Haki zote zimehifadhiwa